Alichofanya Mkuu wa Mkoa wa Dar, Makonda kwa Pierre Mzee wa Liquid ni udhalilishaji na kinyume cha haki za binadamu

Alichofanya Mkuu wa Mkoa wa Dar, Makonda kwa Pierre Mzee wa Liquid ni udhalilishaji na kinyume cha haki za binadamu

Kwahiyo tuendelee kujenga taifa linalojenga watu kama akina Lemutuz, steve nyerere na akina Pierre? Kwamza si bora hata huyo steve nyerere anajulikana ni msanii katika yaifa hili na pengine katika kazi zake alisha na analipa kodi

Huyo Piere ni msanii wa nini? Analiingizia kipi taifa zaidi ya kuwa spoiler

Dumelang
Ukiuliza Pierre ni msanii wa nini, mimi nitakuuliza Steve Nyerere ni msanii wa nini?

Tunachoshangaa ni unafki wa mkuu wa mkoa kumpinga Pierre wakati watu wake wa karibu hawana maadili na wengine ni wapuuzi kumshinda Pierre.

Ni kama baba ambae mwanae ni mwizi, ila hasemi. Anawasema watoto wa familia nyingine.

Kama kweli anayo nia ya dhati ya kulinda maadili, aanze na wanaomzunguka.

NB: vipi kizazi cha kufoji vyeti, chenyewe kinatufaa?

- KANA -
 
Unamfahamu Yule Mkenya aliyepata umaarufu kwa kubeba chakula aina ya Makande kwenye foleni ya kupiga kura ?
Yafungeni basi na Magazeti ya Udaku.
Nyie Watukufu acheni kumwangalia Piere.
Sisi tunapenda kumwangalia na anatufurahisha.
Na umaarufu tumempa sisi tunaye mpenda na sio yeye kwamba ameutafuta kwa kutushawishi.
Sisi ndio tuliomshawishi na tukamrekodi kama tunavyorekodi Komedi nyingine.
Mnatuharibia biashara zetu.
Mnataka tukaibe ?


Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi unaringanisha tukio la mtu kubeba makande kwenye foren ya kupiga kura na anacho trend huyo Pierre, mbaona kubeba makande kwenye foreni ya kupiga kura ni news hata mainstream media can take it na ika trend.

Lets take a brake. We need something more serious to take this country to a next stage.



Dumelang
 
Ni baada ya siku chache Makamu wa Rais Mama samia Suluhu kumpongeza msanii maarufu Liquid Pierre kwa kufanikisha ushindi wa Taifa Stars.



Majibu ya Pierre.

View attachment 1058778

Kampeni ya tokomeza zero na aliyoongea bwana msambwada yamedhihirisha zero kwel kwel na wakati anaobgea huo utymbo wazero wengi walicheka kiukwel kati ya alikashfu na aliyekashfiwa mwenye zero hapo ni aliyekashfu hahahaaaa Mr ZERO AMEONYESHA ZERO YAKE TENAAAAA
 
From day one nilivyo skia huyu mlevi nae ni mtu maarufu nikajua kabisa Tanzania inahitaji kujitathimini upya, kuna kila sababu za msingi Paul Makonda akabidhiwe nchi baada ya Magufuli, maana naona Tanzania kuna wapumbafu wengi sana kiasi kwamba kwa level za Uzee wa Magufuli hawezi kukabidhia nazo.....
Hapo utajipima mwenyewe katika kundi la Watanzania wapumbavu we uko namba ngapi? halafu pia pima kati ya Pierre na Makonda nani ni wa hovyo hovyo?
download.jpg
images (3).jpg
images (4).jpg
IMG-20190331-WA0013.jpg
 
Moja ya Jambo baya kwenye maisha Ni kujiona wewe ni Bora kuliko wote, haya Mambo ya kuhukumu kwa nje yametufanya tuwadharau wanaoishi na familia zetu( house boys and girls), yametufanya tuwadharau wasiosoma, yametufanya tuwadharau mafundi mchundo na vyuo vetu vya ufundi, yametufanya tuwadharau wakulima, yametufanya tuishi kwa kuabudiwa.

