Infiltrator
Senior Member
- May 13, 2017
- 126
- 227
🌍 Africa.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unasifia manati? Afrika bado sana!Novemba 24, 2021 Kijana wa miaka 13 raia wa Burkina Faso, Aliou Sawadogo akiwa na manati yake porini akiwinda ndege, aliona kitu kikiambaa angani.
Sawadogo akatoa jiwe kutoka katika kaptula yake kisha akaliweka katika kigozi cha manati na kuanza kutafuta shabaha.
Akavuta pumzi na kuzishusha kwa kuachia jiwe lililoenda kuidungua ndege nyuki (drone) iliyokuwa angani.
Ndege nyuki hiyo ilikuwa ikipiga picha za kijasusi ambazo serikali ya Ufaransa huzitumia kwa manufaa yake.
Baada ya kuidondosha "drone" hiyo akaiokota kurudi nayo mjini.
Wananchi wakamtunza tuzo ya ushujaa kwa kumuinua juu kisha kuzunguka naye mitaani huku wakiimba nyimbo za kumsifu mtoto huyo.
Ndimi Juma Wage
Dodoma.
View attachment 2753072View attachment 2753073
Ahahahahaha! Manati oyeee! African technology oyeee!!!Hahahah.
Nasifia uwezo wa Sawadogo kudondosha drone kwa manati.
Ni kipawa kilichoibuka kutoka mafichoni.
Yaani kwa kuwa kabahatisha kudungua drone ndio sifa ya kupelekwa jeshini..!!Huyo dogo alitakiwa awe viunga vya jeshi, kama bado mdogo, awe shule za jeshi
Si bora smebahatisha...ok, mbona wanazurura naye mtaani kama pongezi si bora wampe ajira?Yaani kwa kuwa kabahatisha kudungua drone ndio sifa ya kupelekwa jeshini..!!
FUNZO-Madrones hutunguliwa kwa urahisi na vitu visivyoeleweka kisayansi.
kuwa mpole...Hii makala iliibwa na kuondoshwa jina langu.
Plz tuache kutenda huo uovu.
Analipiginia Taifa lake! Awe amepewa au lah ila amelinda taifa lake.Tunajifunza kutokana na Makosa. Hayakusemwa ni Makosa ya nani, yaweza kuwa ya kwetu au ya wengine.
Muhimu ni kujifunza (funzo).
Kijana alistahili zaidi ya hicho, huenda walimpatia maana taarifa zaidi kumuhusu huyo dogo zimekuwa ngumu kupatikana.