Sambusa kavu
JF-Expert Member
- May 4, 2015
- 806
- 1,296
Leo ndio nimeamini jamaa hayuko sawa kichwani yani kuzimika mic unatoa lawama kwa Salam wakati ulitakiwa kuwalaumu waandaaji wa show,,Huyu jamaa anafeli sana kwa wivu usio na msingi. It's obvious kuna foul play, ila Diamond na team yake hawana juice ya kufanikisha kitu kama, nor do they have a reason to anyway.
Kilichotokea, ni technical foul-play kutoka kwa waandaaji. Ni wazi hawakujipanga, na Kiba akatolewa kafara.
Cha kufanya, ni Kiba kuwabana waandaaji kupitia makubaliano yao(kama yapo), na jamaa watoe report ya kilichotokea na kumsafisha mshkaji, pengine wamlipe fidia. Otherwise, hili ni doa kubwa kwa msanii wa level yake, na anazidi kuchafua kwa kutoficha upumbavu wake.
Kama uwepo wake ulikuwa sio ruhusa basi wala asingalikuwepo pale... kwa hiyo bado naziona sababu za kiba ni za kijinga na kitoto, hivi salam ndio alikuwa mhandisi wa sauti wa hiyo show?Tatizo ni ssalaam alifata nini backstage.... alienda kama nani.. na kufata nini. Na ili iweje.. aliiitwa? Alikiba keep cool ur talented than one they compare to...
Leo ndio nimeamini jamaa hayuko sawa kichwani yani kuzimika mic unatoa lawama kwa Salam wakati ulitakiwa kuwalaumu waandaaji wa show,,
Rayvanny bwana...Raymond ni hatari sanaaa!!!huyu mtoto hafai hata kwa kulumangia[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kiba asipochunga ,kuna wanamziki waa hattari wanakuja,
kwa hali ninayo iona ni wazi Alikiba anapaswa kutafutiwa daktari wa saikolojia kwakweli hayuko sawa...Jamaa niliwahi kuona interviews zake mbili tu kwa Millard, nikajua tu hayuko okay. Adui yake ni yeye mwenyewe.
Wakuu mnakumbuka tukio la Kiba kuzimikiwa na mic kwenye tamasha la Mombasarocks?
Akihojiwa na kipindi cha Mseto Citizen na mzaz Willy Tuva, Kiba alidai kuzimika kwa mic yaweza kuwa ni figisu za Sallam SK yule meneja wa Diamond coz kipindi anapafomu SK alikuwa nyuma ya stage.
Umemaliza yote mkuuKuna mambo mengine kama haya ndio huwa tunasema uswahili. Alikiba anashangaa meneja wa Diamond kukaa backstage, na eti anahoji kwa nini asingekaa VIP kama ishu ni kuona shoo. Hivyo kwa mtazamo wake yeye Alikiba anahisi meneja wa Diamond ndiye aliyezima Mic. Katika hali ya kawaida tu hivi inawezekana meneja wa Diamond akazima Mic kwenye hughuli isiyo yake? Anyway tuachane na uswahili wa Alikiba na pengine ndio maana anashindwa kufanya mambo makubwa katika muziki pamoja na ukongwe alionao katika muziki.
Kazi ya kuwa meneja wa mwanamziki ni kubwa sana kama unamua kujishughulisha na kuhakikisha mwanamziki wako unayemsimamia anafika mbali. Sote tunaelewa ni jinsi gani WCB walivyo wanzuri wa kutumia kila aina ya upenyo wanaopata katika kuhakikisha kazi zao zinafika mbali. Chris Brown kaja Kenya pamoja na uongozi wake, hivi mlitegemea Sallam akae tu ametulia, au akae VIP ametulia anangalia shoo badala ya kutengeneza contacts na uongozi wa Chris Brown? Hivi Alikiba anajua kweli namna connections na wasanii wa nje zinavyopatikana? Anajiuliza why Sallam akae backstage, heee sasa alifikiri Sallam ataongea na uongozi wa Chris Brown wapi? Mwenzake anahangaika kufanya connections na wasanii wakubwa yeye anakaa kufikiria kwamba mtu anaweza kusafiri kutoka Dar hadi Mombasa kwa ajili ya kwenda kuchomoa Mic. Huu ufinyu wa mawazo ndio unamfanya kila siku aishie kulalamika na kuhisi anahujumiwa. Leo tunapopewa ratiba ya tour ya Diamond na Neyo UK si kazi ambayo imefanyika kitoto, bali watu wametumia fursa na nafasi zinazojitokeza kuweza kutengeneza connections kama hizo. Au tumeshasahau ni namna gani Neyo na Diamond walikutana? Au hatujajua ni namna gani Diamond na Swiss Beats wamekutana?
Kifupi Alikiba ana safari ndefu ya kujifunza kuhusu namna ya kutafuta soko la muziki. Akiendelea kuwa na fikra mgando kama hizo ataishia kulalamika tu na mwishowe atashindwa kufanya vinzuri kwa sababu ya kutaka kushindana na Diamond. Mwenzake Diamond sasa hivi anafocus kwenye soko ya Ulaya maana Afrika ameshamaliza, America ameshaingia, ila yeye Alikiba anawaza kwamba mtu atapoteza hela zake kwenda Mombasa kuchomoa Mic. Daaah kweli tunatofautiana .
Hahaha Aseehivi kiba na Simba na Yanga wana undugu?
maaan miaka nenda rudi wanategemea mapato ya milangoni
Alifuata nini back stage,ukijua mtu atatafuta sababu kupitia wewe muepuke...ni sawa na wazazi wanapowaambia watoto usicheze na mtoto yule mtakolofishana tu..kwa hiyo ni jukumu lako kumpitia mbalisababu amesema ni 'muda" wa Chris sasa salam ndo alipanga ratiba?
alitakiwa akae wapi??Alifuata nini back stage,ukijua mtu atatafuta sababu kupitia wewe muepuke...ni sawa na wazazi wanapowaambia watoto usicheze na mtoto yule mtakolofishana tu..kwa hiyo ni jukumu lako kumpitia mbali
..
Ally Kiba ana matatizo na management yake ina matatizo zaidiAlifuata nini back stage,ukijua mtu atatafuta sababu kupitia wewe muepuke...ni sawa na wazazi wanapowaambia watoto usicheze na mtoto yule mtakolofishana tu..kwa hiyo ni jukumu lako kumpitia mbali
..