Ki-msingi hakuna ugomvi kati ya diamond na baba yake. Kilichopo ni uelewa mdogo wa diamond. Diamond aliwekewa UKUTA na mama yake kwa kuelezwa(kupitia dhiki walizopitia) na kuaminishwa kuwa,zile shida zote,za kukosa Ada,viatu,uniform,chakula nk. Zilisababishwa na baba yake. Maneno hayo ukimueleza mtoto mdogo,ktk kipindi cha shida,hayamtoki!!
Kwa hiyo hata baada ya kukua,diamond aliendelea kuamini kile alichoelezwa na mama yake na amekishika hadi leo akiamini maisha yote mabaya aliyopitia yalitokana na kutengana kwa wazazi wake na baba kuondoka!!
Hili ni kosa la mama diamond kuweka ukuta(chuki) kati ya mtoto na baba. Lkn hakumueleza sababu za kutengana kwao. Diamond naye anafanya ujinga uleule kwa kumuadhibu baba yake,huku mafanikio yake wala hayatokani na mama yake. Mama yake hakuwa mwanamuziki kusema alilirithi,wala hayatokani na elimu aliyomsomesha. Shule hakumpeleka na hata darasani hakuwa na akili kutokana na lishe duni. Na hili la kukosa akili ndo linaendelea mpaka leo. Maana hata kukosa uwezo wa kutafsiri Jambo ni ukosefu wa akili. Kifupi mama yake na diamond ndo aliyemharibu diamond na yote anayofanya Domo kwa sasa ni matokeo tu..!!