Alivyoifanya Mobutu Congo DR ndio wanavyoifanya CCM Tanzania. Ni suala la muda tu Tanzania itakuwa kama Congo

Alivyoifanya Mobutu Congo DR ndio wanavyoifanya CCM Tanzania. Ni suala la muda tu Tanzania itakuwa kama Congo

Jobless unatokwa na mapovu, huu muda ungeutumia kutafuta kibarua upate hata hela ya kula... Uzembe wako na familia yako kushindwa kujiimarisha kiuchumi usitafute watu wa kuwalaumu...
Tangu uanze kubwabwaja umefaidika nini sasa? Eti una kazi nzuri ipi hiyo ya kuuza matrako labda
Mkuu imagine mtazamo wako ndo uwe unaaksi 80% ya mtazamo wa watz.
Hata ubinafsi wa wacongo utakuwa nafuu mara kumi elfu kuliko sisi.

Pia uzi kama huu matusi ya nguoni kulikon?.kuisema ccm na viongoz walio madarakani kwa nia ya kujenga taifa msichukulie kuwa ni kukosa kaz au chuki binafsi. Ujue hata mchezaj mwenye mpira ndiye anasemwa au kutazamwa,akimpasia mwingine naye huyo atasemwa pia.
 
Ndiyo maana nakuita Tahira. Msuya alianza kazi lini? Alikua waziri wa biashara na viwanda na baadaye akawa Waziri Mkuu mara mbili wakati wa Nyerere na Mwinyi.

Uchumi wa Tanzania uliporomoka kikubwa zaidi baada ya Vita ya Uganda- 1978/ baada ya hapo ndiyo kukawa Hakuna pesa na baadaye shillingi kuporomoka.

Sasa Mwinyi alifanya nini? Mwaka 1992 nchi ilifirisika. Aliyeanza kuinua nchi alikua Mkapa.

Wewe unamsikiliza Zitto? Soma vitabu
Utabisha ila ukweli ni kuwa mpenda demokrasia aling'atuka akaacha nchi ikiwa hoi kiuchumi ' mkondo wa uchumi ulikuwa umechafuka kwa zaidi ya miaka kumi huku mashirika ya Umma yakijiendesha kwa hasara'. Hizi ni nukuu za Prof. Mukandala akimuelezea Rais Ali Mwinyi katika uzinduzi wa Kitabu chake cha Mzee Rukhsa, soma uk. 205 wa kitabu chake.

Screenshot_20250219-095154.jpg
Screenshot_20250219-095154.jpg


Cleopa David Msuya akiwa Waziri wa Uchumi, Fedha na Mipango ndio aliyeokoa uchumi wa Tanzania enzi za Mwinyi kwa kufuta ushauri na andiko lake kwa mjibu wa Rais Ali Mwinyi mwenyewe.
Screenshot_20250219-095348.jpg
 

Attachments

Kwa tukio la kutekwa Mtanzania mwenzetu
Tanzania ishakuwa kama kongo mbona .......
Namba moja watu wameaminishwa burudani
Uchawa nk
Dar naiona kama Kinshasa vile

Ova
Nakubaliana na wewe ndugu.

Nimeangalia ile clip inayoonesha tukio la mtu kutekwa mchana kweupe huko Pwani alafu watu wanachukuq video wanashindwa hata kumsadia.

Nimeumia sana maana inathibitisha haya ndo madhara ya kutengenezewa kizazi cha vijana wanaowaza uchawa, kujipendekeza na starehe. Kizazi kisicho na maarifa na kisichoelewa maana ya Haki.
 
basi itoshe kusema kwamba awamu ya 4 iliharibu hii nchi, itachukuwa generation kuirudisha hii kwenye mstari, ni kama laana iliyo kwenye ukoo inaharibu vizazi hadi vizazi, tuiombee nchi yetu …
 
Kwa tukio la kutekwa Mtanzania mwenzetu

Nakubaliana na wewe ndugu.

Nimeangalia ile clip inayoonesha tukio la mtu kutekwa mchana kweupe huko Pwani alafu watu wanachukuq video wanashindwa hata kumsadia.

