BLACK MOVEMENT
JF-Expert Member
- Mar 11, 2020
- 4,548
- 11,901
- Thread starter
-
- #181
Hao wanatetea hadi MaviCha Ajabu huyo alieandika Hapo ni mmojawapo wa kijana ambaye hana Ajira ila ndio wa kwanza kuwakandia vijana wenzake sijui kichwan chake kimejaa funza watupu Sana huyu choice variable ni miongoni wa Chawa asie na Faida Wala kutambulika
Kama kazi huko hazipo_Waarabu na wazenji hawatofautiani tabia kwenye ubaguzi. Yet mtu anatoka bongo anaenda kufanya ubeki 3 gulf countries😁 ni vichekesho sana.
Hapa bongo kama hunipeleki Nordic Countries au Canada bado hujanitoa humu. Siwezi kwenda kufanya kazi na watu wenye roho za kimasikini.
Bora nitulie homeKama kazi huko hazipo_
Mmoja ni Dokta....mwingine ni nani😇😇😇acha kifananisha visivyofananishwa.View attachment 3179827
Bahamas wanaenda fanya kazi, sisi tuendelee na mijadala ya Mbowe na Lisu kutwa nzima humu, tunakwa mno
Kazi za kubeba boxWatanzania wapo Poland na KINGEREZA hawajui Wanapiga kazi, wanangu wengine walikua Ukraine(kabla ya vita) na English hawajui. Ulaya ukilitoa nchi chache zinazo zungumza KINGEREZA nchi zilizo Baki hawajui English, English yao imejaa ubabaifu kama bongo tu. Ulaya kama unaenda Kwa kazi za nguvu sio lazima uwe na KINGEREZA kiingii cha kuombea maji tu kinatosha.
Anakera sana huyu kima na mazoba wenzake , Tanzania hii leo hii hata ukiitisha usahili wa kazi za ovyo kama ubeki tatu , utapata maelfu na probably Malaki ya watu na graduates wa vyuo vikuu jobless humo wengi wa kutosha ,tena wamemaliza miaka mingi huko nyuma na ni jobless mpaka leoCha Ajabu huyo alieandika Hapo ni mmojawapo wa kijana ambaye hana Ajira ila ndio wa kwanza kuwakandia vijana wenzake sijui kichwan chake kimejaa funza watupu Sana huyu choice variable ni miongoni wa Chawa asie na Faida Wala kutambulika
Wanasiasa wasipotiwa jamba jamba na wao wanabweteka Vijana wa GenZ Kenya waliligundua hilo.Wako busy kubet
Cha msingi maokoto.Kazi za kubeba box
KabisaWanasiasa wasipotiwa jamba jamba na wao wanabweteka Vijana wa GenZ Kenya waliligundua hilo.
Maelezo marefu lakini umeandika upuuzi mtupu! Hiyo paragraph ya mwisho ndo tatizo la Tanzania na sio huo upuuzi ulioandika hapo juu kiasi cha kujiona wewe ndo una akili sana! Mfano tu weka tu tangazo kuhusu DV Lottery Program ambayo hulipi hata senti 5 uone watu watakavyoponda. Au na hiyo ni hadi hadi balozi ziwatangazie Watanzania? Btw, ni Mtanzania gani mwenye uwezo wa kuanzisha agency ambae hafahamu kwamba huko Arabuni kuna kazi za aina mbalimbali zikiwemo skilled and non-skilled labors?! Nimetoa mfano mdogo sana; wa well established agencies hata kwa ajili ya wafanyakazi wa ndani TZ! Hilo nalo ni hadi serikali itoe matangazo?Unaonekana una uwezo mdogo wa kufikiri, Tanzania tuna balozi ngapi zipo Tanzania hapa za Nchi nyingi? Waziri anashindwa kwenda kuuliza huko kwenu Kuna fursa gani japo vijana kadhaa waende wakapate Kazi ? kupunguza wimbi la vijana wasio na Ajira kama Nchi imeshindwa kutengeneza mazingira mazuri ya kuwapa Ajira walio na vigezo Kuna ubaya gani wakaenda huko nje ili wawekeze Tanzania.. Tena hakuna kitu kizuri kama serikalini ikawa ndio imekudhamini sababu sio rahisi kudhulumiwa maslahi Yako
Sasa mnataka vijana wabaki mtaani wanabanana mnafurahia mnappita Kazi zenye uhitaji watu 500 wanakuja watu 9000 kwenye usaili.
Ubinafsi Roho za Chuki kuwa na vigezo wasio na Upeo Viongozi wenye uwezo mdogo kabisa tunasikitika Sana wanasiasa wenye uwezo mdogo ndio wanapewa dhamana ya kuongoza Raia
Tuna balozi nyingi hapa Germany, finland, U.K , UAE wao wameshindwa vipi? Kuna balozi wapo mtandaoni kuandika sijui "quotes" waonekane wanabusara ujinga mtupu .
.
Tukiwa Nje ya Nchi unakutana na wakenya na nchi zingine unajiuliza Tanzania Tatizo nini?
