Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
- Thread starter
- #21
Mhindi akajibu, ‘Seyid yangu, sisemi kwa umbo lake la nje ila kwa manufaa yake ninayoyapata. Kazi yangu ni kumpanda tu na kama nataka kwenda mahali fulani, hata kama ni mbali, kwa dakika chache tu hujiona nimefika. Basi Seyid yangu, haya ndiyo yanayomfanya farasi huyu kuwa wa ajabu kabisa, na kama kwa enzi yako utaniruhusu kumpanda, utaweza kusadikisha mwenyewe.’
Huyu Mfalme wa Ajemi aliyekuwa akipendezwa na kila jambo la ajabu, wala naye hakupata kuona farasi wa namna ile, akamwambia Mhindi ampande farasi, ili apate kuonyesha manufaa yake, Mara akampanda na kumwuliza mtafme wapi anakotaka kumtuma. Mfalme akamwambia, ‘Wauona mlima ule-e?’ Akaonyesha kilele cha mlima mkubwa mno uliopanda juu mawinguni, yapata mwendo wa saa kasorobo kutoka pale Shirazi mpaka kufika huko. ‘Nenda kaniletee tawi la mikindu inayoota chini yake.’
Mfalme alipotamka maneno haya yule Mhindi akaizungusha sukurubu iliyowekwa juu ya shingo ya farasi karibu na tandiko, mara akapaa hewani kama umeme asionekane tena. Muda wa robo saa Mhindi akaonekana anarudi, amechukua tawi la mkindu mkononi mwake, akimteremsha chini farasi wake karibu na kiti cha enzi, akashuka na kuliweka lile tawi mbele ya mfalme.
Sasa mfalme akasadikisha ule mwendo wa ajabu wa yule farasi na akatamani awe naye yeye, na hivyo ndivyo ilivyokuwa, maana yule Mhindi alikuwa tayari kumwuza, na mfalme naye alikuwa akimtazamatazama farasi kama aleyekwisha kumnunua.
Mwisho akamwambia Mhindi, ‘Kwa umbo lake la nje tu, sikumdhania kuwa ni mnyama wa manufaa jinsi hii, nami nimefurahi sana kwa kunionyesha kosa langu, na ikiwa utaniuzia sema bei yako. ‘
Mhindi akajibu, ‘Seyid yangu, sina shaka kuwa mfalme mwenye hekima kama wewe atanifanyia haki kwa farasi wangu baada ya kuona uhodari wake kwa mara ya kwanza, na mimi sikwenda mbali sana kwa kufikiri kuwa labda utampenda awe wako. Basi ni afadhali nimtoe zawadi, na hivyo nitakupa wewe bwana wangu kwa sharti moja. Farasi huyu sikumfanya mimi ila nilipewa na mtu aliyembuni, kwa kubadilishana na binti yangu, tena kwa kuniapisha kiapo kuwa sitotengana naye vivi hivi tu, ila kwa kitu cha thamani sawasawa.’
Mfalme akamwambia, ‘Taja cho chote utakacho. Milki yangu ni kubwa yenye miji mikubwa mikubwa mizuri. Chagua uupendao, uutawale mpaka mwisho wa maisha yako.’
Mhindi hakuona ukarimu huo unatosha kama vile alivyoona mfalme. Akajibu, ‘Seyid yangu, ninakushukuru sana sana kwa kunipa utawala, ila nakusihi usinikasirikie, ikiwa nasema kuwa naweza kukutolea farasi wangu kwa kubadilishana na binti yako.’
Wafuasi wa mfalme waliposikia maneno haya wakaangua vicheko wakacheka, na Feroz Shah mwana wa mfalme, ambaye, ndiye mrithi wake, akakasirika sana kwa ufedhuli kama ule. Lakini mfalme alifikiri kuwa haitamwia thamani kubwa kutokana na binti yake kwa kupata mchezo mzuri kama ule. Basi wakati mfalme alipokuwa akisitasita kujibu, mwanawe akaingilia kati akasema, ‘Seyid yangu, afadhali usifanye haraka kumjibu bazazi huyu fidhuli. Fikiri jinsi damu ya babu zako itakavochanganyika na kuwa duni.’
Mfalme akajibu, ‘Mwanangu, najua wasema ndivyo, lakini naona huitambui thamani ya farasi, na kama nikiyakataa kweli mashauri ya Mhindi, ataondoka aende akamwambie mfalme mwingine maneno haya haya, nami hivyo nitaona kushindwa nikimfikiri mtu ye yote mwingine kuipata hii Ajabu ya Saba ya Dunia.