Nimeumia sana maana inathibitisha haya ndo madhara ya kutengenezewa kizazi cha vijana wanaowaza uchawa, kujipendekeza na starehe. Kizazi kisicho na maarifa na kisichoelewa maana ya Haki.
basi itoshe kusema kwamba awamu ya 4 iliharibu hii nchi, itachukuwa generation kuirudisha hii kwenye mstari, ni kama laana iliyo kwenye ukoo inaharibu vizazi hadi vizazi, tuiombee nchi yetu …
Ni hatari sana.

Masuala haya ya kutekana hapa Tanzania jinsi yanavyofanyika ni kama vile ilivyokuwa nchini Zaire (DRC) enzi za Utawala wa Dikteta Mobutu Sese Seko, Watu walikuwa wanatekwa mchana kweupe kama hivi wanavyofanya hawa Watekaji kwenye video hii. Nchini Zaire ilikuwa ukitekwa namna hiyo basi utapelekwa moja kwa moja nyumbani kwake Rais Mobutu Sese Seko kwenye makazi yake yaliyopo katika Kijiji Cha Gbadolite ili ukateswe na kisha kuuawa. Hali ilikuwa mbaya sana kupita kiasi nchini Zaire, naona hali kama hiyo hiyo sasa hivi ipo nchini Tanzania. Ni hatari kubwa sana kwa Usalama wa Umma na nchi yote kabisa kwa ujumla wake.
Matukio ya namna hii yana madhara mabaya sana ambayo kamwe hayataweza kuja kurekebishika.

Nashangaa Sana kuona kwamba Serikali iliyopo ipo kimyaaa kabisa licha ya kwamba vilio vya Wananchi ni vikubwa sana katika kulaani matukio ya namna hii. Kulikoni hasa huko Serikalini?
 
basi itoshe kusema kwamba awamu ya 4 iliharibu hii nchi, itachukuwa generation kuirudisha hii kwenye mstari, ni kama laana iliyo kwenye ukoo inaharibu vizazi hadi vizazi, tuiombee nchi yetu …
Kwwki kabisa. Shida za msingi zilianzia hapa
 
Ni hatari sana.

Masuala haya ya kutekana hapa Tanzania jinsi yanavyofanyika ni kama vile ilivyokuwa nchini Zaire (DRC) enzi za Utawala wa Dikteta Mobutu Sese Seko, Watu walikuwa wanatekwa mchana kweupe kama hivi wanavyofanya hawa Watekaji kwenye video hii. Nchini Zaire ilikuwa ukitekwa namna hiyo basi utapelekwa moja kwa moja nyumbani kwake Rais Mobutu Sese Seko kwenye makazi yake yaliyopo katika Kijiji Cha Gbadolite ili ukateswe na kisha kuuawa. Hali ilikuwa mbaya sana kupita kiasi nchini Zaire, naona hali kama hiyo hiyo sasa hivi ipo nchini Tanzania. Ni hatari kubwa sana kwa Usalama wa Umma na nchi yote kabisa kwa ujumla wake.
Matukio ya namna hii yana madhara mabaya sana ambayo kamwe hayataweza kuja kurekebishika.

Nashangaa Sana kuona kwamba Serikali iliyopo ipo kimyaaa kabisa licha ya kwamba vilio vya Wananchi ni vikubwa sana katika kulaani matukio ya namna hii. Kulikoni hasa huko Serikalini?
Sahihi kabisa
 
Ni hatari sana.

Masuala haya ya kutekana hapa Tanzania jinsi yanavyofanyika ni kama vile ilivyokuwa nchini Zaire (DRC) enzi za Utawala wa Dikteta Mobutu Sese Seko, Watu walikuwa wanatekwa mchana kweupe kama hivi wanavyofanya hawa Watekaji kwenye video hii. Nchini Zaire ilikuwa ukitekwa namna hiyo basi utapelekwa moja kwa moja nyumbani kwake Rais Mobutu Sese Seko kwenye makazi yake yaliyopo katika Kijiji Cha Gbadolite ili ukateswe na kisha kuuawa. Hali ilikuwa mbaya sana kupita kiasi nchini Zaire, naona hali kama hiyo hiyo sasa hivi ipo nchini Tanzania. Ni hatari kubwa sana kwa Usalama wa Umma na nchi yote kabisa kwa ujumla wake.
Matukio ya namna hii yana madhara mabaya sana ambayo kamwe hayataweza kuja kurekebishika.

