Alikuwa wapi siku zote?

Alikuwa wapi siku zote?

Halafu tukisema wanawake hawana akili tutaonekana wakorofi
Ogopa viumbe wanaitwa Wanawake yaani kwa Roho mbaya aliamua kumnyima jamaa kitumbua siku kibao kwa kisingizio mpaka ndoa halafu kaamua kumpa fala mwingine tu kirahisi rahisi tu kabla ya ndoa sasa ulichokwepa kwa jamaa wa mwanzo ni nini?
Faken kweli imeniuma sana your selfish in high level make me to
Get The JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala Out of Here!
(GTFOH) nigga!

Shabhashhhh!
😬😬
 
Kumbe kutongozana kwenye Uzi wa watu kuna asilimia kubwa ya kula kimasihara eeh
 
Ama kweli ibilisi wa mtu ni mtu!

Huyu mwamba anataka kuniharibia ila amechelewa kipindi Niko field hospital x yeye alikuwa intern hospital hiyo hiyo, nilitokea kumpenda sana hii ni baada ya yeye kuonesha dalili za kunipenda., Kutokana na kuwa mpweke takribani miaka 24 ikabidi nijisogeze karibu naye Ili twende sambamba!

Naam,.tulifanikiwa! tukawa tupo close nikawa naenda kwake sometimes, na outing za hapa na pale.

Nilimuweka Wazi juu ya Hali yangu yakuwa mpweke takribani miaka 24 hivyo Nikamsihi kuwa natamani haya yawe ni mahusiano yangu ya Kwanza na ya mwisho, imeant nilitaka anioea kabla ya kula tunda kapasino.

Naam, alikubali na akaniahidi atafanya hivyo ndani ya mwaka huo
Licha ya kuwa close nae ila hakuwahi kunambia nimuonjeshe mapishi yangu jambo amabalo nililipenda saana kutoka kwake.

Wakati nakaribia UE ya mwisho alipata kazi Zanzibar hospital x hivyo akawa na mbali Mimi Hali iliyopelekea mahusiano yetu kufifia Kwan alikuwa anadai mara kwa mara niende Zanzibar kumtembealea NAMI nilikaza shingo kwani nilihofia chakula changu kinaweza kuliwa kabla ya wakati.
Alivokuwa anarudi Bara alikuwa hanambii isipokuwa nilikuwa napata habari zake kupitia kwa marafiki zake na status zake.

Baada ya siku kadhaa akanambia tuachane maana siko tayari kumpa ushirikiano, na akadai ana mchumba wake hivyo nisimtafute niliumia sana kiukweli., na kilichonifanya niumie zaidi ni kwamba nilikuwa nimeshamtambulisha Hadi nyumbani ,itoshe kusema alinitia aibu!

Toka juzi ananisumbua anataka turudiane baada ya kusikia naolewa, yote Tisa kumi, alivyo mshenzi kamtumia text My future hubby kuwa et hajamalizana na Mimi akaambatanisha na picha tukiwa wote kama udhibitisho, picha zenyewe nilikuwa 3rd year hukoo. Ila nashukuru mume wangu mtarajiwa hata hajastuka Kwan yeye ndo aliyepiga teke akavunja mlango baada ya kitasa kugoma kufunguka

UNIKOME, NAJUA UPO HUMU UNASOMA HUU UZI ,NARUDIA TENA, UNIKOME.

Mpaka ifike hiyo trh 13 ntaona mengi!
Zamani mwanaume alikuwa akienda ukweni kujitambulisha. Ila nowadays mwanaume anapelekwa kwa ndugu atambulishwe
 
Back
Top Bottom