Elections 2010 Alichokiomba Dr Slaa ni kusitisha kutangaza matokeo, sio Umwagaji damu

Wameingia bank kuu wakaiba pesa za EPA, leo kura iwashinde?
 
Tatizo ni nini lakini? Mtu anatoa hoja na maswali yake, kama ilivyodhamiriwa na JF. Mwingine hajibu chochote na kumtu-si tu kuwa wewe fisadi la ccm. Huo ni ujuha! Tena amecomment vizuri kuwa kutakuwepo amani, na mnamtukana. Kwa hiyo CHADEMA mnataka kuwa chama cha vurugu? Je, haki haiwezi kupatikana kwa amani? Nyinyi ndio wenye kuamini kuwa amani haiji ila kwa ncha ya upanga?

Tusipoziba ufa, tutajenga ukuta.
 
we mwanjelwa mtazamo wako wa mwanzo ulikuwa negative kwa Dr. Slaa wala usitake kujikoshwa kuwa ni Chadema baada ya kupewa live. Ondoka hapa na upuuzi wako

Sipingi, ni kweli. Niko negative hasa kwa hatua alichokua leo. Definetely niko disappointed mno hasa kwa kauli za leo. Never before.
 

Kama ulivyo Junior, unahitaji muda kuelewa mambo. Sheria si shida, hata ingekuwepo, bado kuna chances za kushindwa. Si kwamba sheria ikiwemo basi ukikata rufaa lazima ushinde. Mimi naongelea organisation kwa maana ya kujipanga kwa njia nzuri tu na si kuhamasisha vurugu. Ila sina hakika kama unaelewa. Muhimu tambua kuwa hata kama sheria ingekuwepo, siyo lazima ukikata rufaa ushinde.
 
Jamani mumsamehe tu huyu Mwanjelwa.

Inaonekana ni lifisadi flani linalomvulia suruali makamba.
 

Kama angesimamia huko mimi pia ningeunga mkono. Ninachochelea ni ile kauli ya uchochezi. Kwamba amepokea simu kutoka sehemu kadhaa na kama wakiamua hakuna cha CCM wala Chadema wala yoyote! Kura zihesabiwe kweli na naunga mkono sana. Asije rudia kauli yake ya kinazi na ya kichochezi tena. That was uncalled for and wrongly timed
 


Nina mashaka na uraia wako.

Mtu uko nyumbani kwako, unaibiwa na mwizi unamwona, badala ya kumkamata unasema Nimepiga simu polisi, wanakuja kumkamata!

Hahahaha! Duh!

Nakuhurumia!
 
Waislamu oyeeeee, waikristu nendeni mkandamane kanisani tutaonana 2015.
 
Waislamu oyeeeee, waikristu nendeni mkandamane kanisani tutaonana 2015.

wewe jamaa umevamili hili jamvi na ukuendeleza maneno yako hayo unaweza kula ban. ok poa nitarudi badae kukujibu ,wewe kwanza unaonekana ni kundi la watu waliojiunga ndani ya siku za hivi karibuni ndani ya hao watu kuna mamluki kibao wametumwa sasa ww sijui nani kakutuma mpaka ss hivi sijapata picha
 

Kuna watu wamesafiri toka mkoa mmoja kwenda mwingine, na wengine kuvuka mikoa kadhaa kwenda kupiga kura. Hii inaonyesha thamani ya kura ya mtu ikoje. Wanatambua kuwa KURA ndo njia ya AMANI ya kudai haki kwa walio wanyonge na wasio wanyonge. Haki hii ikihujumiwa na mtu akadai AMANI kwanza, lazima aanze kutafuta tafsiri ya neo AMANI. Njia kuu ya amani ni kutatua mambo kwa HAKI, yaani TUME kukubali kuwa IMEUMBUKA.

Karne za mbumbumbu zimeisha. Naamni kuwa MASKINI JEURI hudai haki yake kwa amani LAKINI akikandamizwa anakubali umwite majina yoyote.....

Kwakuwa TUME imewekwa na UMMA, na kwa kuwa UMMA ndo wanataka iwe hivi, KIAONGOZI makini anapaswa kutanguliza busara zaidi ya ubabe.

Mungu fumbua masikio ya wote wanaoamini ktk kutumia ndguvu kuwa UTULIVU wa muda mrefu wa Wa Tanzania ni kama UTULIVU tu. Usiombe watu wavumilivu wakakosa UVUMILIVU......

Ni vema TUME ikalitambua hili, wa Tanzania ni wastaarabu sana. Wanajua kuwa wasipolidai hili, baada ya kutangazwa rasmi mshindi, hawawezi kisheria kandamizi kusilizwa....
 

