Udharirishaji uliofanywa na Makonda jana kwa Pierre Liquid, si jambo la heri. Kwamba watu wa 'hovyo' kama Pierre ndio wanao pata umaarufu. Huu ni uwivu wa hali ya juu kama si udhahifu aliouonyesha jana.
Mbona yeye alitangaza 'nusu bei', kwa hiyo hakuona kwamba huu ni ulevi? Huyu mtu anatabia fulani ambayo inaudhi na inakera. Kila mtu anayo njia ya kujipatia ridhiki. Pierre si mlevi wa kutupwa kama vile tunavyoambiwa, lakini amejipatia umaarufu, na anatengeneza pesa. Sasa we Makonda anawashwa na nini?
Nimegundua kitu. Katika psychology, kuna kitu kinaitwa 'defence mechanism',
kwamba mwili au wewe mwenyewe unafanya kitu ili kuficha udhaifu fulani. Makonda hana vyeti, na tunajua historia yake ya elimu hadi kutumia jina la mtu, na hili amewahi kukili mwenyewe nyakati fulani jinsi alivyokuwa anaitafuta elimu hadi kuchoma mkaa huko Mbezi Luis. Sasa jana kwa kuwa ilikuwa ni harambee ya Jokate Mwegelo ya 'Tokomeza Zero', akakumbuka historia yake ya elimu, akahisi huenda watu wanamuwaza yeye, hivyo akatafuta pakufichia udhahifu wake, ikawa ni kwa Pierre. Huu si uungwana hata kidogo.
Pierre si Amba Rutty kwamba ameigiza video za ngono. Pierre siyo Jambazi wanaotusumbua na kuhatarisha amani yetu. Pierre si kahaba kwamba anajiuza. Pierre si malaya kwamba anaeneza magonjwa. Pierre si nabii wa uongo kwamba anatapeli watu kama ilivyo kwa wengi. Pierre si mwanasiasa anayefanya mikutano ya siasa. Pierre anatafuta ridhiki kama yeyote yule. Anatumia kipaji na umaarufu wake. Umaarufu katika dunia hii ndiyo pesa. Au tatizo ni kwamba ametangazwa na kuwa maarufu kuliko yeye? Tunajua, hapendi mtu amzidi umaarufu. Amwache Pierre atafute pesa.
Tunaomba Makonda atoe boriti ndani ya jicho lake kabla yakutoa kibanzi katika jicho la Pierre. Na unapomnyooshea mwenzako kidole, hakikisha vyako viko safi.
NB: Mods,naomba huu uzi usiunganishwe na mwingine wa tukio la jana. Haya ni maoni huru.
Sent using
Jamii Forums mobile app