Ajira za TAMISEMI 21,200 Kila Halmashauri Inaweza Kupata Nafasi 115 kama Zikigawiwa kwa Usawa

Ajira za TAMISEMI 21,200 Kila Halmashauri Inaweza Kupata Nafasi 115 kama Zikigawiwa kwa Usawa

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
MHE. EZRA CHIWELESA - AJIRA 21,200 KILA HALMASHAURI INAWEZA KUPATA WATUMISHI WAPYA 115 KAMA ZIGAWIWE KWA USAWA

Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Mhe. Eng. Ezra Chiwelesa ameunga mkono hoja na kuchangia katika bajeti ya Wizara ya Ofisi ya Rais - Utumishi na Utawala Bora.

Mhe. Chiwelesa amesisitiza uwazi na ugawaji sawa wa nafasi za ajira zinapotoka kwani kati ya Nafasi 21,200 zilitolewa na TAMISEMI kila Halmashauri inaweza kupata wafanyakazi wapya 115.

Mhe. Chiwelesa amesema Serikali itumie busara kuwaangalia vijana waliohitimu vyuo vya Utalii wenye umri zaidi ya miaka 25 ambao jeshi halikuwaajili kwa kigezo cha kuzidi miaka 25 kwani wanaujuzi na wazazi wao walitumia gharama kubwa kuwasomesha.

Mhe. Chiwelesa amesisitiza pia kuwa ajira za sekta zingine za TRA, TANESCO, BoT n.k pia ziwekwe wazi wakati wa mchakato wa kuwapata watumishi kama ilivyo kwa TAMISEMI. Kwani kumekuwa na tabia ya kuangalia undugu, ukabila na watoto wa viongozi katika sekta mbalimbali.
 

Attachments

  • CHIWELESA 19.MP4
    56.7 MB
  • WhatsApp Image 2023-04-19 at 15.44.08.jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-19 at 15.44.08.jpeg
    107 KB · Views: 14
Sasa shida iko wapi mkuu.

Hata hivohiyo ni kwa wastani bila shaka, maana kwa upande wa afya naona sio halmashauri zote zipo kwenye kanzi data. Unakuta mkoa mmojawa.wilaya 5 zipo 2 au 3 au 1 tu do kwa uwiano huo bado sio sahihi.
 
Inshort izo nafasi ni chache sana ukizingati na idadi ya vijana walioko mtaani.
 
Wakuu hizi nafasi inakuaje kwa wenye leseni ya zanzibar kwa upande wa afya mbona mfumo unawatema
 
Hiyo haitawezekanaz maana kuna mikoa mingine ina Halmashauri nyingi, sasa huwez kulinganisha mkoa wenye Halmashauri 7 na mwenye Halmashauri 3 eti wapate mgawo sawa
 
Hiyo haitawezekanaz maana kuna mikoa mingine ina Halmashauri nyingi, sasa huwez kulinganisha mkoa wenye Halmashauri 7 na mwenye Halmashauri 3 eti wapate mgawo sawa
Lakini idadi ya shule kila mkoa zinajulikana mkuu.
 
Inshort izo nafasi ni chache sana ukizingati na idadi ya vijana walioko mtaani.
Tamisemi inatakiwa iajiri kwa mwaka mara 2. Hebu fikiria waalimu wanastaafu anytime, yearly, miaka mitano hakukuwa na ajira, mashule yamejengwa karibu kila kata. Nashule shikizi na madarasa.

Udahili umekuwa ukiongezeka kila mwaka. Hao walimu wanaoajiri kidogo ivyo wana nia ya dhati kuinua elimu?
 
Back
Top Bottom