Mucho Mucho
JF-Expert Member
- Mar 7, 2012
- 245
- 256
Yuko sahihi...inafungwa na pesa inakua tranferred to BOT..kwa maelekezo toka mahakama,km kuna pesa za biashara zitakuja through that account,either zitarudishwa zilipotoka or bank itazizuia na kuwapata taarifa..ambapo idhini tena ya mahama itahitajika.Kumbe inawezekana.... Leo mhudumu pale mahakamani anasema eti ni lazima ifungwe
usifikiri kila kitu unapigwa...utaishi maisha magumu.Kuna makarani hakuna kitu kichwani, wanataka kukutengenezea ugumu utoe noti
Ni lazima uwafungulie account, siku hizi kufunguwa account ni dakija tano tu.Asante sana maelezo yako yanaeleweka.
Na je kama baadhi ya wanufaika kama wazazi ambao ni wazee wa kijijini hawana account bank??
Ni gazeti la uhuru au lolote la serikali?Ni lazima uwafungulie account, siku hizi kufunguwa account ni dakija tano tu.
Hizo pesa hapewi mtu yeyote mkononi, wanufaika wote wanaingiziwa kwenye account.
Subiri mkipata fomu za mgawanyo wa pesa mahakamani, zile fomu sasa wafuate kijijini wafungulie account then utawajizia fomu watasaini halafu watakaa wanasubili tu mzigo wao usome kwenye account.
Wakati wa shauri utamueleza uhalisia hakimu kwamba kuna wazee afya haziwaruhusu kufika mahakamani kwahiyo mnawawakilisha nyinyi chini ya hati ya kiapo.
Halafu kwenye process nilisahau mkishafunguwa mirathi inabidi muende kuitangaza kwenye gazeti la uhuru na lile gazeti likitoka mkate kile kipande cha tangazo unakileta mahakamani kinakaa kwenye file.
Siyo lazima kuwaita, unaweza ukasubiri stage mtakayopewa fomu za kujaza mgao wa pesa ukaenda wewe na fomu ukawafungulia account ukawasainisha fomu unaondoka na copy tu za kadi zao za bank, huna haja ya kuwasumbuwa.Sawa ngoja niwaite wafungue account
Ni gazeti la uhuru mkuu, weka siasa pembeni, ccm ni jinamizi ambalo haliwezi kuwaachia Watanzania leo au kesho.Ni gazeti la uhuru au lolote la serikali?
Asante kwa elimu mkuu ila hiyo kaa kimya yako imekaa kishari sana. Sio ugomvi ndugu.Kama hujui kitu kaa kimya, pesa ya marehemu account ikishafungwa na branch yake pesa yote inaingizwa kwenye account ya mahakama, then mkishajaza fomu za mahakama za wanufaika na mgao wao mahakama ndio inazigawa zile pesa kama mlivyojaza kwenye fomu mgawanyo direct kila mnufaika anaingiziwa kwenye account yake.
Hakuna wa kupewa pesa zote eti yeye ndio atawagawia wenzanke.
Ila kwenye mgao mjane lazima apate mgao mkubwa zaidi kuliko watoto ndio busara inataka hivyo mahakama inaawachia wenyewe mpange mgao wenu.
Mideko upo sahihi na huu ndiyo utaratibu lakini sio kuhamishiwa kwenye account ya mahakamaPesa haingii mahakamani isipokuwa mirathi ikitoka ikiwa imekubaliwa , bank wanatoa chek ya balance iliyopo kwenye account ya marehemu , chek haiwez kutoa pesa mpka igongwe muhuri wa mahakama husika iliyosimamia hiyo mirathi, halafu inarudishwa bank, pesa zitatolewa ikiwa warithi wote mliotajwa kwenye mirath mkiwepo bank kaona maelekezo mengi naona kaamua kumfupishia hapo.
Uhuru siyo gazeti la serikali ni la ccmNi gazeti la uhuru au lolote la serikali?
Shukran pia kwa elimuHuwezi kuanzia benk unaenda kwanza na hizo documents mahakamani na baada ya mahakama kukupitisha kama msimamizi wa mirathi ndio wanakupa barua ya utambulisho unaenda nayo bank
Unaomba Ushauri Nusu nusu....Asanteni wakuu...
Haulazimiki kuwa gazeti ka Uhuru peke yake,mimi mwaka juzi nilipeleka katika gazeti la Mwananchi ofisi zao zipo pale Jmall building,gazeti lolote lenye wigo mpana kwenye usambazajiNi gazeti la uhuru mkuu, weka siasa pembeni, ccm ni jinamizi ambalo haliwezi kuwaachia Watanzania leo au kesho.
Dr matola naomba msaada wako nna changamoto kama hii naomba nitafute 0685280541Kuna members wamekupa maelezo sahihi ila ngoja nikunyooshee kidogo.
Je wewe ni mnufaika wa hiyo mirathi, kama ndio je hizo pending transaction zinatalajiwa kuingizwa lini kwenye hiyo account?
Kama ni hivi karibuni subilini msifunguwe mirathi kwanza pesa iingizwe.
Pesa ikishaingizwa mnafunguwa mirathi ambapo utaratibu ni kwenda mahakamani na mukhtasari wa kikao cha familia ambao mmeteuwa msimamizi wa mirathi, mukhutasari ugongwe muhuri wa serikali ya mtaa, ni vizuri mkiandika kwa mkono msichape tafuteni mwanafamilia mwenye muandiko mzuri atawaandikia.
Mkishafunguwa mirathi mahakamani kama hakuna malumbano yoyote ya kifamilia kugombea chochote shauri linapelekwa faster na msimamizi wa Mirathi anateuliwa na mahakama na anapewa barua ya utambulisho wa msimamizi wa mirathi.
Sasa hapo ndipo mahakama itaandika barua kwenda bank husika kufunga account ya/za marehemu na kuleta hesabu ya pesa yote kwenye account ya mahakama, hii barua anapeleka msimamizi wa mirathi.
Baada ya hesabu kupokelewa kwenye account ya mahakama, msimamizi wa mirathi atapewa fomu ya idadi ya wanufaika/ warithi ajaze mgawanyo wa pesa yote ya marehemu kwa wanufaika bila kuzidisha hesabu wala kupunguza kwa kile kilichopo kwenye account.
Mkishakamilisha kujaza hizo form na kuzirudisha mahakamani zikiwemo copy za card zenu za bank basi kifuatacho ni kusubiri kwa muda kama wa mwezi mmoja utasikia msg kwenye simu muhamala umeshasoma kwenye account zenu simple as that.
Kama kuna vitu sensitive unaona vinakusumbuwa nicheck private nitakupa muongozo wote, hakuna kitu kinaniuma kama mtu anafariki halafu pesa zake zinapotea kwa sababu ya kukosa backup tu na baadaye familia inaishi kwa dhiki wakati marehemu aliwaandalia maisha na future nzuri.
Ok.Dr matola naomba msaada wako nna changamoto kama hii naomba nitafute 0685280541