Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,761
- 216,011
Walikutana Ben na Rose shuleni wakiwa wote wamefaulu darasa la saba. Licha ya uwanafunzi Ben alikua na kipaji cha kuimba na kupiga gitaa. Weekends alitumbuiza kwenye bar na pia alialikwa kwenye maharusi. Kwa kifupi wote Ben na Rose hawakutoka katika familia zenye uwezo.
Mama yake Rose alikua single parent mwenye watoto wawili. Mdogo wake Rose alikua ni w kiume. Ben na Rose walipoanza urafiki, Ben alielewa matatizo mengi aliyokumbana nayo Rose. Kuna siku alimpitia waende shuleni alikuta vyombo vya kina Rose vinatupwa nje kwa kuwa hawajalipa pango. Ben alitoa pesa ya pango kwa miezi mitatu.
Mdogo wake Rose alisoma private na mama alihangaika sana na ada. Ben alichukua jukumu zima la kumsomesha shemeji. Ben alipanga ghetto lake, ndani sigara kwa sana na jioni alitunga nyimbo na kufanya mazoezi na gitaa lake.
Mitihani ya kidato cha nne Ben alipata div four ya na gentlemen, Rose alipata div two ya nguvu. Hakukua na pesa za kumfanyia Rose shopping ya kuendea shule. Ben alipiga mzigo mpaka alipata pesa n a kila mwezi alimtumia laki moja ya matumizi shuleni.
Rose akiwa shuleni mama yake aliugua sana. Ben hakutaka kabisa kumsumbua Rose aliyekuwa katikati ya mitihani, Ben alilipia mahitaji ya mama Rose na alilipa huduma ya boda boda wa kupeleka chakula hospitali. Baada ya mitihani Rose alirudi nyumbani na kumkurta mama yake ametoka hospitali.
Rose alikwenda chuo kikuu na alipata mkopo 100%. Ben aliendelea kuitunza familia ya Rose. Alimwambia Rose tukija kuoana angalau mmoja wetu atakua na elimu. Rose alikua mrembo kama jina lake.
Baada ya kumaliza chuo, Rose aliitwa Dar kwenye interview baada ya kuisambaza CV yake mitandaoni. Alimpigia simu rafiki yake wa chuoni akamuomba akae nae kwa siku atakazokua Dar. Rose anafika Magufuli terminals rafiki amezima simu. Rose alipanick.
Khaleed alikua na issue zake za kibiashara pale stand, alimuona Rose analia, Khaleed alimsalimia na kutaka kujua kisa na mkasa. Khaleed ni mtoto mkubwa wa tajiri mmoja na ndiyo kwanza amerudi kutoka USA akikokua anasoma Masters. Yeye ndiye hare to the family business empire.
Khaleed alimuonea huruma sana Rose, alimchukulia hoteli na kumwambia apumzike. Kesho yake alimfuata asubuhi na kumpeleka kwenye interview. Rose hakubahatika katika interview ile. Khakeed aliomba amtembeze kidogo Dar kabla hajaelekea kwao Kolomije.
Baada ya siku tatu kuwa Dar, Khaleed alimuomba Rose waende Mombasa kwa siku tano. Waliishi siku tano Mombasa wakila bata. Rose alizima simu siku zote, kuanzia zile siku tatu za hotelini Dar, Khaleed alimpigia kwa simu ya hoteli.
Aliporudi Kolomije Ben alitaka kujua sababu ya simu kuwa off muda wote, wakiwa wanaongea Khaleed alipiga simu. Ben aliomba tu maelezo yaliyonyooka. Rose alifunguka yote, Ben alilia kama mtoto. Khaleed alifanikiwa kumuoa Rose baada ya kubadili dini.
Mama yake Rose alikua single parent mwenye watoto wawili. Mdogo wake Rose alikua ni w kiume. Ben na Rose walipoanza urafiki, Ben alielewa matatizo mengi aliyokumbana nayo Rose. Kuna siku alimpitia waende shuleni alikuta vyombo vya kina Rose vinatupwa nje kwa kuwa hawajalipa pango. Ben alitoa pesa ya pango kwa miezi mitatu.
Mdogo wake Rose alisoma private na mama alihangaika sana na ada. Ben alichukua jukumu zima la kumsomesha shemeji. Ben alipanga ghetto lake, ndani sigara kwa sana na jioni alitunga nyimbo na kufanya mazoezi na gitaa lake.
Mitihani ya kidato cha nne Ben alipata div four ya na gentlemen, Rose alipata div two ya nguvu. Hakukua na pesa za kumfanyia Rose shopping ya kuendea shule. Ben alipiga mzigo mpaka alipata pesa n a kila mwezi alimtumia laki moja ya matumizi shuleni.
Rose akiwa shuleni mama yake aliugua sana. Ben hakutaka kabisa kumsumbua Rose aliyekuwa katikati ya mitihani, Ben alilipia mahitaji ya mama Rose na alilipa huduma ya boda boda wa kupeleka chakula hospitali. Baada ya mitihani Rose alirudi nyumbani na kumkurta mama yake ametoka hospitali.
Rose alikwenda chuo kikuu na alipata mkopo 100%. Ben aliendelea kuitunza familia ya Rose. Alimwambia Rose tukija kuoana angalau mmoja wetu atakua na elimu. Rose alikua mrembo kama jina lake.
Baada ya kumaliza chuo, Rose aliitwa Dar kwenye interview baada ya kuisambaza CV yake mitandaoni. Alimpigia simu rafiki yake wa chuoni akamuomba akae nae kwa siku atakazokua Dar. Rose anafika Magufuli terminals rafiki amezima simu. Rose alipanick.
Khaleed alikua na issue zake za kibiashara pale stand, alimuona Rose analia, Khaleed alimsalimia na kutaka kujua kisa na mkasa. Khaleed ni mtoto mkubwa wa tajiri mmoja na ndiyo kwanza amerudi kutoka USA akikokua anasoma Masters. Yeye ndiye hare to the family business empire.
Khaleed alimuonea huruma sana Rose, alimchukulia hoteli na kumwambia apumzike. Kesho yake alimfuata asubuhi na kumpeleka kwenye interview. Rose hakubahatika katika interview ile. Khakeed aliomba amtembeze kidogo Dar kabla hajaelekea kwao Kolomije.
Baada ya siku tatu kuwa Dar, Khaleed alimuomba Rose waende Mombasa kwa siku tano. Waliishi siku tano Mombasa wakila bata. Rose alizima simu siku zote, kuanzia zile siku tatu za hotelini Dar, Khaleed alimpigia kwa simu ya hoteli.
Aliporudi Kolomije Ben alitaka kujua sababu ya simu kuwa off muda wote, wakiwa wanaongea Khaleed alipiga simu. Ben aliomba tu maelezo yaliyonyooka. Rose alifunguka yote, Ben alilia kama mtoto. Khaleed alifanikiwa kumuoa Rose baada ya kubadili dini.