Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
cult ni imani kama ilivyo dhehebu lako unalo abudu, serikali haitakiwi kuingilia imani ya mtu yeyote kama hamna kosa lolote linalovunja sheria za nchi.
Ni rahisi sana kumsilimisha mkristo yeyote awe padri,askofu,mlei,mtawa sijui fratel nk kuwa muislamu ila ni ngumu sana kumfanya muislamu hata asieswali wala kupitia madrasa kuwa mkristo
We utakuwa mpumbavu hakika,unadhani isiponyesha mvua hao watu wa serikali watakufa njaa?Waache kutafuta huruma mitandaoni. Wafanye kama manabii wengine walivyofanya. Nabii Eliya alivyoona anaonewa na dola alifunga anga mvua isinyeshe. Sasa zamu ya Suguye kusimama kama Nabii
Hakuna kufunguliwa, njaa hadi iwatie adabu, kwanza uaskofu umepewa na nani ww? Mnapeana majina kila aina kutafuta fedha, mara Nabii, mara askofu, mara mtume, serikali imefanya uamuzi mzuri sana, sisi tunasimama na serikali
Ni rahisi sana kumsilimisha mkristo yeyote awe padri,askofu,mlei,mtawa sijui fratel nk kuwa muislamu ila ni ngumu sana kumfanya muislamu hata asieswali wala kupitia madrasa kuwa mkristo
Sasa tunashindana na Nigeria kuwa na matapeli wanaojiita manabii. Ningekuwa rais wangekimbia nchi. Angalia Rwanda, hawana upuuzi huu wa manabii wa urongoAlichokisema Nabii #Bashando "Mimi ni miongoni mwa watu ambao sikuuelewa kabisa ufunuo wa nywele na kucha wa Nabii Suguye, na niliukosoa hadharani, ila pamoja na kutokuuelewa haunipi sababu ya kushangilia huduma ya WRM kufungwa.
Hapa kuna jambo ambalo watu wengi hatuelewi.
Ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya Suguye na WRM, ambapo Suguye ni mwenyekiti wa taasisi ya WORD OF RECONCILIATION MINISTRY (WRM) na mtu ambaye Mungu anamtumia katika huduma ya kinabii, na WORD OF RECONCILIATION MINISTRY ni kanisa ambalo watu wanakusanyika kumwabudu Mungu.
Hivyo basi kufunga kanisa la WRM siyo kumkomoa Nabii Suguye bali ni kuwakomoa watu elfu nne waliyoamua kuabudu ndani ya kanisa la WRM.
Ndiyo maana Suguye alisafiri kwenda Marekani lakini WRM ikaendelea na shughuli zake hapa Tanzania. Kilio changu kikubwa mimi kama mwenyekiti wa UMOJA WA HUDUMA ZA KITUME NA KINABII TANZANIA (UHKKT), ni watu elfu nne kunyimwa haki yao ya kikatiba ya kuabudu.
Lakini pia ni kuipunguzia serikali mapato ya fedha za kigeni ambazo watu kutoka mataifa mbalimbali walikuwa wanakuja Tanzania kwa ajili ya kufuata maombi katika huduma ya WRM.
Nirudi kwenye swala la ufunuo wa kucha na nywele, inawezekana Nabii Suguye akawa alionyeshwa na Mungu au lah.. Lakini hata kama ufunuo ule ulikuwa haujaeleweka au una makosa ndani yake, siyo jukumu la serikali kuingilia kati huo ufunuo maana serikali haina dini, na katiba imetoa uhuru wa watu kuabudu bila serikali kuingilia..
Serikali inaweza kuingilia kati ibada ambayo itajumuisha jinai ndani yake... Kwa mfano ningesikia Nabii Suguye amekamatwa kwa sababu ametuhumiwa kuuza madawa ya kulevya, kubaka, kuiba, kuua, au kuvunja sheria za nchi kwa namna yeyote ile, hapo nisingefungua mdomo wangu kuongea, ningesubiria kuona mahakama ikitenda haki..
Ndiyo maana siku ya kwanza tu nilipopewa taarifa kuwa huduma ya WRM imefungwa nilipiga simu kwa Msajili na kumuuliza kuna jinai gani imegunduliwa katika huduma ya WRM? Na nilipopewa jibu nikamtafuta Nabii Suguye na uongozi wake bila mafanikio hadi hapa juzi nilipofanikiwa kuonana na Nabii Suguye uso kwa uso ndipo nikasikiliza kwa upande wake na kubaini baadhi ya makosa ndipo nikaamua kusimama na Nabii Nicolous Paul Suguye .
Kama tatizo ni ufunuo wa kucha na nywele naamini BARAZA LA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE TANZANIA (CPCT) lipo na lina mamlaka ya kumuita kiongozi yeyote wa imani ya kipentekoste na kumuhoji na kutafuta busara ya kuondoa sintofahamu iliyojitokeza kwenye jamii..
Lakini kwa kuwa huduma ya Suguye siyo mwanachama wa CPCT bado CPCT wangeweza kuutumia UMOJA WA HUDUMA ZA KITUME NA KINABII TANZANIA kumuita Suguye na kukutana nae kwa kikao cha kuondoa sintofahamu iliyojitokeza, maana kucha na nywele ni swala la kiimani ambalo lingeweza kutatuliwa na baraza na chama cha imani husika.