Mwanjelwa said:
Ninachochelea ni ile kauli ya uchochezi
CCM OYEE said:
Waislamu oyeeeee, waikristu nendeni mkandamane kanisani tutaonana 2015.
mabeja said:
Huyo Slaa amepoteza dira. Ameona Maalimu Seif ameula na yeye anataka apate umakamu kwa kulazimisha. Asubiri katiba ibadilishwe kwanza ndiyo atapata umakamu. Asitutishie na watanzania hatuko kwenye kumwaga damu. Labda damu yake ndiyo imwagike!!
"Ukikuta mahali mawazo ya vijana na wazee yanafanana, ujue hapo pamedumaa" - J. S.Warioba.
 

wewe kilaza ni nini kiwango cha busara? busara yako wewe mjinga haiwezi hata kidogo kui-chalenge busara ya werevu,
kama umesoma katiba ungekuwa unajua kuwa tume imepewa mamlaka ya kupitiliza kwa maana ikisha mtangaza mshindi wa urais hakuna kupinga kwa namna yeyote, ndio maana Dr. anapinga before kutangaza ili kwenda sambamba na matakwa ya sheria.
ubunge unaruhusiwa kupinga mahakamani wakati wowote, pia kwa taarifa yako sheria imetungwa kuelekeza mahakama kusikiliza haraka kezi za uchaguzi(ubunge) ccm inatumia mijitu mijinga kama wewe inayodhani ina busara kumbe haina tofauti na mav..., hebu onyesha utofauti wako na nyani basi!!!!!!!!!!!
 

Wewe umezidi kuwa na pupa, labda pia analytical skills ziko low. Soma thread nzima baadaye ndiyo utoe mawazo yako.
 
Hii thread imebadilishwa jina, labda kwa sababu zake binafsi mod. Kauli ya mheshimiwa Slaa inabakia kwenye records za nchi kama moja ya kauli kali za kichochezi kuwahi kutolewa na mtu wa calibre baada ya zile za Mtikila miaka ya 1993-1997. Unaposema "unapigiwa simu na watu wa Shinyanga na maeneo mengine watu wakikuuliza wafanye nini na baadaye kusema kuwa unaweza wafanya watu waingie mitaani" hii ina maanisha kujaribu kutibua taratibu za kawaida za shughuli za watu na kuwarengeshea watu hao wauwawe. Na hii kauli inatolewa na Padre, ambaye kila mmoja Duniani angetegemea yeye awe wa kwanza kusimamia misingi ya amani na utengano wa kisheria kwa kushirikisha imani za kiroho.

Nilimfurahia sana. Nimetumbukia nyongo.
 
Imeonekana kuna ARI ZAIDI ya kuchakachua demokrasia ya wananchi,NGUVU ZAIDI kama inavyotumiwa sasa na vyombo vya dola,KASI ZAIDI ya wizi na ufisadi.Mwanjelwa Mahakama ipi hiyo wakati ushindi wa Rais haupingwi mahakamani.Watu mitaani washachoka na ubabaishaji ,mtu asikwambie eti upinzani utaleta fujo,kwanza kwa kipi walichonacho,DOLA ipo upande wa CCM.CCM ndio watakaoanzisha fujo kwani wamezoea kula kwa mrija
 
Alichodai Dr. Slaa ni uhakiki wa kura upya kwa kulinganisha na takwimu alizonazo zilizowakilishwa na mawakala na kusainiwa na Returning Officers walioajiriwa na serikali hiihii. Kuna ubaya gani kufanya hivyo ili kujiridhiha pande zote tatu yaani mgombea anayedaiwa kushinda, mgombea anayedaiwa kushindwa na wananchi wenye mashaka ya kura zao kuchakachuliwa na tume iliyopoteza sifa ya impartiality kwa jinsi ilivyohandle utoaji wa matokeo.
Hapa napata shaka kama takwimu zinazosomwa na NEC si za kupikwa na "Usalama wa taifa". Mimi naamini, zoezi la uhakiki wa hesabu walizopata wagombea hawa wawili lingetekelezwa, lingemwongezea mshindi heshima mbele ya watanzania ambao sasa wameichukia CCM, Kikwete na hata watu wanaojihusisha nayo, jamani tatizo liko wapi hapa kuhesabu moja na moja na moja na mia mbili na..... ni kazi kubwa mno zaidi kuliko kukabiliwa na chuki na zahama toka kwa watu wanaoamini wameporwa ushindi? Mtu asiniambie ati Katiba haisemi hivyo; huo utakuwa upumbavu wa kupindukia kwa vile ni Katiba hiyohiyo haijasema chochote juu ya serikali ya umoja wa kitaifa kule Zanzibar ila ilifanyika vile kulinusuru taifa na siasa za chuki na uhasama. Tunawasihi wenye busara wasipinge uhakikiwa kura kishabiki bali waweke maslahi ya taifa mbele. Sote tumeshuhudia na tumeona kwa macho yetu majibu yaliyokuwa yamebandikwa ya matokeo ya kura alizopata Kikwete, Slaa na wengine ambazo baadhi ni tofauti kabisa na zile zilizotangazwa kule zilikopigwa; sasa tumwamini nani, Tume ambayo imepelekewa taarifa au wadau wenye nakala za matokeo toka sehemu kura zilikopigwa zikiwa zimethibitishwa na vyombo halali?
 
Kuhakiki kura kila mtu anaunga mkono, kama ni lazima, anyway. Hapa tunaongelea kauli zake za kinazi. Kauli za kichochezi. Kauli ambazo mdomoni mwa mtu wa aina yake, kisiasa, kijamii na kidini, hazikutarajiwa.
 
Kuhakiki kura kila mtu anaunga mkono, kama ni lazima, anyway. Hapa tunaongelea kauli zake za kinazi. Kauli za kichochezi. Kauli ambazo mdomoni mwa mtu wa aina yake, kisiasa, kijamii na kidini, hazikutarajiwa.

crap.... jambazi na fisadi la kupindukia wewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…