Nashangaa Sana kuona kwamba Serikali iliyopo ipo kimyaaa kabisa licha ya kwamba vilio vya Wananchi ni vikubwa sana katika kulaani matukio ya namna hii. Kulikoni hasa huko Serikalini?
Itafika wakati na wao watakuwa wanatekwa piga nkupige kama Mexico

Ova
 
Hongera sana mleta mada. Uliyoyasema ni ukweli mtupu.

Leo hii karibia kila nafasi muhimu ya uongozi ambayo ingetoa mwanga kuelekea kwenye maendeleo, wapo machawa wapuuzi kabisa wenye upeo duni, wasiojua chochote zaidi kumtajataja Samia na kumwabudu.

Mchango wa CCM kuiangamiza Tanzania, kuua ubunifu na maendeleo ya nchi, hautaweza kusahaulika kamwe.

Tazama ndani ya Serikali kuu, nani unaweza kusema ni super intelligent, siyo mnafiki, mbunifu, mwadilifu na ambaye anaonesha uongozi wenye matumaini? Hakuna, hakuna kabisa. Hakuna hata mmoja!!

Hawa machawa wa Rais wanaipeleka Tanzania kuwa koloni la waarabu ambao wanapewa kila rasilimali muhimu ya nchi ili washikilie uchumi, na watanzania wabakie kuwategemea hao waarabu kwa kila kitu. Usipomiliki uchumi, ujue umekuwa mateka na mtumwa ndani ya nchi yako.

Hongera sana kwa andiko hilo muhimu, mleta mada. Na wale ambao tayari akili yao imekwishapofushwa, machawa punguani, watakukejeli, lakini ukweli wa andiko hili utasimama daima. Na tufahamu kuwa hakuna chawa mwenye akili timamu na mkweli wa nafsi. Ili uwe chawa, lazima kichwani kuwe kumeyumba, na uamini kuwa bila kujibanza kwa mtu fulani, huna uwezo wa kuishi kwa kutegemea uwezo na maarifa yako. Na hawa machawa ndiyo sasa waliojazana Serikalini, halafu kuna watu bado wanatarajia kuwa haya machawa yataliongoza Taifa kuelekea kwenye maendeleo ya kweli.
 
Hongera sana mleta mada. Uliyoyasema ni ukweli mtupu.

Leo hii karibia kila nafasi muhimu ya uongozi ambayo ingetoa mwanga kuelekea kwenye maendeleo, wapo machawa wapuuzi kabisa wenye upeo duni, wasiojua chochote zaidi kumtajataja Samia na kumwabudu.

Mchango wa CCM kuiangamiza Tanzania, kuua ubunifu na maendeleo ya nchi, hautaweza kusahaulika kamwe.

Tazama ndani ya Serikali kuu, nani unaweza kusema ni super intelligent, siyo mnafiki, mbunifu, mwadilifu na ambaye anaonesha uongozi wenye matumaini? Hakuna, hakuna kabisa. Hakuna hata mmoja!!

Hawa machawa wa Rais wanaipeleka Tanzania kuwa koloni la waarabu ambao wanapewa kila rasilimali muhimu ya nchi ili washikilie uchumi, na watanzania wabakie kuwategemea hao waarabu kwa kila kitu. Usipomiliki uchumi, ujue umekuwa mateka na mtumwa ndani ya nchi yako.

Hongera sana kwa andiko hilo muhimu, mleta mada. Na wale ambao tayari akili yao imekwishapofushwa, machawa punguani, watakukejeli, lakini ukweli wa andiko hili utasimama daima. Na tufahamu kuwa hakuna chawa mwenye akili timamu na mkweli wa nafsi. Ili uwe chawa, lazima kichwani kuwe kumeyumba, na uamini kuwa bila kujibanza kwa mtu fulani, huna uwezo wa kuishi kwa kutegemea uwezo na maarifa yako. Na hawa machawa ndiyo sasa waliojazana Serikalini, halafu kuna watu bado wanatarajia kuwa haya machawa yataliongoza Taifa kuelekea kwenye maendeleo ya kweli.
Asante mkuu! In short CCM wametuulia Taifa. Tusubiri maziko yetu.