Kila kiumbe kimeletwa Duniani kwa sababu, naamini waliomlea Makonda wangemwona hafai toka utotoni Leo asingekuwa hapo alipo. Wapo watu wametufanya tuwe na adhi tulizonazo na tukijifanya kusau tulipotoka ndipo tunajikuta tunatoa kauli kama hizi za mkuu wa mkoa kwamba watu ovyo ndio wanaonekana maarufu.....unamwita binadamu mwenzio wa ovyo kwa sababu TU wapo wanaokutukuza....it pains kwa mkuu wa mkoa kutuona Watanzania ni watu wa ovyo.

Yamkini piere before hakuonekana wa muhimu kwenye familia yake lakini leo wapo anaowasomesha na kuwapa huduma mbalimbali.....uongoz ni busara na siyo ubaguzi, mkuu wa mkoa anaongoza masikini, matajiri na wenye uwezo.......Mkuu wa mkoa hapo umemkosea huyo kiumbe mwombe radhi na umwite umpe ajira au umfanyie cancelling kumtoa huko usikokupenda umweke kwenye level unayodhani inamfaa

Lakini pia acha wivu, umaarufu wa mtu unatengenezwa. Wewe kalewe utuambie konki uone Kama utakuwa maarufu....wakuondoe hapo kwenye ukuu wa mkoa urudi kujitegemea kama Kama Kuna atakayekuita viti vya mbele

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yangu hayo mambo yanahtaji tafakur ya kina co kwa hyo unaemwambia ambaye uwepo wake tu hapo alipo kwa mbeleko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wafikiri nani katufikisha hapa, kupimana matezi dume, kuwadhalilisha watu kwa madawa ya kulevya, kuwadhalilisha wanawake na watoto pale ofisini, kuwadhalilisha waalimu wapande bure kwenye daladala, kuwataka kuwapima watu ukimwi majumbani mwao. Tumekua Taifa la kipumbavu sababu ya same person. Alaf unadai Kenya nini wakat juzi hapa aliitwa hukohuko.
Mabadiliko yanaanza na wewe. Sio na makonda. Nadhani jana kafanya kitu tu bora kati ya vitu bora bila kujali aliwasilisha vipi lakin deep down ya hii issue tunahtaji kuwa serious kidogo kuwa nakizazi kinachojitambua

Tatizo teknolojia inatupeleka kasi sana kuzidi mahitaji yetu ya wakati husika

Dumelang
 
Huwa simuungi mkono Makonda lakini jana kaongea point. Nchi imekuwa ya wajinga hii, mambo yakipumbavu ndio tunayapa kipaumbele.

Kwanza huyo Pierre ni msanii wa kitu gani? Yan Taifa linaacha kujielekeza katika hoja zinazojenga na kuendeleza vizazi vijavyo, elimu, afya na ustawi wa jamii, tunakaa kusifia pombe na kukuza majina ya walevi.

Hapa jirani Kenya tu hawana trend za kipumbavu hivi. Juzi niliona Msanii wa Kenya anashangaa wa Tz wanavyo comment kwenye post za watu maarufu "wanauza uchi na wanawake kwenye magroup" ndiko taifa la wapumbavu likikofika na wafuasi wa vitu hivi wengi na vitoto vya sekondari na chuo wanaolia kila siku hawana ajira.

Kesho kabinti kamemaliza form 4 kanafungua akaunti ya kukaa uchi akiuza **** kwasababu tu ukifanya hivo Nchi hii ndio una trend

Naunga mkono kabisa kemeo la Makonda

Dumelang
So, Kenya ndio mfano wetu wa kuigwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukisoma maneno ya konk utajua kuna kitu ndani yake upeo wake wa akili ni mkubwa kushinda vile tunavyodhani maneno aliyo yatoa ni makubwa sana na mazito sana kiubinadamu na kiimani.binadamu tunasahau tulipotoka na kusahau waliotuweka hapa tulipo.makonda kajibiwa kisomi zaid na mzee was fireeeeee hapo ndipo tunajua fikra njema huwa zipo na busara zipo pia.tusimhukumu mtu kwa udhaifu wake huwa sipend unafki Leo konki wanamuona hafai je wanayofanya WCB na kina wema ndio yanapaswa kuchekewa?
Amemuongezea konk umaarufu zaid huyo mr ZERO aka BASHITE
 
Ukiuliza Pierre ni msanii wa nini, mimi nitakuuliza Steve Nyerere ni msanii wa nini?

Tunachoshangaa ni unafki wa mkuu wa mkoa kumpinga Pierre wakati watu wake wa karibu hawana maadili na wengine ni wapuuzi kumshinda Pierre.

