Ali Kiba ahujumiwa tuzo za Afrimma. siri yafichuka

Aje imetoboa wapi? acha kujidanganya aje ni nyimbo maarafu tanzania na kenya , hapo Uganda kwenye haina umaarufu
Juzi alikiba anasema mkubwa kuliko Wizkid wanaijeria wanauliza alikiba ndo nani
Ngoja akaperform aje kule mtv mama uone kama umepenya

Ok basi ngoja niseme unachopenda kusikia, Salome na collabo la pepa wemba ndiyo zimetoboa Africa hahaha
 
Pole Ali Kiba kwa kuhujumiwa! Inabidi ukaoge maji ya baharini manake naona mdudu wa kuhujumiwa anazidi kukufuata! Mara unazimiwa mic; mara kwa mwaka wa pili mfululizo unadhulumiwa tuzo zako! Mara Sallam akupokonye collabo yako na Ne-Yo!! Yaani watu wana roho mbaya... bora ukashiriki zako Grammy Awards tu kama mambo yenyewe ndo haya!!!
 
Amekuelewa
 
Mleta uzi ungefanua vizuri kuhusu vigezo vinavyozingatiwa...pengine kura ni moja ya vigezo ila vipo vingine zaidi.
Japo sio mfuatiliaji sana ila kuna kitu inautwa MAJAJI..Pia wana nafasi kubwa
 
MONDI AKA DOMO ANAJULIKANA KWA FITINA HILO LIPO WAZI
 
Mleta uzi ungefanua vizuri kuhusu vigezo vinavyozingatiwa...pengine kura ni moja ya vigezo ila vipo vingine zaidi.
Japo sio mfuatiliaji sana ila kuna kitu inautwa MAJAJI..Pia wana nafasi kubwa
Ukipata jibu la hili swali with reference, tafadhali naomba uni-tag ili nije kuongeza ilmu!
 
Hebu tusaidie hiyo link inayoonesha idadi ya kura kwa kila mshiriki. Other wise ni maneno ya mkosaji tu.
 
Hebu tusaidie hiyo link inayoonesha idadi ya kura kwa kila mshiriki. Other wise ni maneno ya mkosaji tu.
Nimemuomba Tmuller ani-tag akipata jibu la swali lake! Tafadhali Mkuu; na wewe ukipewa hiyo link naomba uni-tag ili nami nipate darsa!
 
Wenzenu WCB na Navy Kenzo wana group zaidi ya 20 za kupiga kura, na kila member wa group anapiga kura 20 kwa siku. Nyie team Kiba mnaishia lawama na kuona mnaonewa. Mziki wa sasa siyo wa mazoea tena. MZIKI UNATAKA YAFUATAYO.
1. Promotion.
2. Good management.
3. Creativity.
4. Team work.
5.Interaction and
6. Cooperation.
Sasa Kiba hayo yote hayupo anategemea miujiza. Abadilike na aache lawama, akubali kuwa chini ya watu ili afanikiwe. Wenzenu wataimba hadi ngonjera na kung'aa Nyie mtaendelea kutunga na kuimba vizuri mtaishia Kenya.
 
nyie mnaojiita team kiba mtampoteza kabisa huyo star wenu, acheni kumtia moyo kiba kwa kusingizia vigezo visivyo eleweka kama kashindwa kubalini na mumwambie akaze buti na ajiulize kwanini yeye tu kila siku anaonewa sio mnatengeneza hoja zisizo na macho wala miguu kumtetea
 
Eti kiba hajapata nomination hata moja mtvmama, hivi wewe umelewa viroba au? Best collaboration n song of the year

Usipaniki Mkuu na wala hakuna haja ya matusi..
Nazidi kukusisitizia kuwa Kiba hajawa nominated MTV MAMA, hizo nomination ulizozitaja wanaostahili pongezi ni Sauti Sol sio Kiba coz yeye ameshirikishwa tu! Nitashangaa kama Kiba akifurahi na kuruka ruka kwa nomination za Sauti Sol..
 

Meza mate Mkuu, relax, breathe in..

Now let's talk; sio sahihi kuwalingishia WCB kuwa Kiba ametajwa kuwania tuzo ya MTV EMA coz wenzenu diamond mwaka jana tu sio tu kwamba alikuwa nominated pekee bali pia alishinda tuzo hiyo na kuirudisha Tanzania..

Mkuu narudia tena kukushauri, Menejimenti ya Kiba inatakiwa iwe ni mikakati na mipango madhubuti!! Kiba akiendeleza chuki na Majungu siku si nyingi atapotea kabisa..
 
Wewe ndo unaiona kubwa leo?
Diaomond hiyo mtv ema kachukua 2 ,mtv ema europe na world wide ipo madale pale
 
Kiba hana nomination mtv mama tuzo inatoka moja kama wakishinda inaenda sauti sol, mtv wanajua nyimbo ya sauti sol
 
Bado kuna safari ndefu sana
Alikiba na Diamond wote ni watanzania na wote wanajua Mziki, Wapeni sapoti Vijana wenu.
Kwa kauli hizi ambazo nimeziona humu, hakika bado tuna safari ndefu sana ya kufika kule tuendako.
Mimi nilidhani kama umekwenda shule ukiingia ktk Biashara unaangalia namna ya kuaply SWOT Analysisi,
sasa mara figisu,
Mara uchawi,
Mara Maiki,
Penye riziki hakukosi fitina, hii ni biashara kama biashara nyingine. Kwa hiyo fitina ziwepo au zisiwepo ni changamoto za kawaida, Cha msingi ni kujipanga.
Kama hujifunzi kutokana na makosa usitarajie ipo siku utapiga hatua.
Siku zote watu wanapokufananisha na mwingine JUA bado hujafanya tofauti, Fanya vitu adimu(huwezi kupata kitu ambacho wengine hawana bila kufanya ambacho wao hawajawahi kufanya). Piga hatua kali zaidi!
Ni ngumu sana kukubalika na watu, inabidi upige hatua mpaka wakushangae.
Haya Mambo ya figisu ooh mara anabebwa yalikuwaga primary, wengi wetu tuliyapitia. Lakini unajua kile ambacho tulikuwaga tunafanya,
Unapiga mpaka hakuna wa kukuangalia tena, yani unatengeneza gap mpaka wanaogopa kukuangalia.

Kwa hiyo whether team kiba au team mond, Muhimu ni kushauri Vijana wetu wafanye kazi ambazo hazikuwahi kufanyika ili akitoa ngoma moja inatoboa vizazi na vizazi, mimi nitafurahi sana kama siku moja mtanzania atatengeneza nyimbo kali kwa lugha yeyote ile ili ifikishe VIEWS at least BILLION MOJA. That might be history in Africa as at 21st century Tunakuweka ktk kumbukumbu muhimu duniani.

So tusiwavunje moyo, acheni kuwafananisha kwa sababu kila mmoja is best at his own.
 
Kiba hana nomination mtv mama tuzo inatoka moja kama wakishinda inaenda sauti sol, mtv wanajua nyimbo ya sauti sol

Hahahahaha hapa ndio unafiki wenu unapojulikana, ikitokea huo wimbo upate tuzo mtasema wimbo ni wa sautsol kiba hausiki ila ikitokea huo wimbo ukose tuzo mtasema kiba kakosa tuzo. Hahahahahahahaha wanafiki ninyi, tulia tuwanyooshe coz mlizoea vya kunyonga kwenye vi afrimma vyenu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…