Hali ni mbaya sana maana naskia hadi wenye akili na mawazo mazuri na huru huko Serikalini wanatengwa na kunyimwa nafasi kwa kigezo eti hawana nidhamu.

Kwa ninavyoona the only way out ili tuweze kurekebisha palipoharibiwa sana ni CCM kuondoka madarakani either kwa njia halali au haramu. Na walivyo na kiburi na kutengeneza wajinga wengi hadi kwenye vyombo vya ulinzi na usalama. Njia pekee ninayodhani itawayoa ni coup.
 
Hongera sana mleta mada. Uliyoyasema ni ukweli mtupu.

Leo hii karibia kila nafasi muhimu ya uongozi ambayo ingetoa mwanga kuelekea kwenye maendeleo, wapo machawa wapuuzi kabisa wenye upeo duni, wasiojua chochote zaidi kumtajataja Samia na kumwabudu.

Mchango wa CCM kuiangamiza Tanzania, kuua ubunifu na maendeleo ya nchi, hautaweza kusahaulika kamwe.

Tazama ndani ya Serikali kuu, nani unaweza kusema ni super intelligent, siyo mnafiki, mbunifu, mwadilifu na ambaye anaonesha uongozi wenye matumaini? Hakuna, hakuna kabisa. Hakuna hata mmoja!!

Hawa machawa wa Rais wanaipeleka Tanzania kuwa koloni la waarabu ambao wanapewa kila rasilimali muhimu ya nchi ili washikilie uchumi, na watanzania wabakie kuwategemea hao waarabu kwa kila kitu. Usipomiliki uchumi, ujue umekuwa mateka na mtumwa ndani ya nchi yako.

Hongera sana kwa andiko hilo muhimu, mleta mada. Na wale ambao tayari akili yao imekwishapofushwa, machawa punguani, watakukejeli, lakini ukweli wa andiko hili utasimama daima. Na tufahamu kuwa hakuna chawa mwenye akili timamu na mkweli wa nafsi. Ili uwe chawa, lazima kichwani kuwe kumeyumba, na uamini kuwa bila kujibanza kwa mtu fulani, huna uwezo wa kuishi kwa kutegemea uwezo na maarifa yako. Na hawa machawa ndiyo sasa waliojazana Serikalini, halafu kuna watu bado wanatarajia kuwa haya machawa yataliongoza Taifa kuelekea kwenye maendeleo ya kweli.
Naona una hasira kali kweli!
 
Mobutu ni kama Amin wanasingiziwa mambo mengi sana ila walikuwa mtu wema. Mobutu katawala miaka 32 wakati mpenda demokrasia wetu katawala miaka 22 wote kwa pamoja wameacha uchumi wa nchi zao ukiwa goigoi na dhaifu kuliko awali. Tuepuke propaganda za kumsingizia Mobutu.
Hapa umetetea nini kilogic?
 
Mwaka 2020 niliandika uzi humu jamvini kuhusu tofauti ndogo iliyokuwepo baina ya Congo ya Mobutu na Tanzania!

Niliandika uzi ule kwa sababu kuna vitu vingi sana vilivyokuwa vinatokea wakati ule havikuwa na tofauti na mambo yaliyokuwa yanatokea nchini Congo kipindi cha Mobutu. Niliweka na Documentary waliyoiandaa wazungu inayoonesha namna Congo ya Mobutu ilivyokuwa (Nashauri wanabodi muiangalie hadi mwisho bila kuchoka na mtajifunza kitu hakika).


Labda watu hawafahamu.

Congo tunayoiona leo ya vijana kuwasifia watu wenye hela na kuwaabudu badala ya kujikita kwenye kupata maarifa ya kuisaidia nchi yao kwenda mbele iliasisiwa na aliyekuwa Rais wa Nchi hiyo Mobutu Seseko Kuku wa Zebanga.

Baada ya kushika madaraka, Mobutu alitengeneza Congo ya machawa. Ilikuwa huwezi kupata cheo au nafasi Serikalini bila kuonesha unyenyekevu wako na kujipendekeza kwako kwake.

