Ali Kiba dharau zitakuponza, heshimu kitu cha bure

Ali Kiba dharau zitakuponza, heshimu kitu cha bure

Mkuu umesahau kipindi cha show ya tigo music pale leaders ambapo jamaa alikataa kuwasalimia wasanii wenzake akiwemo mwana FA ambae walikuwa wamefanya nae kolabo ya kiboko yangu, alafu akamaliza akaruka ukuta akasepa
Duuu kama ni kweli alifanya hivyo basi msimlaumu bila shaka yatakuwa ni masharti ya waganga.
 
Tatizo mnajigonga sana kwake. Mwacheni kama alivyo
 
Ameshapotea kwenye game huyu!
Dharau zilimponza, zikamponza na bado zimeendelea kumponza!
Mond ni mjanja ndio maana nasema hata akianguka ni rahisi kusimama.
Kiba kwa dharau zake na kujiona amefika pamoja na kujitenga kwake kumemfanya azidi kudidimia siku hadi siku.
Kwanza amenikera sana kukaa karibu mwaka mzima alafu akaja na pambio la ajabuajabu!
 
Kuwa shabiki wa Alikiba inabidi ujitoe ufaham kweli kweli huyo jamaa ana roho ya majivuno na kujiskia kweli kweli alafu anajiita king, sijui king wa nini wakati boya tu

Wenzake washavuka boda huko na makolabo na akina Rick ross, neyo, omarion ye yupo yupo tu na nyimbo zake za kishamba alafu anajiita king, ukiingia ukurasa wake wa instagram hajamfollow hata mtu mmoja, hapo ndio utamjua huyu jamaa ni kiazi, hata kuwafollowa wasanii wenzake hajawafollow, inamaana hana cha kujifunza kwa wenzake
 
Acheni uchawi wenu na timu yenu ya kishetani mnatumia nguvu kumshusha kiba ila hamuwez, kila MTU ana mapungufu yake maana kiba naye kaumbwa kama binadamu yeyote .. Labda tukuulize wewe mtoa mada wewe umekamilika?? Tena inawezekana ikawa afadhali ya kiba kuliko ww ni vile tu hujulikan..Mkamilifu ni Mungu pekee
Umeelewa lakini kinachozungumziwa? Kama mkamilifu ni Mungu pekee kitu ambacho ni kweli je mtu akionyeshwa mapungufu yake ili ajirekebishe ni kosa? Kwako wewe hayo aliyoyafanya Kiba ni sahihi na kuambiwa ukweli ni kutaka kumshusha au kumpandisha?
Kiba anahitaji mashabiki kuliko mashabiki wanavyomhitaji, ukileta dharau watu watamuona hata Mkaanga Sumu ni bora zaid yako na utabaki na jina lako.
 
M
MODS PLEASE DON'T MOVE OR MERGE THIS THREAD

INAGHARIMU SHILINGI 0.00 KUWAHESHIMU WATU WENZAKO

Kujiheshimu na kuheshimu wengine ni mmoja ya nguzo kuu katika mafanikio, Hii imedhihirishwa tena baada ya msanii Ali kiba kuwa katika skendo mbali mbali za kudharau watu wengine na kujiona yeye ndio mwamba kitu ambacho kimehaaribu sana muziki wake.

Ikumbukwe ya kwamba Ali Kiba hayupo socially interractive lakini hili pekee sio la kumfanya asiweze kuheshimu wenzake, Naposema huyu hayupo socially interractive ni kwamba sio mtu wa kujichanganya changanya na watu na ndio maana kuna kipindi menejimenti yake ilimwambia ajaribu kupata mashabiki zaidi kupitia kuwa socially interractive, Hatua ya kwanza hii walianza kumfanya Ali Kiba apande dala dala ajimix na watu lakini ilikuwa ni dhahiri kaisa huyu kaka mkubwa alikuwa anavumilia tu kuwemo kwenye dala dala,,,Tizama hapa

Kuna kipindi msanii mwenzake Harmorapa alienda kumpokea airport na alikuwa ame mwandali alikiba t-shirt kaisa lakini unajua kilitokea nini, Unaambiwa ali kiba aliikataa akafunga kioo cha gari ila baada ya muda kidogo inadhaniwa kwamba management yake ilimlazimisha tu aichukue hio t-shirt

Wiki kadhaa zilizopit tulishuhudia live bila chenga msibani, Msanii Diamond alipofika mibanid na kuanza kusalimiana na wenzake kwa heshima ya kupeana mkono kwa mkono hali ilikuwa tofauti kwa Ali kiba ambae alitoa kiganja pale alipopewa mkono wa salamu, Hili tukio lilikuwa ni wazi kabisa kaka braza ana dharau mno

Ali Kiba ni Mswahili na amekulia Uswahilini ila cha ajabu hawezi kuishi Kiswahili.
Kubwa zaidi wanaomzunguka hawampi Ushauri wa kumjenga ama hakubali kushauriwa.
Hivi anapungua nini akijishusha kwa Jamii inayomzunguka ambao ndo Mashabiki zake? Au kuitwa King ndo anaona amemaliza kila kitu?
Bado anahitaji kujifunza zaidi lasivyo atazidi kupoteza Mashabiki zake!
mkuu mibanid na kaisa ndio mini rekebisha maneno yako right now
 
Mie huwa napata shida sana mtu unapoacha kazi zako na kuanza kufuatilia maisha na mapungufu ya wenzio. Watu hatuwezi kufanana ila nadhani ni vyema tujikite kuyajua mapungufu yetu na kuyafanyia kazi na kuachana na watu wengine.
Well Said Bro....
Mtu mishipa ya vidole inamsimama kumsema mwenzie ambae hata hajui kama ana exist...

Mtu sio shabiki wake sasa kinakuuma nini?? pamoja na hayo mapungufu mbona ana wafuasi?

Ngozi nyeusi ina tabu sana.
 
Tabia huwa haina dawa,mnaweza kumlazimisha hiyo tabia mnayoitaka ya kujichanganya ndio akaharibikiwa,bora abakie hivyohivyo..
 
Komaa na mishe zako kwani na ww ukimpotezea kuna tatizo?
 
Back
Top Bottom