emmarki
JF-Expert Member
- Nov 22, 2012
- 1,001
- 1,430
Alichokisema Nabii #Bashando "Mimi ni miongoni mwa watu ambao sikuuelewa kabisa ufunuo wa nywele na kucha wa Nabii Suguye, na niliukosoa hadharani, ila pamoja na kutokuuelewa haunipi sababu ya kushangilia huduma ya WRM kufungwa.
Hapa kuna jambo ambalo watu wengi hatuelewi.
Ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya Suguye na WRM, ambapo Suguye ni mwenyekiti wa taasisi ya WORD OF RECONCILIATION MINISTRY (WRM) na mtu ambaye Mungu anamtumia katika huduma ya kinabii, na WORD OF RECONCILIATION MINISTRY ni kanisa ambalo watu wanakusanyika kumwabudu Mungu.
Hivyo basi kufunga kanisa la WRM siyo kumkomoa Nabii Suguye bali ni kuwakomoa watu elfu nne waliyoamua kuabudu ndani ya kanisa la WRM.
Ndiyo maana Suguye alisafiri kwenda Marekani lakini WRM ikaendelea na shughuli zake hapa Tanzania. Kilio changu kikubwa mimi kama mwenyekiti wa UMOJA WA HUDUMA ZA KITUME NA KINABII TANZANIA (UHKKT), ni watu elfu nne kunyimwa haki yao ya kikatiba ya kuabudu.
Lakini pia ni kuipunguzia serikali mapato ya fedha za kigeni ambazo watu kutoka mataifa mbalimbali walikuwa wanakuja Tanzania kwa ajili ya kufuata maombi katika huduma ya WRM.
Nirudi kwenye swala la ufunuo wa kucha na nywele, inawezekana Nabii Suguye akawa alionyeshwa na Mungu au lah.. Lakini hata kama ufunuo ule ulikuwa haujaeleweka au una makosa ndani yake, siyo jukumu la serikali kuingilia kati huo ufunuo maana serikali haina dini, na katiba imetoa uhuru wa watu kuabudu bila serikali kuingilia..
Serikali inaweza kuingilia kati ibada ambayo itajumuisha jinai ndani yake... Kwa mfano ningesikia Nabii Suguye amekamatwa kwa sababu ametuhumiwa kuuza madawa ya kulevya, kubaka, kuiba, kuua, au kuvunja sheria za nchi kwa namna yeyote ile, hapo nisingefungua mdomo wangu kuongea, ningesubiria kuona mahakama ikitenda haki..
Ndiyo maana siku ya kwanza tu nilipopewa taarifa kuwa huduma ya WRM imefungwa nilipiga simu kwa Msajili na kumuuliza kuna jinai gani imegunduliwa katika huduma ya WRM? Na nilipopewa jibu nikamtafuta Nabii Suguye na uongozi wake bila mafanikio hadi hapa juzi nilipofanikiwa kuonana na Nabii Suguye uso kwa uso ndipo nikasikiliza kwa upande wake na kubaini baadhi ya makosa ndipo nikaamua kusimama na Nabii Nicolous Paul Suguye .
Kama tatizo ni ufunuo wa kucha na nywele naamini BARAZA LA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE TANZANIA (CPCT) lipo na lina mamlaka ya kumuita kiongozi yeyote wa imani ya kipentekoste na kumuhoji na kutafuta busara ya kuondoa sintofahamu iliyojitokeza kwenye jamii..
Lakini kwa kuwa huduma ya Suguye siyo mwanachama wa CPCT bado CPCT wangeweza kuutumia UMOJA WA HUDUMA ZA KITUME NA KINABII TANZANIA kumuita Suguye na kukutana nae kwa kikao cha kuondoa sintofahamu iliyojitokeza, maana kucha na nywele ni swala la kiimani ambalo lingeweza kutatuliwa na baraza na chama cha imani husika.