Chama chake alikiita chama dola na kuwatengeneza wa Congo kukisifu chama chake na yeye binafsi. Zilitungwa nyimbo za kumsifu, zilitengenezwa nguo zenye picha zake pamoja na kofia ambazo vijana, wamama na watu wa Congo walitengenezewa utaratibu wa kuzivaa ili kumsifu na kuonesha kuwa maendeleo ya Congo ni yeye na hakuna Congo bila yeye.

Badala ya wananchi wa Congo kutengenezwa kufikiri vizuri kwa fikra huru kwa ajili ya maendeleo yao kwa miaka mingi ijayo, walitengenezwa kuwaza maendeleo ni mtu na bila kumsifu huyo mtu mkono hauwezi kwenda kinywani.


Matokeo ya hayo ni kwamba badala ya kutengeneza vijana na watu wenye akili kwa faida ya nchi yao, walitengeneza mapooza kichwani ambao ndo walipewa madaraka na Mobutu, hivyo nchi ya Congo alishindwa kustawi na kuhimili maadui wa ndani na nje maana walioshika uongozi hawakushika kwa merit ila kwa kujipendekeza kwao kwa Mobutu na chama chake.

Hali hii ndo yanayotokea sasa nchini Tanzania, kwetu Mobutu wetu ni CCM.

Kuanzia mwaka 2012, CCM walianza kutengeneza mfumo wa siasa zilizoshika hatamu leo hii. Walitengeneza mfumo wa vijana wanaoonesha kuwapigania, kuwatetea na kuwasemea vizuri viongozi wao kupewa madaraka makubwa ya uongozi kwenye utumishi wa Umma. Hii ilianza kwa Nape baada ya kumtukana Lowasa na kuonesha kuwa chawa wa JK alikabidhiwa Ukuu wa Wilaya na baadae cheo ndani ya CCM.

Ilifuata kwa Makonda ambaye nae baada ya kuonesha kuwa chawa wa JK kwa kumsema vibaya Lowassa akazawadiwa ukuu wa wilaya.

Kubwa zaidi ni Magufuli ambaye kwenye kila hotuba za kuzindua miradi ya ujenzi alikuwa anamsifia JK mwishowe JK akaona ndo awe Rais wa Tz.

Kipindi cha JK, vijana waliokuwa vyuoni waliotengenezwa na siasa za namna hiyo walianza kuzawadiwa nafasi ya uongozi na utumishi Serikalini kama DAS, DED, DC na nyinginezo.

Alipokuja Magufuli ndo alilifanya suala hili zaidi ya alivyofanya Kikwete. Magufuli alikuwa akikuona leo umemuongelea vizuri kwenye chombo cha habari kesho yake unasikia Msigwa kakutangaza wewe kuwa DC/DED/DAS/RAS/KM au Mwenyekiti wa Bodi au Mjumbe wa Bodi. Watu waliacha kupewa vyeo kwa uwezo wao ila kutokana na uchawa wao kwa Rais na chama chake.

Matokeo yake hali hii imeendelea na kukua hadi kwenye maisha ya kawaida. Mitaani machawa ndo wanqpewa fursa, kwa wasanii wanaotunga nyimbo za kuwasifia viongozi ndo wanapewa tenda za kufanya kazi na Taasisi za Umma ili wapige hela.

Sasa hali hii imefika climax. Siku hizi fedha za umma (kodi za wananchi) zinazotengwa kwenye bajeti ya Serikali kutekeleza miradi mbalimbali zinahusishwa na mtu kusifiwa binafsi kuwa anafanya yeye. Utasikia Magufuli kafanya haya, hakuna kama Magufuli, mara Samia kafanya haya, hakuna kama Samia.

Sasaivi huko CCM kama huvai kofia yenye nembo ya SSH au Samia au nguo yenye picha ya Samia unaonekana kama sio mwenzao.

Kwa wasio na akili wanaweza kuona jambo hili ni la kawaida sana ila kwa wenye akili napenda kuwaambia hizi ni dalili rasmi kuwa Tanzaniartunaenda kuwa kama Congo.

