Alhad Salum alia na Mwamposa kuwaombea wanawake wa kiislamu, awataka mashehe waanzishe vilinge vya dua kuwaponya wanawake!

Sasa mnasumbuka Nini? Qur'an 5:52-52,"Enyi mlioamini msiwafanye mayahudi na wakristo kuwa marafiki wenu....." Lakini mnaenda kutafuta miujiza kwa Mwamposa.
Kwanza hiyo Aya ilikuwa inawahasa waislamu kipindi kile ambacho Uislamu ulikuwa unalinganiwa,kwahiyo kulikuwa na upigaji Vita mkubwa juu ya Uislamu na uadui ulikuwa mkubwa mno,,,,kwahiyo waislamu walikuwa wanahaswa wasifanye Urafiki na kuwapa Siri zao kwani hao wenzao mwisho wa siku wanawageuka na kuwafanyia uadui dhidi Yao.

Lkn haimaanishi Uislamu hautaki kufungamana kama jamii na wakristo laa! Ila ilikuwa kipindi kile cha uadui mkubwa,,,,na kuna Aya inasema walio karibu zaidi katika Uislamu na hata kusilimu ni wakristo na sio wayahudi.


Ila linapokuja swala la ibada au kumwabudu Mungu,,,,basi Uislamu Una mipaka yake,Ila hao wanaokuja huko kuombewa hawaijui Imani yao
 
Kama kichwa cha uzi kinavyojieleza.

Itoshe tu kusema haya yote yanathibitisha kazi njema anayofanya Nabii na Mtume Mwamposa.

Yesu ndiye mponyaji!
Kwani tatizo liko wapi? Imani si ni suala binafsi? Mkristo akienda kuombewa na shehe kuna tatizo, si ni maamuzi yake? Yaan tunataka sasa kuingilia maamuzi ya mtu binafsi kwa sababu ya dini? Huo sasa ni ujuha
 
Yesu ni Upendo
Ni kweli Yesu ni Upendo wala hatukatai Hilo,,,,,na Imani ya Muislamu haijakamikilika kama haamini Malaika wa Mwenyezi Mungu,vitabu vyake Kwa maana zaburi,torati na injili,na mitume wake wote,ndio maana Yesu kama waislamu Tunamheshimu na kumtambua kama Nabii wa Mungu,kwahiyo muislamu yoyote akimpinga Yesu basi Imani yake ni batili.
 
Akomeeee, bikra Maria tuombee.
Akikuombea uliona matatizo hawataki wahi law Mwamposya

Wako wenzio kibao wameombs hiyo sala weee hakuna majibu ya matatizo yao walipoenda kwa Mwamposya yakaisha

Usiwe na tai ya dini shingoni wakati una kilichokubana kwenye maisha Tafuta ufumbuzi ukiwemo kwenda kwa Maposya .Ukifa na Tatizo wakati ufumbuzi upo huko ni kujiua !! Maisha sio watu wanakuanaje au dini inakuonaje au viongozi wa dini wanakuonaje ukienda kutafuta ufumbuzi kwa Mwamposya .Uwe jasiri na usiogope mtu hawakukuleta duniani wao mijungu. Shida ni yako unayeumia ni wewe na maumiivu ya shida au Tatizo linayemuumiza ni wewe mwenye nalo.Ni wajibu wako na haki yako kabisa kutafuta ufumbuzi popote ikiwemo kwa Mwamposya
 
Kwani tatizo liko wapi? Imani si ni suala binafsi? Mkristo akienda kuombewa na shehe kuna tatizo, si ni maamuzi yake? Yaan tunataka sasa kuingilia maamuzi ya mtu binafsi kwa sababu ya dini? Huo sasa ni ujuha
Tena ujuha wa hali ya juu

Katiba ya nchi yenyewe imetoa uhuru wa mtu kuabudu popote .Aende msikitini sawa aende kanisani sawa aende huabudu mizimu sawa.Katiba ya nchi imeruhusu Huo.uhuru hautakiwi kuingilia shehe,imamu ,padri au mchungaji nk.Ana uhuru wa kuabudu popote
 
Kwa ufupi Uislam bila Ukristo haujakamilika.