Ni kama baba ambae mwanae ni mwizi, ila hasemi. Anawasema watoto wa familia nyingine.

Kama kweli anayo nia ya dhati ya kulinda maadili, aanze na wanaomzunguka.

NB: vipi kizazi cha kufoji vyeti, chenyewe kinatufaa?

- KANA -
Tulia kidogo kwanza. Steve bila kujali ukaribu wake na Makonda nadhani ana muda sana kwenye game na alianza kuigiza sauti za viongozi enzi hizo ikiwepo ya hayati Mwl J. K NYERERE

amea appear kwenye Bongo Movie kadhaa kama muigizaji. So kwa vyovyote anacho kinachompa nafasi kama msanii

Dumelang
 
View attachment 1058576"watu kama wakina Pierre sijui,watu wa hovyo hovyo ndio wanakua maarufu watu wa maana hawajulikani,tunajenga jamii ya watu gani?"

Haya ndio maneno ya Makonda wakati anahutubia kwenye tamasha la tokomeza zero Kisarawe,lililofanyika jana Mlimani City,ambalo pia Pierre alikuwa moja kati ya watu waliohudhuria.

Hivi mtu kama Pierre kuwa maarufu yeye inamuuma nini? anaposema ni mtu wa hovyo katika lipi? kati ya Pierre na hao wasanii wake ambao daily wanshinda makahamani kwa kesi za hovyo hovyo,wanatukanana mitandaoni live, wanavujisha picha za ngono mitandaoni, wanabadili wanawake/mabwana kila uchwao na bado anawahusudu na kuwaona wa maana nani ni wa hovyo sasa?

Muache mzee wa watu aingize kipato chake kihalali, ilimradi havunji sheria za nchi.
Huyu jamaa ni housing tu ndio ya kiume ila motherboard yake ni ya kike kabisa, ana wivu na tabia za kike kike, hata dada zangu si kama yeye jamaa ni too much, halafu zero braini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama BBC wamemwona wakampa Airtime ni wasanii wangapi wakubwa hawaujui mlango wa BBC ? Bahati ya mtu usiilalie mlango wazi bwana [emoji16] huyu mtu ni wivu tu umemjaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mabadiliko yanaanza na wewe. Sio na makonda. Nadhani jana kafanya kitu tu bora kati ya vitu bora bila kujali aliwasilisha vipi lakin deep down ya hii issue tunahtaji kuwa serious kidogo kuwa nakizazi kinachojitambua

Tatizo teknolojia inatupeleka kasi sana kuzidi mahitaji yetu ya wakati husika

Dumelang
Too late for that mzee, ule ni ushauri tu, hauwez kumshurutisha mtu, yapo mambo mengi ya msingi ya kutufanya tuwe pamoja mfano mzuri ni report ya CAG hiyo ni big thing lakini umeona hata mahali inazungumziwa kuanzia tbc mpaka vyanzo vyote vya serikali. Ukiona wananchi wanapenda hivyo vitu ujue wamechoka na upuuzi na maigizo yanayoendelea
 
Kama BBC wamemwona wakampa Airtime ni wasanii wangapi wakubwa hawaujui mlango wa BBC ? Bahati ya mtu usiilalie mlango wazi bwana [emoji16] huyu mtu ni wivu tu umemjaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio tu bibi sii hadi Dachi Welle na mdogomdogo anaweza enda hadi si eni eni au kuhojiwa na Steve Sackur
 
So, Kenya ndio mfano wetu wa kuigwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
They are serious on issues than us. Tunataka au hatutaki. Kenya ni East African Business Hub.

Kenya wana uchumi mkubwa kuliko nchi yeyote Afrika Mashariki.

Kenya wana safaru yenye Nguvu kuliko sisi. Kenya wanafanya kazi uwezi linganisha na sisi.

Sasa usipojiringanisha na jirani mnaefanana unataka tukajiringanishe na Marekani?

Dumelang
 
Kama BBC wamemwona wakampa Airtime ni wasanii wangapi wakubwa hawaujui mlango wa BBC ? Bahati ya mtu usiilalie mlango wazi bwana [emoji16] huyu mtu ni wivu tu umemjaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Unazungumzia BBC gani? Siku hzi kuna BBC? Hii inayosikika na yenye wasikilizaji Tanzania tu. BBC iliokuwa nyepesi kama uji wa mgonjwa, ambayo kwenye page zake za insta inabishana na wanao comment?

Dumelang
 
Back
Top Bottom