Alichofanya Mkuu wa Mkoa wa Dar, Makonda kwa Pierre Mzee wa Liquid ni udhalilishaji na kinyume cha haki za binadamu

Makonda kwa kupenda kutembelea chaki hajambo

Kila eneo katika jamii lina watu wake maarufu..asitake kuleta ujuaji mwingi..wasanii wa muziki na sanaa wengi wao pia si watu wa ovyo pia,mbona jamaa hajawasema??


Aache wivu..Pierre atabaki kuwa juu
 
Haikuwa njia sahihi kuzungumza hivyo kama RC !
Linapokuja suala la maadili mbona kuna wengine kutwa walikuwa wana post pic wakiwa watupu

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kosa la Pieri Likwidi konk ni kuwa timu kibakuli, wakati Bashite ni mlezi wa wachafu.

Pili likwidi konk alimtukana mwandishi wa habari sijajua ni wawasafi maana mbele yake ilikuwepo maiki ya WCB.

Bifu la Wasafi na Likwidi lilianzia kwenye wimbo wa tetema, Reyvan aliingiza maneno na vionjo vya Likwidi bila ridhaa yake.

Likwid akasema wangemwomba ama kumshirikisha yeye mwenyewe ama wampe hata kifuta jasho Wasafi wakakaza.

Ukitaka kujua Bashite anaroho mbaya, huyo Pieri kwenye uhamasishaji Taifa stars alitumika, ila kwenye mechi akazuiwa na Pieri likwidi alitaka aingie kwa masupastar akazuiwa.

Kwenye hafla ya ikulu jina lake lilikatwa, japo Mama Samia kwa heshima na taadhima akamtaja kwa kutambua mchango wa Pieri Likwid konk....hicho kitendo kilimuuma sana Bashite.

Sasa leo mkuu wa wilaya akamwalika kwenye shughuli ya tokomeza ziro, hiki kitendo kimemuuma sana Rais wa Dar kuona jamaa anazidi kuwa juu/kileleni.

Kuna hatari hata makampuni yaliyoanza kufanya kazi na Pier yakasitisha mikataba iwe kwa hiari ama kwa lazima maana Rais wa Dar hapendizwi na wanachokifanya.

Hata hivyo ukiangalia kiundani alietukanwa hapo na Makonda ni Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate aliemwalika Pieri Likwid Konk.

Pole Likwid Pierr Konk utabaki kuwa juu kileleni.
 
From day one nilivyo skia huyu mlevi nae ni mtu maarufu nikajua kabisa Tanzania inahitaji kujitathimini upya, kuna kila sababu za msingi Paul Makonda akabidhiwe nchi baada ya Magufuli, maana naona Tanzania kuna wapumbafu wengi sana kiasi kwamba kwa level za Uzee wa Magufuli hawezi kukabidhia nazo.....
 
Makonda is right

Pierre is another bad example
 
Nimeiona clip kwa kweli Makonda kachemka sana. Wivu unamsumbua. Kachemka sana ktk hili. Alafu bmaskini jamaa kakaa pembeni anacheki tu jamaa akimponda. Nimejisikia vibaya sana kaonewa sababu ya wivu wa jitu.
makonda anatakiwa ajue watanzania wana haki ya kupumzika na kufurahi baada ya kazi. Pierre ni nembo yetu ya kupumzika na kufurahi baada ya kazi. Kuna wemgine tusio walevi tukimuona tu hata kama tuko nyumbani basi tunaburudika kwa uwakilishaji wake.
 
Mmh hapana ndugu jamii ina watu wa kila aina.. Hebu angalia kama kina Mr bin au John Walker... J. Walker mpaka leo ni brand maarufu duniani ya kilevi....
Imagine kama taifa watu kama hawa ndio tegemeo kwanini Pierre konk asipate shavu...? View attachment 1058620

Jr[emoji769]
 
Nchi gani hiyo aiseee...... Jambo gani alilofanya kubwa

Sent from my TECNO K7 using Tapatalk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…