Alikiba yuko wapi

na wewe umeliona... mi mara ya kwanza nilipoona term nilijua ni typing error, oooh nikaiona term kwa mara ya pili, mara chambani, mara arakeli, lol

that all u can comment??? sasa nikupe kazi naona utaiweza, uwe unapitia post zangu uniambie nilipochapia. malipo ni muda wako.
 

Unakosea sana. Aidha hujui muziki, au unasukumwa na ushabiki. Mwana ni wimbo wa kwanza wa Bongo Flava kwa siku za karibuni kutamba bila ya kuwa na video.
Elewa kwamba, wanamuziki wengi wa Bongo wanaongea kwenye midundo ya muziki, hawaimbi. Ila Ali Kiba anajua kuimba, na zaidi anajua sana kuandika. Kiba ni baba lao.
Ova
 

Hiyo inaitwa "kufa kufaana" kwa upepo huu kiba hana budi kukausha hadi msimu wa diamond upite..
 

Hiv kweli unafuatilia mziki.??

Ni hivi wimbo wa mdogmdgo ulikua juu sana pamoja na vdeo kali..
Baada ya alikiba kuja na mwana bila video,mdogo mdogo ukafunikwa..

Lakin pia mwana haujakaa mda kwenye chati,hii n baada ya mkubwa na wanawe kutoa Niseme..

Mzki wa bongo kwa sasa umeshikwa na yamoto band,pamoja na mwana kwa mbali,kitorondo umepotea kabisaa..

Kinachomuweka juu diamond kwa sasa ni ujinga ujinga wake na wema sepetu..
 
hahahahahaa hadi nimecheka kwa sauti, kumbe ujinga unalipa??? kwa hiyo ujinga ujinga ndio unaomfanya dai apate show nyingi za nje, ujinga ujinga ndio unaomfanya dai awe nominated kwenye awards za mbele.
najua inakuwa sana ngumu kwenu kumeza, lkn ukweli ni kwamba kizuri chajiuza...........

hivi unajua hakuna wimbo uliokwishapigiwaga vuvuzela kama mwana, hakunaaaaa, nguvu zilizotumika kuutangaza mwana zilitosha kabisa kuuhamisha mlima kilimanjaro ukaja hapa dar.na kulidhibitisha hili ndani ya mwezi mmoja tu team kiba yote chali nguvu kwisha kabisa, kila anaejaribu kutamka mwana anahisi kichefuchefu.na ndio maana nimewaita hapa kuwakumbusha jamani kupenda gharama msichokeee.
 

Mdogomdogo si kwenye maharusi , si kwenye vipaimara yaani kila sehemu huo wimbo wa mwana sijawahi usikia hata zaidi ya mara 10 tokea utoke...publicity kubwa ila hamna kitu
 
Point taken binti kitorondo

Huwezi ukawa na Audio nzuri halafu video mbaya ukategemea kufika mbali kwenye soko la muziki..

Diamond ni mjanja kwa sababu anatoa nyimbo zinazouza kimataifa (za kuchezeka)na ndani.. My number one ndio nyimbo iliyouza na kutamba zaidi bongo kama mtu anabisha aulize ma dj wa vituo mbalimbali vya redio
 

Ila kweli mkuu ile video siyo ya kutoa kiba video haivutii kabisa sijui tatizo lipo wapi.
 

Ndio unalipa..

Ni kama ujambazi unavolipa lakin watu wenye akili hatuufanyi..
Ni kama umalaya unavolipa lakin wanawake wenye akili hawaufanyi..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…