AJIRA ZA WALIMU: Safari hii hatutavumilia figisu figisu kwenye ajira ya walimu kama nyakati nyingine

AJIRA ZA WALIMU: Safari hii hatutavumilia figisu figisu kwenye ajira ya walimu kama nyakati nyingine

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Imekuwa ni kawaida kuona figisu figisu ikitawala katika ajira za walimu. Baadhi ya figisu figisu hizo ni kama ifuatavyo.

1. Kutangazwa kwa nafasi za walimu wa Physics na Hesabu lakini wakachaguliwa baadhi ya walimu wa biology na chemistr. Walimu wa chemistry na biology ambao hawakuomba wakaona wamepigwa chenga ya mwili.

2. Mwalimu mmoja jina lake kutoka zaidi ya mara mbili. Matukio ya namna hii yalikuwa kwenye idadi amb ayo si rahisi kuona kuwa ni bahati mbaya. Inaonekana kuna nafasi zimehifadhiwa kwa baadhi ya watu ambao hawakuwa na sifa za kuchukuliwa moja kwa moja.

3. Kuajiriwa walimu ambao wamemaliza chuo juzi wakati walimu waliohitimu miaka mingi iliyopita wa masomo hayo hayo wakiwa wameachwa.

ongezeeni zingine!

Tuseme mapema safari hii tutawekeana pingamizi mahakamani kama uozo kama huo utajirudia. Na ni lazima uwepo uwazi wa hali ya juu kuhusu vigezo vinavyopimika vitakavyotumika.

Kigezo kimoja kisichokuwa na upendeleo ni wa foleni kwa masomo husika. Yaani waliohitimu mwanzo wachaguliwe kwanza.

Hiyo itafanya waliobaki wawe na amani huku wakijua angalau nao wamesogea kwenye foleni. Lakini ukiajiri wahitimu wa hivi karibuni na kuwaacha wahitimu wa miaka ya nyuma kwa masomo yale yale inavunja moyo na kukatisha tamaa swana.

Wakubwa tunawaomba wasithubutu kusumbua watendaji kwa vimemo!! Ningeshauri mkubwa yeyote akisumbua na kimemo, utaratibu ufanyike wa kukianika hapa Jf na mitandao mingine ya kijamii.

Hiyo itakuwa ni adhabu kubwa sana kwake na tutamwomba mama amtengue!! Takukuru na vombo vingine vya dola iweni macho kwa hili.
 
Mpaka muda huu tayari wahitimu mshapigwa na kitu kizito kitambo sana. Imagine unaruhusiwa kutuma maombi, halafu nafasi inayohitajika unakuta ni moja tu! Huku waombaji mkiwa zaidi ya 20 - 100+ kwenye shule moja!!!!

Mwisho wa siku watachagua watu wao, na nyinyi mtashauriwa kuomba tena wakati mwingine. Kiufupi Tamisemi ni janja janja sana.
 
mwalimu acha stress unapanic sana mapema mbona tulia tamisemi ifanye kazi yake,vp kwani huko kweni mbuguni hadi leo bado hujapata kumiliki kitalu ya tanzanite uachane na ajira za walimu
 
Imekuwa ni kawaida kuona figisu figisu ikitawala katika ajira za walimu. Baadhi ya figisu figisu hizo ni kama ifuatavyo.
1. Kutangazwa kwa nafasi za walimu wa Physics na Hesabu lakini wakachaguliwa baadhi ya walimu wa biology na chemistr. Walimu wa chemistry na biology ambao hawakuomba wakaona wamepigwa chenga ya mwili.
2. Mwalimu mmoja jina lake kutoka zaidi ya mara mbili. Matukio ya namna hii yalikuwa kwenye idadi amb ayo si rahisi kuona kuwa ni bahati mbaya. Inaonekana kuna nafasi zimehifadhiwa kwa baadhi ya watu ambao hawakuwa na sifa za kuchukuliwa moja kwa moja.
3. Kuajiriwa walimu ambao wamemaliza chuo juzi wakati walimu waliohitimu miaka mingi iliyopita wa masomo hayo hayo wakiwa wameachwa.

ongezeeni zingine!