Kwa hakika sisemi kuwa nitayakubali masharti yake, lakini naye pengine huenda akatoa sharti ingine, basi kwa kitambo hiki tulicho hapa ningependa umwangalie farasi huyu, na kwa ruhusa ya mwenyewe, umjaribu mwendo wake.’
Yule Mhindi aliyekuwa akisikia maneno haya ya mfalme akaona iko dalili ya kupata vile alivyokusudia, akafurahi na kuridhia kwa yale aliyotaka mfalme. Akaja kumsaidia mwana wa mfalme apate kupanda farasi na kumwonyesha namna ya kumwendesha, Lakini kabla hajamaliza kumwonyesha yule kijana akaizungusha Sukurubu, na mara ile ile farasi akapaa hewani akawa haonekani tena.
Watu wote waliokuwapo kuangalia wakakaa kungojea kwa muda, wakitaraji kuwa pengine huenda mara wakamwona kwa mbali akirudi, hata mwisho yule Mhindi mwenyewe akawa na hofu. Ndipo akaenda akajiangusha kifudifudi mbele ya kiti cha enzi, na kumwambia mfalme, ‘Seyid yangu, bila shaka umeona kuwa mwanao hakufanya subira, hakunidirikisha kumwambia yote yaliyokuwa haja kumwambia ili aweze kurudi mahali alipoondokea. Basi nakusihi usiniadhibishe; kwani hilo si kosa langu, wala usinipatilize kwa mashaka yo yote yátakayompata.’
Kwa hofu kuu aliyokuwa nayo mfalme akasema kwa hasira ‘Lakini kwa nini hukumwita arudi wakati ulipomwona anatokomea?’
Mhindi akajibu, ‘Mwendo wake wa kasi ulinitia bumbuazi hata kama ningalimwita hangalisikia. Lakini natutumai kuwa atafahamu kuizungusha sukurubu ya pili, ambayo itamfanya farasi kushuka chini.’
Mfalme akasema, ‘Ehe! Kama akifanya hivyo, kitu gani kitakachomzuia farasi hata asishukie baharini, au kumwangusha majabalini na kuvunjika kenyekenye?’
Mhindi akajibu, ‘Usiwe na hofu, bwana wangu, maana yule farasi ana akili ya kuvuka bahari, na kumpeleka mpandaji wake popote atakapo kwenda.’
Mfalme akamjibu, ‘Vema basi, lakini fahamu kuwa asiporudi tena kwa muda wa miezi mitatu, wala haniletei habari yo yote kuwa ni salama, maisha yako yatapotea.’ Kuisha kusema hivi akaamuru askari wake kumkamata Mhindi wamtie gerezani.
Kwa kitambo hiki chote, yule Feroz Shah mwana wa mfalme alikuwa amepaa hewani kwa furaha, na kwa muda wa saa nzima alizidı kupaa juu hata ile milima mikubwa mikubwa ilionekana sawasawa na tambarare. Kisha halafu akawaza kuwa sasa nai wakati wa kushuka chini, na kufanya hivyo ilimlazimu azungushe sukurubu kuelekeza njia, lakini kwa bumbuazi na hofu aliyokuwa nayo hakuthubutu hata kidogo. Ndipo alipokumbuka kuwa hakufanya subira kuambiwa namna ya kushuka chini tena, mradi akajiona hatari imemsimamia. Kwa bahati akili zake hazikumpotea, ndipo akaanza kuitazama shingo ya farasi kwa makini sana, hata mwisho kwa furaha yake kuu akagundua kigingi kidogo, kidogo sana kuliko kile kingine, karibu na sikio la upande wa kulia. Hata alipokizungusha, mara akajiona anashuka chini pole pole kuliko vile alivyopanda.
Wakati huo ulikuwa giza, na kwa vile ambavyo mwana wa mfalme hakuweza kuona kitu, alimwachilia farasi ajiongoze mwenyewe. Ilikuwa usiku wa manane Feroz Shah mwana wa mfalme alapogusa chini, amechoka, hasa kwa vile alivyokua hajala kitu tangu asubuhi.
