Kama kuna kitu miye nadharau hapa Tz ni mwanamichezo. Hata mcheza bao, karata na draft. Namdharau. Badala ya mazoezi heavy na akili nyingi watu wanahama nyumbani wanahamia Mlingotini na Pemba ati kusindikwa. Sijui wamekuwa nyanya au nyama!! Jamani, pigeni hadithi na kina Kanu na Drogba. Wawaeleze siri ya mafanikio yao.
Mnatishwa na "vijini" vya Akilimali. Mnaacha kutafuta wachezaji wenye kujituma wakiwa uanjani mnawategemea watumainia hirizi. Niliachaga kucheza mpira tangu nikiwa chuoni kwa sababu tu kocha aliniletea hirizi ati niivae. Kwa sababu nilikuwa nampenda sana kocha nikaona nisimuudhi. Kuivaa tu, hata kabla ya half time, mguu ukavunjwa mara 2. Nikajuta kuivaa hirizi yake.
Tujiulize. huko Pemba ka kuna ndumba ya mpira, kumetoka timu ngapi bora?? Huko mlingotini Bwagamoyo, timu yao ya wilaya ni ipi?? Acheni uzuzu, piga zoezi heavy na soma tricks za mchezo, vaa moyo wa kujituma ukijua kuwa michezo ni kazi na ajira ka vile Accounts au IT. Kalaghabao na ubozi wenyu wanamichezo wenzangu. Msinichukie ni mawazo yangu tu wala sijamtukana mtu.