Albert Chalamila: Nimeandika wosia nikifa nizikwe Kiislamu

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema miongoni mwa mambo ambayo anayapenda ni kuhusu jinsi waumini wa Dini ya Kiislam wanavyowazika wapendwa wao na kueleza kuwa ameandika wosia kwamba atakapofariki, anataka kuzikwa kama Waislam wanavyozikwa.

Your browser is not able to display this video.

 
Mkuu wa Dar amesema anaupenda uislam na akifa ameandika wasia azikwe kiislamu.
Ameyasema hayo hivi karibuni jijini Dar Es salaam.
Video inakua hivi punde
Afande Sele 'Seleman Msindi' mwislamu alisema akizikwa azikwe kiasili yaan apigwe moto baadae akili zilipomrudi akabadirisha mtazamo, kwa hio mkuu wa Mkoa bwana Alubati Chalamila na yeye tunampa muda akili zikimrudia ataeleza vizuri kwa sasa bado muda wake haujafika na hafi kesho wala kesho kutwa
 
Hafi kesho wala kesho kutwa? Anatumia pumzi za ulaya na sio za Allah?
 
Mimi kama Mkristu naifuta kabisa hiyo kauli yake, kwa sababu hakufanya hivyo kwa hiari yake. Bila shaka ameshinikizwa ama moja kwa moja au mazingira yamemlazimisha kufanya hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…