Alichokisema nabii Bashando baada ya huduma WRM iliyo chini ya nabii Suguye kufungiwa

cult ni imani kama ilivyo dhehebu lako unalo abudu, serikali haitakiwi kuingilia imani ya mtu yeyote kama hamna kosa lolote linalovunja sheria za nchi.

Cult sio dhehebu, ni imani kwa mwasisi wa dini sio Mungu. Akina kibwetere, Akina Jim Jones akaaua maelfu ya watu, akina David koreshi na juzi hapa Tanzania mungu Zumaridi.
 
Mambo ya aibu yanatokea kanisani mpaka serikali imeingilia Kati. Huku Zumaridi anajiita mungu huku Suguye na kucha zake. Mambo ya ajabu Sana,
 
Serikali iongeze kibano dhidi ya hawa wajasiriamali wa Injili, waabudu mashetani, occultic prophets wanaojificha nyuma ya neno ufunuo. Wakiacha wakaota mizizi kama Nigeria au South Africa taifa litakuwa kwenye hali mbaya sana. Hakuna jina lingine alilopewa mwanadamu limpasalo kuokolewa kwalo zaidi ya jina la Yesu. Kutumia visaidizi kama chumvi, maji au mafuta ni ushirikana kama ushirikana mwingine tu.
 
Waache kutafuta huruma mitandaoni. Wafanye kama manabii wengine walivyofanya. Nabii Eliya alivyoona anaonewa na dola alifunga anga mvua isinyeshe. Sasa zamu ya Suguye kusimama kama Nabii
We utakuwa mpumbavu hakika,unadhani isiponyesha mvua hao watu wa serikali watakufa njaa?

Hizi sijui ni roho za kichawi hizi?!Watu wafe njaa kwa sababu ya suguye?
Hivi hujui hata wachawi wanafunga mvua isinyeshe wakipata watu wajinga kama wewe?!

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna kufunguliwa, njaa hadi iwatie adabu, kwanza uaskofu umepewa na nani ww? Mnapeana majina kila aina kutafuta fedha, mara Nabii, mara askofu, mara mtume, serikali imefanya uamuzi mzuri sana, sisi tunasimama na serikali

Kwani kuna sehemu maalumu ama utaratibu maalumu wa kupewa hayo majina?naomba unielekeze hiyo sehemu.
 
Ni rahisi sana kumsilimisha mkristo yeyote awe padri,askofu,mlei,mtawa sijui fratel nk kuwa muislamu ila ni ngumu sana kumfanya muislamu hata asieswali wala kupitia madrasa kuwa mkristo

Sio rahisi kama unavyofikiria
 
Sasa tunashindana na Nigeria kuwa na matapeli wanaojiita manabii. Ningekuwa rais wangekimbia nchi. Angalia Rwanda, hawana upuuzi huu wa manabii wa urongo
 
Hawa ni wachumia tumbo. Ukristo unachezewa sababu ndio dini pekee ukiwa na biblia unaweza kufanya chochote kwa jina la Ukristo!

Serikali haipaswi kuingilia lakini hata hilo baraza lao ni waganga njaa na wenye matendo binafsi yanayowafanya wasiweze kukemeana! Bora mchungaji mdhambi kuliko anayetumia maandiko kupotosha imani.

Kutafuta ugali kwa jina la muumba hapana! Bashando ambaye siku hizi ni chawa wa nabii kama yule wa Arusha ni dhahiri hamtetei Kristo. Hukumu mbinguni ipo ndugu zangu!

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Tatizo mnafikiri kila kinachoitwa Kanisa ni Kanisa.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Biashara mpya imezuka ya kuuza maji na mafuta. Mwenye kanisa (Kristo Yesu) akawaonya wafuasi wake miaka hiyo kama anavyoonya leo. "na manabii wengi wa uongo watatokea... nao WATAWADANGANYA WENGI" Angalia, usiwe miongoni wa wajinga wanaodanganywa.
 
Hawa manabii kwa kweli naomba Mungu anisamehe ulaji Sanaa upo mbele.
Uzuri wake hawa manabii huwa hawagongi hodi nyumbani kwa mtu kuwaita waje kusali na kutoa sadaka.Ni watu wenyewe kutaka ku-fasttrack hata mambo ya Rohoni ndiyo yanayowakosti wahanga.na wataendelea kupigwa."Ukiijua kweli itakuweka huru na utakuwa huru kweli kweli"
 
Sio rahisi kama unavyofikiria
Huo ndio ukweli acha kujifariji hivi nikuulize kati ya waislamu na wakristo nani wanaongoza kusilimu? Kwahuku wilaya ya masasi kila ukiokawa ukoo wa wakristo tupu kuna waislamu na vile vijiji ambavyo kulikuwa na ukristo tupu saivi kuna waislamu kibao wanawake na wanaume wanasilimu balaa sana
 
Basi imekuwa tofauti, sisi huku nyanda ya juu kusini tunaufuta uislamu. Kila mkutano wa injili tunaofanya kuna waislamu wanaokoka. Wiki iliyopita kuna shehe wa BAKWATA wilaya moja aliokoka maana tulimuombea na akatokwa mapepo na sasa anamtumikia Yesu aliye hai. Huko Masasi ni eneo lenye waislamu wengi na binafsi nieleweshe huyo/hao wakristu wanabadilisha dini au mnakutana nao vipi hadi abadili dini zaidi ya mbinu yenu ya kuoa wakristo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…