Wakati Gambo anaongea kuhusu uporaji wa fedha za kigeni Arusha ghafla nikajiskia kuomba kumpa taarifa muongeaji
Nilijiskia kutamka maneno haya:
"Muheshimiwa naibu Spika naomba kumpa taarifa mchangiaji kuwa wakati uporaji huo unafanyika yeye ndiye aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Zoezi lile alilisimamia yeye mwenyewe Kama mwenyekiti wa vyombo vya ulinzi na usalama wa mkoa
Mh. Spika, naomba kumpa taarifa mchangiaji kuwa viongozi wanaosimamia uvunjifu wa sheria za nchi ni wahaini na kwa kitendo kile alihujumu uchumi wa nchi yetu hivyo anastahili kuwa gerezani kwa sasa na sio kwenye Bunge lako tukufu"
Wakati nawaza hivyo ghafla usingizi ukaishi nikijikuta kumbe Mimi ni Uncle Jei Jei tu hata mtaa ambapo jengo la bunge lipo sijui unaitwaje. Nikajisonya tu Kama Makonda alivyowasonya Waziri Mkuu na wastaafu enzi zile akiwa Paul Makonda kweli kweli sio leo anavyotambulika kama Baba Keagan