Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 33,679
- 49,841
Ulishawahi kujiuliza, kwa nini ukienda dukani unaweza ukakuta kitu cha shilingi 50, 100, 200 n.k?
Je hivyo vitu vinatoka wapi, ni kiwandani au ni mtu anajitengenezea? Mfano kuna biskuti, pipi, jojo, nyembe, pulizo n.k
Ukipata jibu, utagundua vingine vinatoka viwandani, na hivyo viwanda vimewaajiri wasomi mbali mbali; na uuzwaji wa hivyo vitu kwa bei ndogo ndogo ya shilingi 50 n.k ndio vinavyowalipa wale waajiriwa wenye digrii zao mishahara.
Kwa mazingira hayo sasa; wewe mpambanaji unatakiwa uamke, anzisha na wewe bidhaa zako zionekane kwenye maduka mbali mbali; lasivyo utaajiriwa na kuwa mtumwa mpaka unakufa.
Unaweza kuanza kiutani utani tu; mfano unaweza kutafuta maduka 20 n.k, hao ukawa unawapelekea bidhaa yako, mfano karanga zilizokaangwa na kuwekwa kwenye pakti, baada ya siku mbili tatu unazungukia mauzo.
Bahati nzuri biashara kama hiyo haiitaji mtaji mkubwa; ni wewe kuweka aibu chini na kuchapa kazi.
Haya kazi kwenu wapambanaji.
Je hivyo vitu vinatoka wapi, ni kiwandani au ni mtu anajitengenezea? Mfano kuna biskuti, pipi, jojo, nyembe, pulizo n.k
Ukipata jibu, utagundua vingine vinatoka viwandani, na hivyo viwanda vimewaajiri wasomi mbali mbali; na uuzwaji wa hivyo vitu kwa bei ndogo ndogo ya shilingi 50 n.k ndio vinavyowalipa wale waajiriwa wenye digrii zao mishahara.
Kwa mazingira hayo sasa; wewe mpambanaji unatakiwa uamke, anzisha na wewe bidhaa zako zionekane kwenye maduka mbali mbali; lasivyo utaajiriwa na kuwa mtumwa mpaka unakufa.
Unaweza kuanza kiutani utani tu; mfano unaweza kutafuta maduka 20 n.k, hao ukawa unawapelekea bidhaa yako, mfano karanga zilizokaangwa na kuwekwa kwenye pakti, baada ya siku mbili tatu unazungukia mauzo.
Bahati nzuri biashara kama hiyo haiitaji mtaji mkubwa; ni wewe kuweka aibu chini na kuchapa kazi.
Haya kazi kwenu wapambanaji.