Kutoa sarafu ya nchi ambayo ni Shilingi ya Tanzania
Kusimamia na kudhibiti mabenki na taasisi za fedha
Kusimamia na kudhibiti mifumo ya malipo nchini.
Kuhifadhi akiba ya nchi ikiwemo fedha za kigeni
Benki ya Serikali
Benki ya Mabenki; na
Kutoa ushauri juu ya masuala ya uchumi na fedha kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Dola ya Kimarekani ni fedha ya kigeni ambayo hutumika kwa miamala ya kimataifa kwa karibu asilimia 85 katika kuagiza bidhaa nje ya nchi.
Ukweli ni upi juu ya kukauka kwa dola ya kimarekai pamoja na shilingi ya Tanzania Kenki Kuu
Tarehe 16, 08, 2023 Tanzania leaks walichapisha habari kupitia mtandao wa Twitter kuwa wana taarifa za uhakika kuwa Benki ya Tanzania imekaukiwa dola na shilingi.
Benki Kuu ya Tanzania tarehe 18, 08, 2023 imekanusha kupitia mtandao wa twitter juu ya madai kuwa imekaukiwa na dola kwa kuandika kuwa huo ni uongo na unapaswa kupuuzwa.
Julai 17 2023, Beni Kuu ya Tanzania kupia kwa Gavana wa Benki Kuu, Bw. Emmanuel Tutuba,ilikirikuwepo kwa upungufu wa Dola za Kimarekani huku ikiwatoa hofu watanzania kuwa uhaba huo haujafikia kiasi cha kuleta hofu.
JamiiForums, imethibitisha kuwa taarifa ya kukauka kwa dola za Kimarekani katika benki Kuu ya Tanzania si ya kweli, na kwamba kilichopo nchini ni upungufu(uhaba) wa Dola na si kukauka kabisa.
Mwanamke sio wa kuupa uongozi wa nchi .yeye kakuta kuna mahela yamejaa kayatapanya huku na kwel akawagawia wezi ,watu wakashangilia eti nani kama mama sass kipo wapi
Jana nikwenda tawi la bank fulani ambapo nina nina account hapo nilikuwa na invoice kutoka China kuna vitu nilitaka kununua.Nikaambiwa kuna watu wapo kwenye foleni ya kupata dola toka juzi.Kwa siku hilo Tawi la hiyo bank wanaruhusiwa na Hazina,kutoa mwisho dola elfu mbili.Kama naweza na mimi nipange foleni au niandike barua nipate kibali toka hazina,kama jambo langu ni dharura🚶🏃♂