Tukija kuruhusu mambo haya yaingiliwe na serikali kwanza tutakuwa tunafungua mlango wa serikali kuendesha ibada zetu na huko mbeleni tutashindwa hata kulitaja jina la Yesu Kristo na kuanza kusifia watawala na sera zao, na jambo la pili ni kupunguza nguvu kwenye baraza na umoja wa huduma...
Ushauri wangu kwa mitume na manabii wote wa Tanzania, msiyadharau haya mabaraza wala vyama ambavyo vina dhamana kisheria ya kutafsiri imani mbele ya serikali, ni vizuri kabisa kuomba uanachama na kujiunga ili serikali inapowatafuta iwakute huko ndani, lakini pia muwe na nguvu ya kushiriki uchaguzi wa kuchagua viongozi ambao hawatakuwa na udhehebu wa kutumia vibaya nafasi zao kuchongea watu wa imani ambazo hawajazielewa..
Najua kwenye utumishi kuna makosa mengi sana na katika makosa hayo inabidi kupata viongozi wanaoweza kulea na kuonya kwa upendo kwa kusudi la kurekebisha na siyo kukomoa kwa maslahi ya kidini na kidhehebu...
Ile dhana ya kusema unajitenga peke yako ili uweze kufanya huduma kiutulivu, hautaki chama wala baraza siyo njema sana, jitahidini kushirikiana na baraza na chama kwa maslahi ya mwili wa Kristo....
Namalizia kwa kusema, kama serikali imeweza kumtikisa mtumishi mkubwa kama Suguye, vipi mimi na wewe ambao ndiyo tunaanza huduma? Ninavyosimama na Suguye simuoni yeye kama Suguye ila ninaona hatari kwa watumishi wadogo mnaoanza huduma na hamna hata usajili, tukilinyamazia hili kwa kweli huko mbele mambo yatakuja kuwa magumu kama ilivyo nchi ya Rwanda.
Nimeona comment za watumishi wanaoanza huduma wakicheka na kufurahi kwa kilichoipata huduma ya WRM nikakumbuka usemi ambao Yesu alisema, "HERI MNAOCHEKA SASA KWA MAANA MTALIA NA KUSAGA MENO....
Mimi Mhashamu Baba Askofu Bashando nasimama na Nabii Nicholaus Suguye 🙏
Hapa kuna jambo ambalo watu wengi hatuelewi.
Ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya Suguye na WRM, ambapo Suguye ni mwenyekiti wa taasisi ya WORD OF RECONCILIATION MINISTRY (WRM) na mtu ambaye Mungu anamtumia katika huduma ya kinabii, na WORD OF RECONCILIATION MINISTRY ni kanisa ambalo watu wanakusanyika kumwabudu Mungu.
Hivyo basi kufunga kanisa la WRM siyo kumkomoa Nabii Suguye bali ni kuwakomoa watu elfu nne waliyoamua kuabudu ndani ya kanisa la WRM.
Ndiyo maana Suguye alisafiri kwenda Marekani lakini WRM ikaendelea na shughuli zake hapa Tanzania. Kilio changu kikubwa mimi kama mwenyekiti wa UMOJA WA HUDUMA ZA KITUME NA KINABII TANZANIA (UHKKT), ni watu elfu nne kunyimwa haki yao ya kikatiba ya kuabudu.
Lakini pia ni kuipunguzia serikali mapato ya fedha za kigeni ambazo watu kutoka mataifa mbalimbali walikuwa wanakuja Tanzania kwa ajili ya kufuata maombi katika huduma ya WRM.
Nirudi kwenye swala la ufunuo wa kucha na nywele, inawezekana Nabii Suguye akawa alionyeshwa na Mungu au lah.. Lakini hata kama ufunuo ule ulikuwa haujaeleweka au una makosa ndani yake, siyo jukumu la serikali kuingilia kati huo ufunuo maana serikali haina dini, na katiba imetoa uhuru wa watu kuabudu bila serikali kuingilia..