Yani ili imani ya uislam iweze kusimama inabidi ijitengemezee misingi kwenye misingi ya Imani ya Kikristo.

Ndio maana Uislam siku zote unakomaa kujiprove kupitia Biblia (refer ishu ya Isa kuwa Yesu etc..)
 
Shida haina baunsa. Ukiwa na shida sanasana changamoto za ugonjwa mkubwa huchagui unatibiwa wapi. Iwe kwenye tunguri sawa, iwe msikitini sawa iwe kanisani sawa. Wapo wanaofanya kwa siri ni wanafiki wengi sana lakini wapo wanaokuwa wazi na Mungu anawasamehe
 
Si waislamu ila wanamajina ya kiislam
 
Hapana haupo sahihi,,,,Dini ni moja Tu ambayo inamwamini Mungu Mmoja,,,,ndio maana vitabu vyote vya Mungu kuanzia zaburi,torati ,injili na Qur'an vyote vinamtangaza Mungu mmoja,kwahiyo Uislamu ni Dini kongwe Sana.

Tumezungumza ktk baadhi ya nyuzi kuwa Uislamu ni kujinyenyekeza Kwa Mungu Mmoja Tu,huo ndio Uislamu,,,,kwahiyo mitume wote na Manabii walikuwa na Imani mmoja,,,ndio maana tunamtambua Yesu na kumkubali,,,,,,kuhusu Yesu kujulikana kama Issa ndani ya Qur'an ni Jina Tu lililotumika huko kama Abraham/Ibrahim,,,,,Moses/Musa,,,,Gabriel/jibril
 
Ngoja nami nifungue kanisa langu kama kuna mtu anataka awe kitengo cha SADAKA BASI aseme mapema
 
Sio hata habari kubwa kwani hata wakristo huenda kwa waislamu kutafuta uzima wa afya zao,yamkini ni ktk kutafuta uzima binafsi sioni km ni tatizo..
 
Uislam sio dini kongwe,hauna hata miaka 1500 toka uanze. Uislam umeanza miaka 600 baada ya Ukristo..

Najua utabisha halafu utakuja na zile hadithi za sijui Adam alikuwa mwislam na blah blah zingine mnazokaririshana msikitini.

Uislam SIO Dini kongwe, ni dini ikiyokuja karne ya 6/7 juzi hapo. That's a FACT ambayo ukitumia kichwa chako (bila kushikwa akili) utakubaliana nami.
 
Imani yenu bila kujibanza kwenye Biblia haikamiliki..

Mbona sijawahi kuwasikia Wakristo wakijaribu kujiprove kwa kutumia Quran?
Kwa nini ni nyie mnaojaribu kujiprove kwa kutumia Bible?

We Huoni kuna tatizo hapo?
 
Imani yenu bila kujibanza kwenye Biblia haikamiliki..

Mbona sijawahi kuwasikia Wakristo wakijaribu kujiprove kwa kutumia Quran?
Kwa nini ni nyie mnaojaribu kujiprove kwa kutumia Bible?

We Huoni kuna tatizo hapo?
Sisi tunawapenda hatutaki muende Motoni,,,,,yeyote atakaye mshirikisha Mwenyezi Mungu mwisho mwisho wake ni kuchomwa Moto.

Mwenyezi Mungu anamsifia Ibrahim Baba wa Imani.

"Hakika Ibrahim alikuwa mfano mwema, mnyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu, mwongofu, wala hakuwa miongoni mwa washirikina."

Surah An nahal -120
 
Kwahiyo una fundishwa selfish,duuh kweli hiyo ni hatari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…