Tukija kuruhusu mambo haya yaingiliwe na serikali kwanza tutakuwa tunafungua mlango wa serikali kuendesha ibada zetu na huko mbeleni tutashindwa hata kulitaja jina la Yesu Kristo na kuanza kusifia watawala na sera zao, na jambo la pili ni kupunguza nguvu kwenye baraza na umoja wa huduma...
Ushauri wangu kwa mitume na manabii wote wa Tanzania, msiyadharau haya mabaraza wala vyama ambavyo vina dhamana kisheria ya kutafsiri imani mbele ya serikali, ni vizuri kabisa kuomba uanachama na kujiunga ili serikali inapowatafuta iwakute huko ndani, lakini pia muwe na nguvu ya kushiriki uchaguzi wa kuchagua viongozi ambao hawatakuwa na udhehebu wa kutumia vibaya nafasi zao kuchongea watu wa imani ambazo hawajazielewa..
Najua kwenye utumishi kuna makosa mengi sana na katika makosa hayo inabidi kupata viongozi wanaoweza kulea na kuonya kwa upendo kwa kusudi la kurekebisha na siyo kukomoa kwa maslahi ya kidini na kidhehebu...
Ile dhana ya kusema unajitenga peke yako ili uweze kufanya huduma kiutulivu, hautaki chama wala baraza siyo njema sana, jitahidini kushirikiana na baraza na chama kwa maslahi ya mwili wa Kristo....
Namalizia kwa kusema, kama serikali imeweza kumtikisa mtumishi mkubwa kama Suguye, vipi mimi na wewe ambao ndiyo tunaanza huduma? Ninavyosimama na Suguye simuoni yeye kama Suguye ila ninaona hatari kwa watumishi wadogo mnaoanza huduma na hamna hata usajili, tukilinyamazia hili kwa kweli huko mbele mambo yatakuja kuwa magumu kama ilivyo nchi ya Rwanda.
Nimeona comment za watumishi wanaoanza huduma wakicheka na kufurahi kwa kilichoipata huduma ya WRM nikakumbuka usemi ambao Yesu alisema, "HERI MNAOCHEKA SASA KWA MAANA MTALIA NA KUSAGA MENO....
Mimi Mhashamu Baba Askofu Bashando nasimama na Nabii Nicholaus Suguye 🙏
View attachment 2469637
Tatizo mnafikiri kila kinachoitwa Kanisa ni Kanisa.KAMA swala ni kumuabudu Mungu mwenyezi, Mungu mkuu, Mungu wa kweli, Jehovah, Yesu Kristo aliye hai hata nyumba ya ibada ifungiwe kanisa litaishi milele
MATHAYO 16:18
"Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda."
YOHANA 4:23
"Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu."
Uzuri wake hawa manabii huwa hawagongi hodi nyumbani kwa mtu kuwaita waje kusali na kutoa sadaka.Ni watu wenyewe kutaka ku-fasttrack hata mambo ya Rohoni ndiyo yanayowakosti wahanga.na wataendelea kupigwa."Ukiijua kweli itakuweka huru na utakuwa huru kweli kweli"Hawa manabii kwa kweli naomba Mungu anisamehe ulaji Sanaa upo mbele.
Tatizo mnafikiri kila kinachoitwa Kanisa ni Kanisa.
Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
Huo ndio ukweli acha kujifariji hivi nikuulize kati ya waislamu na wakristo nani wanaongoza kusilimu? Kwahuku wilaya ya masasi kila ukiokawa ukoo wa wakristo tupu kuna waislamu na vile vijiji ambavyo kulikuwa na ukristo tupu saivi kuna waislamu kibao wanawake na wanaume wanasilimu balaa sanaSio rahisi kama unavyofikiria
Mbona hawasilimishwi? Hao wanaenda kwa mwamposa kama kwa mganga wa kienyeji tuHawa waislamu wanaomsifu bwana kwa Mtume Mwamposa?
Huu ni Ushirikina na sio Ukiristo- Huyu asipewe usajiri kwani ipo siku atakuja na mambo ya Kibwetere wa UgandaNywelena kucha amekwenda mbali Sana Bora angewaita wawaombe kimya kimya
Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Basi imekuwa tofauti, sisi huku nyanda ya juu kusini tunaufuta uislamu. Kila mkutano wa injili tunaofanya kuna waislamu wanaokoka. Wiki iliyopita kuna shehe wa BAKWATA wilaya moja aliokoka maana tulimuombea na akatokwa mapepo na sasa anamtumikia Yesu aliye hai. Huko Masasi ni eneo lenye waislamu wengi na binafsi nieleweshe huyo/hao wakristu wanabadilisha dini au mnakutana nao vipi hadi abadili dini zaidi ya mbinu yenu ya kuoa wakristo?Huo ndio ukweli acha kujifariji hivi nikuulize kati ya waislamu na wakristo nani wanaongoza kusilimu? Kwahuku wilaya ya masasi kila ukiokawa ukoo wa wakristo tupu kuna waislamu na vile vijiji ambavyo kulikuwa na ukristo tupu saivi kuna waislamu kibao wanawake na wanaume wanasilimu balaa sana