Serikali inaweza kuingilia kati ibada ambayo itajumuisha jinai ndani yake... Kwa mfano ningesikia Nabii Suguye amekamatwa kwa sababu ametuhumiwa kuuza madawa ya kulevya, kubaka, kuiba, kuua, au kuvunja sheria za nchi kwa namna yeyote ile, hapo nisingefungua mdomo wangu kuongea, ningesubiria kuona mahakama ikitenda haki..
Ndiyo maana siku ya kwanza tu nilipopewa taarifa kuwa huduma ya WRM imefungwa nilipiga simu kwa Msajili na kumuuliza kuna jinai gani imegunduliwa katika huduma ya WRM? Na nilipopewa jibu nikamtafuta Nabii Suguye na uongozi wake bila mafanikio hadi hapa juzi nilipofanikiwa kuonana na Nabii Suguye uso kwa uso ndipo nikasikiliza kwa upande wake na kubaini baadhi ya makosa ndipo nikaamua kusimama na Nabii Nicolous Paul Suguye .
Kama tatizo ni ufunuo wa kucha na nywele naamini BARAZA LA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE TANZANIA (CPCT) lipo na lina mamlaka ya kumuita kiongozi yeyote wa imani ya kipentekoste na kumuhoji na kutafuta busara ya kuondoa sintofahamu iliyojitokeza kwenye jamii..
Lakini kwa kuwa huduma ya Suguye siyo mwanachama wa CPCT bado CPCT wangeweza kuutumia UMOJA WA HUDUMA ZA KITUME NA KINABII TANZANIA kumuita Suguye na kukutana nae kwa kikao cha kuondoa sintofahamu iliyojitokeza, maana kucha na nywele ni swala la kiimani ambalo lingeweza kutatuliwa na baraza na chama cha imani husika.
Tukija kuruhusu mambo haya yaingiliwe na serikali kwanza tutakuwa tunafungua mlango wa serikali kuendesha ibada zetu na huko mbeleni tutashindwa hata kulitaja jina la Yesu Kristo na kuanza kusifia watawala na sera zao, na jambo la pili ni kupunguza nguvu kwenye baraza na umoja wa huduma...
Ushauri wangu kwa mitume na manabii wote wa Tanzania, msiyadharau haya mabaraza wala vyama ambavyo vina dhamana kisheria ya kutafsiri imani mbele ya serikali, ni vizuri kabisa kuomba uanachama na kujiunga ili serikali inapowatafuta iwakute huko ndani, lakini pia muwe na nguvu ya kushiriki uchaguzi wa kuchagua viongozi ambao hawatakuwa na udhehebu wa kutumia vibaya nafasi zao kuchongea watu wa imani ambazo hawajazielewa..
Najua kwenye utumishi kuna makosa mengi sana na katika makosa hayo inabidi kupata viongozi wanaoweza kulea na kuonya kwa upendo kwa kusudi la kurekebisha na siyo kukomoa kwa maslahi ya kidini na kidhehebu...
Ile dhana ya kusema unajitenga peke yako ili uweze kufanya huduma kiutulivu, hautaki chama wala baraza siyo njema sana, jitahidini kushirikiana na baraza na chama kwa maslahi ya mwili wa Kristo....
Namalizia kwa kusema, kama serikali imeweza kumtikisa mtumishi mkubwa kama Suguye, vipi mimi na wewe ambao ndiyo tunaanza huduma? Ninavyosimama na Suguye simuoni yeye kama Suguye ila ninaona hatari kwa watumishi wadogo mnaoanza huduma na hamna hata usajili, tukilinyamazia hili kwa kweli huko mbele mambo yatakuja kuwa magumu kama ilivyo nchi ya Rwanda.
Nimeona comment za watumishi wanaoanza huduma wakicheka na kufurahi kwa kilichoipata huduma ya WRM nikakumbuka usemi ambao Yesu alisema, "HERI MNAOCHEKA SASA KWA MAANA MTALIA NA KUSAGA MENO....
Mimi Mhashamu Baba Askofu Bashando nasimama na Nabii Nicholaus Suguye 🙏