Tetesi: Akagera National Park ya Rwanda inavyochukua wanyama wa pori ya Burigi na Kimisi na kuwafungia kwenye fensi

Tetesi: Akagera National Park ya Rwanda inavyochukua wanyama wa pori ya Burigi na Kimisi na kuwafungia kwenye fensi

Hivi asili ya neno KAGERA ni mto au ni MAPORI?je kuna haja gani ya kuchochea.
Akagera="Ka mto"(mto mdogo) linatokana na neno "kugera" yaani kutiririka,naweza kukosolewa.Nirejee kwenye mada-Mimi ni mpenzi wa chaneli za Wanyama kwenye Kampuni kubwa ya huduma za ving'amuzi Afrika.Juma lililopita nikawa naangalia National Geographic(Wild) nikawa naiona hiyo Akagera ina Wanyama kama wa Serengeti (Copy and Paste) nikawa naangalia mazingira (Habitat?) waliyomo wale wanyama hayafanani kabisa na Africa Savannah,unaona kabisa wale wanyama wamepandikizwa!Kwenye Savannah za Africa ukifuatilia sana utaona mazingira mengi ya mbuga hizi ni ya brown kwa ajili ya kuficha wale wanyama wanaowinda wasionekane na ni tambarare.Akagera imekaa kama Gombe vile na ni greenish.Kwenye ile Documentary nilijua kabisa Rwanda kuna kitu anakitafuta (kukimbiza watalii kutoka TZ!) maana ana ndege nyingi za kutosha zinarandaranda hewani
 
Hii inaweza kuwa ni mada nzito sana ya kuanzia mwaka na ambayo kama watu wanafuatilia (na I know they do) watu wetu wa inteligensia (TISS na wa Jeshi) watakuwa wanaunda task force kuelekea pande hizo kabla ya mwisho wa wiki..

Itapendeza kama ndo hivyo, ila nadhani wanaeza kuwa wanajiandaa na kuzuia maandamano ya 26/April.......
 
Mkuu hatukatai kuwa wanyama huwa wanahama Serengeti na kwenda masai Mara Kenya ambapo uhamaji huo ni wa asili, tatizo la Rwanda ni kujenga fensi kwamba wameingia wasirudi tena Tanzania. Kenya hawajawazuia kurudi

Kwa hiyo hatuwezi kuyalinda hayo mapori mpaka tuyapandishe hadhi?
 
Documentary nilijua kabisa Rwanda kuna kitu anakitafuta (kukimbiza watalii kutoka TZ!) maana ana ndege nyingi za kutosha zinarandaranda hewani
Hivi kweeli?! Tuna hifadhi kama Selou ambayo ni kubwa duniani,tuna Serengeti..give me a break..tunaogopa Akagera National park ya Rwanda?.
 
Hivi kweeli?! Tuna hifadhi kama Selou ambayo ni kubwa duniani,tuna Serengeti..give me a break..tunaogopa Akagera National park ya Rwanda.
Hata sh. 100/=haiwezi kamilika bila sh. 1/= hivyo usidharau hao wachache wanao chukuliwa tuwazuie tuwahami hao wanyama.
 
Hivi asili ya neno KAGERA ni mto au ni MAPORI?je kuna haja gani ya kuchochea.

Huyu mtoa uzi anatumia akili tu sio "facts", Kagera kwa lugha ya kihaya kutiririka kwa maji. Akagera maana yake mto mdogo "a small river" kwa watu wa uganda, rwanda na burundi kuna baadhi ya maneno yanaingiliana na watu wa kagera, Simiyu, Shinyanga , hasa kanda ya ziwa kwa ujumla. Lakini sio kweli kwamba Akagera National Park ya Rwanda inaitwa hivyo kwa ujanja ili kupata advantage Mkoa wa Kagera.

Maelezo yangu hapo juu yasitafsiliwe kana kwamba ninapinga kuwa Rwanda hawafungii wanyama waliovuka nyakati zile kwenye uzio " fance". Maana hata mimi nilishakuwa nazo la kutafiti mazingira yanayovutia wanyama kwenda masai mara Kenya na baadae kurudi Tanzania ili wakiisha kuja huku tuwafungie wasirudi Kenya. Nadhani lilikuwa wazo la kijinga au la ubinafsi, kwani kuna madhara gani wote tukipata kutokana na riziki aliyotupa sisi waja wake ( wakenya na watanzania) Subuana?

Wanyarwanda watakuwa wametenda kitendo cha kijinga na hiyo ni kuharibu ecologia ya dunia kwa kuzuia asili kutawala. Kama wanafanya hivyo, sisi tuna faida kubwa moja, kuwa wanyama wetu waliosalia na kwa kuwa wanazaliana basi hawataingia Rwanda maana uzio unazuia pande mbili. Ni hayo tu.
 
Hio hifadhi ya AKAGERA imeanzishwa Mwaka 1934 hizi nchi zote hazijapata hata uhuru afu unasema eti jina lilibuniwa kuwadanganya wazungu wadhani eti iko Kagera hahah,imekaa Ki SHITHOLE story.
 
Back
Top Bottom