Tuseme mapema safari hii tutawekeana pingamizi mahakamani kama uozo kama huo utajirudia. Na ni lazima uwepo uwazi wa hali ya juu kuhusu vigezo vinavyopimika vitakavyotumika. Kigezo kimoja kisichokuwa na upendeleo ni wa foleni kwa masomo husika. Yaani waliohitimu mwanzo wachaguliwe kwanza. Hiyo itafanya waliobaki wawe na amani huku wakijua angalau nao wamesogea kwenye foleni. Lakini ukiajiri wahitimu wa hivi karibuni na kuwaacha wahitimu wa miaka ya nyuma kwa masomo yale yale inavunja moyo na kukatisha tamaa swana.
Wakubwa tunawaomba wasithubutu kusumbua watendaji kwa vimemo!! Ningeshauri mkubwa yeyote akisumbua na kimemo, utaratibu ufanyike wa kukianika hapa Jf na mitandao mingine ya kijamii. Hiyo itakuwa ni adhabu kubwa sana kwake na tutamwomba mama amtengue!! Takukuru na vombo vingine vya dola iweni macho kwa hili.
Wazo Lako ni zuri sana inatakiwa waanze kuchukua kwa kufuata miaka haileti sense unamuacha mhitimu wa 2016 unamchukua wa 2019 au wa 2020 mwenye sifa zile zile kama wa 2016 .Tamisemi chukueni watu kadri ya miaka waliyomaliza lasivyo watasahau ujuzi wao isitishe hao wanaowaambia wanajitolea si kweli hakuna kitu kama hicho katika kipindi kigumu kama hiki hakuna mhitimu yeyote anaweza acha shughuli za kujitafutia mkate wa kila siku eti awe anafundisha for free hizo supporting document kutoka kwa wakuu kwamba walikuwa wanajitolea sio valid ni fake
 
Kigezo cha kuajiri walimu kulingana na miaka waliyomaliza chuo ni kigezo cha kipumbavu.

Hili ni soko huria, kila mtu apambane kwa uwezo wake aajiriwe.

Yaani mwalimu amekaa anasubiri aajiriwe kulingana na mwaka aliomaliza chuo, mbona kada nyingine hawalalamiki kwamba wa hivi karibuni wanaajiriwa wa zamani wanaachwa?

Waalimu kazi kulia lia tu.
 
Ukweli machungu.

Lakini na sisi wana art tufikiriwe basi
 
Mtu yupo bize kulalamikia mshahara wa laki tano +kazi ngumu😀😀😀😀😀tuna safari ndefu Sana km taifa
 
Waweke kipaumbele kwa walimu wa elimu awali. Wanafunzi wwngi wanamaliza la Saba hawajui kusoma.
 
Umaskini umesimika mizizi watu wanataka kuganga njaa tu
Mtu yupo bize kulalamikia mshahara wa laki tano +kazi ngumu[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]tuna safari ndefu Sana km taifa
 
Kwa nini nyakati zingine mlivumilia na kwa nini safari hamtavumilia. Kitu gani kimekupa nguvu ya kutovumilia kama mwanzo
 
Kwa nini nyakati zingine mlivumilia na kwa nini safari hamtavumilia. Kitu gani kimekupa nguvu ya kutovumilia kama mwanzo
Uvumilivu una mwisho na tumepewa mbinu na ujasiri zaidi wa kupambania haki zetu. Kuna mtu ataadhirika safari hii lkama wakiendelea na utaratibu wa kupeana vimemo!! Uzuri mbinu zote walizokuwa wanatumia na majina ya wahusika yamefahamika!!
 
Back
Top Bottom