Mtasingizia Lugha huo ni Uongo nimetembea Nchi nyingi Lugha ya kiingereza ni baadhi ya maeneo tu wengi wao Lugha hawajui Sana maana inafundishika na Kuna maeneo mengine wanatumia wengi wao waliopo hapo Poland, German , Luxembourg, Switzerland, n.k English siyo lugha ya kwanza Kuzungumza
Kaa fikiria angalia viongozi wenye hiyo dhamana wanauwezo kweli? Wao furaha yao kukaa kwenye hizo gari kula posho kununua magoli na kusuburia uchaguzi ufike waende wakagalegali kwenye mchanga kuomba Kura vijana ambao ni 23-35 wengi hawana Ajira wengi wao wanaamua kujiajiri katika bet na kushabikia simba na yanga kufanya parade
Vijana nawashauri pia muwe mnamoyo wa kusaka fursa Nje zenye ujuzi na zisizo na ujuzi vijana kadhaa nimekutana nao Netherlands, Germany, Poland USA lakini sio wengi kama wenzetu.. tumieni mitandao vizuri
Tuanzie hapo sasa- kwani hatuwezi? Jibu ni kwamba tunaweza! Sasa tatizo lipo wapi? Jibu simple: Watanzania tumekuwa wazito sana kuchangamkia fursa hususani za nje! Mfano mzuri fuatilia tu mijadala kuhusu Green Card lotteries halafu angalia ni Watanzania wangapi watachukulia hilo suala positive! Ukienda Dubai na Qatar kwa mfano, kuna Wakenya kibao na wala hawajaenda kwa mgongo wa serikali.Kwani sisi hatuwezi kuwa na Agencies?
pia ana uwezo mdogo sana anatembelea jina la Baba yakeNaamini Rizi hana hata wazo la kusaidia vijana kupata ajira...yani wazo tu hana yeye anawaza namna nzuri ya kutumbua mafedha aliyoyapata kwenye nchi hii basi.
serikali ya Kenya ina hadi mikataba na hizo Serikali, je Tanzania wana mikata naoTuanzie hapo sasa- kwani hatuwezi? Jibu ni kwamba tunaweza! Sasa tatizo lipo wapi? Jibu simple: Watanzania tumekuwa wazito sana kuchangamkia fursa hususani za nje! Mfano mzuri fuatilia tu mijadala kuhusu Green Card lotteries halafu angalia ni Watanzania wangapi watachukulia hilo suala positive! Ukienda Dubai na Qatar kwa mfano, kuna Wakenya kibao na wala hawajaenda kwa mgongo wa serikali.
Wakenya wanatafutiwa pia, Ruto mwenyewe anawatafutia, Je Serikali ya Tanzania inawatafutia?Maelezo marefu lakini umeandika takataka tupu! Ungekuwa na akili kama unavyojaribu kudanganya wazazi wako na wajinga wenzako tayari ungefahamu uwepo wa fursa zilizopo sehemu mbalimbali duniani bila kusubiri ubalozi huku ukijaribu kushindana na ukweli kwamba Wabongo sio watu wa kutafuta fursa hususani za nje na wengi wao wana akili kama zako! Mfano tu weka tu tangazo kuhusu DV Lottery Program uone watu watakavyopenda. Au hadi hiyo hadi balozi iwaambie?! Btw, ni mara ngapi serikali imekuwa ikizungumzia fursa zilizopo arabuni au unataka kila Mtanzania atumie barua kuambiwa?!
Hiyo ya Ruto unayoisema wewe ni kwavile ulimsikia hivi majuzi lakini Wakenya wameanza kwenda huko miaka mingi sana, na ni Mawakala ndio wanawapeleka huko na sio serikali. Lakini kwa upande mwingine, Wakenya individually ni watu wa kutafuta fursa kuliko Watanzania. Kinyume chake Watanzania ujuaji mwingi. Subiri miezi miwili kisha njoo na id nyingine kisha tangaza fursa zilizopo kwenye hizo nchi na iwe kama survey tu kufahamu mentality ya Wabongo!!Wakenya wanatafutiwa pia, Ruto mwenyewe anawatafutia, Je Serikali ya Tanzania inawatafutia?
Ni rahisi zaidi kupiga picha na yesu kuliko kupata passport bongo!!Kupata passport Bongo, utazungushwa sana, zile njoo kesho zinakuwa nyingi
Hiyo mikataba ilianza baada ya serikali ya Kenya kuona kile ambacho huwa kinawakuta hata Watanzania wachache wanaoenda huko; yaani unyanyasaji. Lakini lingine tunalojisahaulisha, Wakenya ni watu wa kutafuta sana fursa nje ya nchi compared na Wa-TZ na wala hawakusubiri serikali. Matokeo yake wamejenga credibility kubwa sana nje ya nchi ukilinganisha na Watanzania na ndo maana hata kama agency ni middle east based, wataenda Kenya ambako tayari wana historia na Kenyans.serikali ya Kenya ina hadi mikataba na hizo Serikali, je Tanzania wana mikata nao