Basi aliposhuka juu ya farasi, jambo la kwanza alilofanya ni kupatambua mahali alipo, lakini kwa ajili ya lile giza kuu hakuweza kutambua kitu ila alijiona yuko juu sakafuni kwenye jumba kubwa mno, lenye kuzungushwa viguzo vya vya nawe ya marmar. Katika pembe ya sakafu hiyo kulikuwa na kilango kinachofungulia vidaraja vya ngazi inayoendea chini ndani ya nyumba.
Huyu Mfalme wa Ajemi aliyekuwa akipendezwa na kila jambo la ajabu, wala naye hakupata kuona farasi wa namna ile, akamwambia Mhindi ampande farasi, ili apate kuonyesha manufaa yake, Mara akampanda na kumwuliza mtafme wapi anakotaka kumtuma. Mfalme akamwambia, ‘Wauona mlima ule-e?’ Akaonyesha kilele cha mlima mkubwa mno uliopanda juu mawinguni, yapata mwendo wa saa kasorobo kutoka pale Shirazi mpaka kufika huko. ‘Nenda kaniletee tawi la mikindu inayoota chini yake.’
Mfalme alipotamka maneno haya yule Mhindi akaizungusha sukurubu iliyowekwa juu ya shingo ya farasi karibu na tandiko, mara akapaa hewani kama umeme asionekane tena. Muda wa robo saa Mhindi akaonekana anarudi, amechukua tawi la mkindu mkononi mwake, akimteremsha chini farasi wake karibu na kiti cha enzi, akashuka na kuliweka lile tawi mbele ya mfalme.
Sasa mfalme akasadikisha ule mwendo wa ajabu wa yule farasi na akatamani awe naye yeye, na hivyo ndivyo ilivyokuwa, maana yule Mhindi alikuwa tayari kumwuza, na mfalme naye alikuwa akimtazamatazama farasi kama aleyekwisha kumnunua.
Mwisho akamwambia Mhindi, ‘Kwa umbo lake la nje tu, sikumdhania kuwa ni mnyama wa manufaa jinsi hii, nami nimefurahi sana kwa kunionyesha kosa langu, na ikiwa utaniuzia sema bei yako. ‘
Mhindi akajibu, ‘Seyid yangu, sina shaka kuwa mfalme mwenye hekima kama wewe atanifanyia haki kwa farasi wangu baada ya kuona uhodari wake kwa mara ya kwanza, na mimi sikwenda mbali sana kwa kufikiri kuwa labda utampenda awe wako. Basi ni afadhali nimtoe zawadi, na hivyo nitakupa wewe bwana wangu kwa sharti moja. Farasi huyu sikumfanya mimi ila nilipewa na mtu aliyembuni, kwa kubadilishana na binti yangu, tena kwa kuniapisha kiapo kuwa sitotengana naye vivi hivi tu, ila kwa kitu cha thamani sawasawa.’
Mfalme akamwambia, ‘Taja cho chote utakacho. Milki yangu ni kubwa yenye miji mikubwa mikubwa mizuri. Chagua uupendao, uutawale mpaka mwisho wa maisha yako.’
Mhindi hakuona ukarimu huo unatosha kama vile alivyoona mfalme. Akajibu, ‘Seyid yangu, ninakushukuru sana sana kwa kunipa utawala, ila nakusihi usinikasirikie, ikiwa nasema kuwa naweza kukutolea farasi wangu kwa kubadilishana na binti yako.’
Wafuasi wa mfalme waliposikia maneno haya wakaangua vicheko wakacheka, na Feroz Shah mwana wa mfalme, ambaye, ndiye mrithi wake, akakasirika sana kwa ufedhuli kama ule. Lakini mfalme alifikiri kuwa haitamwia thamani kubwa kutokana na binti yake kwa kupata mchezo mzuri kama ule. Basi wakati mfalme alipokuwa akisitasita kujibu, mwanawe akaingilia kati akasema, ‘Seyid yangu, afadhali usifanye haraka kumjibu bazazi huyu fidhuli. Fikiri jinsi damu ya babu zako itakavochanganyika na kuwa duni.’
Mfalme akajibu, ‘Mwanangu, najua wasema ndivyo, lakini naona huitambui thamani ya farasi, na kama nikiyakataa kweli mashauri ya Mhindi, ataondoka aende akamwambie mfalme mwingine maneno haya haya, nami hivyo nitaona kushindwa nikimfikiri mtu ye yote mwingine kuipata hii Ajabu ya Saba ya Dunia.
Kwa hakika sisemi kuwa nitayakubali masharti yake, lakini naye pengine huenda akatoa sharti ingine, basi kwa kitambo hiki tulicho hapa ningependa umwangalie farasi huyu, na kwa ruhusa ya mwenyewe, umjaribu mwendo wake.’
Yule Mhindi aliyekuwa akisikia maneno haya ya mfalme akaona iko dalili ya kupata vile alivyokusudia, akafurahi na kuridhia kwa yale aliyotaka mfalme. Akaja kumsaidia mwana wa mfalme apate kupanda farasi na kumwonyesha namna ya kumwendesha, Lakini kabla hajamaliza kumwonyesha yule kijana akaizungusha Sukurubu, na mara ile ile farasi akapaa hewani akawa haonekani tena.
Watu wote waliokuwapo kuangalia wakakaa kungojea kwa muda, wakitaraji kuwa pengine huenda mara wakamwona kwa mbali akirudi, hata mwisho yule Mhindi mwenyewe akawa na hofu. Ndipo akaenda akajiangusha kifudifudi mbele ya kiti cha enzi, na kumwambia mfalme, ‘Seyid yangu, bila shaka umeona kuwa mwanao hakufanya subira, hakunidirikisha kumwambia yote yaliyokuwa haja kumwambia ili aweze kurudi mahali alipoondokea. Basi nakusihi usiniadhibishe; kwani hilo si kosa langu, wala usinipatilize kwa mashaka yo yote yátakayompata.’
Kwa hofu kuu aliyokuwa nayo mfalme akasema kwa hasira ‘Lakini kwa nini hukumwita arudi wakati ulipomwona anatokomea?’
Mhindi akajibu, ‘Mwendo wake wa kasi ulinitia bumbuazi hata kama ningalimwita hangalisikia. Lakini natutumai kuwa atafahamu kuizungusha sukurubu ya pili, ambayo itamfanya farasi kushuka chini.’
Mfalme akasema, ‘Ehe! Kama akifanya hivyo, kitu gani kitakachomzuia farasi hata asishukie baharini, au kumwangusha majabalini na kuvunjika kenyekenye?’
Mhindi akajibu, ‘Usiwe na hofu, bwana wangu, maana yule farasi ana akili ya kuvuka bahari, na kumpeleka mpandaji wake popote atakapo kwenda.’
Mfalme akamjibu, ‘Vema basi, lakini fahamu kuwa asiporudi tena kwa muda wa miezi mitatu, wala haniletei habari yo yote kuwa ni salama, maisha yako yatapotea.’ Kuisha kusema hivi akaamuru askari wake kumkamata Mhindi wamtie gerezani.
Kwa kitambo hiki chote, yule Feroz Shah mwana wa mfalme alikuwa amepaa hewani kwa furaha, na kwa muda wa saa nzima alizidı kupaa juu hata ile milima mikubwa mikubwa ilionekana sawasawa na tambarare. Kisha halafu akawaza kuwa sasa nai wakati wa kushuka chini, na kufanya hivyo ilimlazimu azungushe sukurubu kuelekeza njia, lakini kwa bumbuazi na hofu aliyokuwa nayo hakuthubutu hata kidogo. Ndipo alipokumbuka kuwa hakufanya subira kuambiwa namna ya kushuka chini tena, mradi akajiona hatari imemsimamia. Kwa bahati akili zake hazikumpotea, ndipo akaanza kuitazama shingo ya farasi kwa makini sana, hata mwisho kwa furaha yake kuu akagundua kigingi kidogo, kidogo sana kuliko kile kingine, karibu na sikio la upande wa kulia. Hata alipokizungusha, mara akajiona anashuka chini pole pole kuliko vile alivyopanda.
Wakati huo ulikuwa giza, na kwa vile ambavyo mwana wa mfalme hakuweza kuona kitu, alimwachilia farasi ajiongoze mwenyewe. Ilikuwa usiku wa manane Feroz Shah mwana wa mfalme alapogusa chini, amechoka, hasa kwa vile alivyokua hajala kitu tangu asubuhi.
Basi aliposhuka juu ya farasi, jambo la kwanza alilofanya ni kupatambua mahali alipo, lakini kwa ajili ya lile giza kuu hakuweza kutambua kitu ila alijiona yuko juu sakafuni kwenye jumba kubwa mno, lenye kuzungushwa viguzo vya vya nawe ya marmar. Katika pembe ya sakafu hiyo kulikuwa na kilango kinachofungulia vidaraja vya ngazi inayoendea chini ndani ya nyumba.