Suala hili linaenda kudumaza sana akili za Watanzania, suala hili linaenda kututengenezea jamii iliyopo Congo leo nchini Tanzania ambayo inaamini kwenye kujipendekeza, kutukuza wenye hela hali iliyofanya Taifa lile leo kufa na kuwa shamba la bibi kwa watu wenye akili (Mataifa mbalimbali ambayo yanaliibia ikiwemo Rwanda na Uganda)

Leo hii Tanzania, Vijana ambao wanashika nafasi zinazopaswa kushikwa na watu smart na intelligent ni vijana ambao wanaamini bila kujipendekeza kwao kwa CCM na Viongozi wao wakuu wasingefika hapo. Vijana hawa hawataweza kuifanya nchi yetu kuhimili hila za maadui wa ndani na nje ambao nchi zao zinawatengeneza kwa kuwapa exposure na kuwatengeneza kuwa smart isivyo kawaida.

Vijana hawa hawataweza kutengeneza Tanzania Dream ambayo inapaswa kutengenezwa na watu wanaoshika nafasi za maamuzi kwa merit na sio uchawa. Watu wanaofanya research na kuandika mambo makubwa na kuyasimamia yawe kweli.

Naionea huruma Tanzania. Kama Vyombo vya dola havitaisaidia kuiondoa CCM madarakani. Sisi ni Congo tunaofuata.
Samia anafanya kazi sana na inaonekana kila mahali. Uchawa wa kulaumiwa ni Mwalimu Nyerere aliyekubaliana na ule muitikio wa 'zidumu fikra sahihi za mwenyekitiiiii' na hadhira ikaitikia 'zidumuuu' ule ulikuwa mwanzo kabisa wa uchawa.

Marais waliofuatia walijikuta wakifuata tabia za kiutawala walizozirithi kwa watangulizi wao wakidhani wanapita katika njia za kawaida za kichama kumbe wanaleta hulka mbaya ya uchawa.
 
Wakongo uchawa walisababishiwa na Wabelgiji waliowatawala, Mobutu aliurithi huo ujinga kutoka kwa mkoloni.

Mzungu alihakikisha anajenga shule nzuri za muziki na vijana wengi wanaoufahamu ili awapumbaze apate kuwaibia vizuri madini yao.

Alipoibuka Lumumba na sera zenye nia ya kumtetea mwananchi wa kawaida akauwawa haraka sana.

Uchawa wa Tanzania ulianzishwa na Mwalimu Nyerere, alipenda kuzungukwa na wapambe wenye umri mdogo akiwa na lengo la kuwalea kisiasa ili waje kurithi nafasi za viongozi wa kwanza wa Tanzania, lengo lake lilikuwa zuri lakini katika michakato ya kichama likazaa hulka ya uchawa.

Walimpamba sana ili malengo yao ya kibinafsi yaweze kufanikiwa, aliwahi kusema wapambe walimwambia Mwalimu usistaafu kwanza wananchi bado wanakupenda na akaendelea kwa miaka mitano mingine lakini baadae machale yakamcheza akagundua kwamba waliomwambia asistaafu kwanza walitaka kutimiza malengo yao binafsi.

Chawa akipewa uhuru wa kuwepo anatimiza lengo lake binafsi la kimaisha , ni watu wanaofukuza na muda wanaopewa baada ya kuufanya upambe wao kwa kiongozi anayekuwepo madarakani.
 
Un
Kuna hoja gani ya kutoa hapa? Yaani Tanzania inafananishwa na Zaire ya Mobutu halafu mimi Mtanzania wa kweli nikae kimya? Eti nitoe hoja!? Upumbavu haujadiliwi!!!!
Ungeacha wajadili watu wenye akili timamu. Wewe ni hao walioharibiwa akili kiasi cha kupofuka kabisa.

Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kuipuuza hii hoja muhimu sana inayoangalia mstakabali wa Taifa.
 
Ha
Mwashambwa..Tlaatlah...Mwijaku, Babalevo...vijana wenye mchango mdogo mnoo kwa taifa
Hao hawana mchango hata kidogo. Hao ni hasara kwa Taifa na familia zao.

Kuwa chawa ni kukubali kuwa punguani mnafika. Mtu aliyeamua kuwa punguani na mnafiki, anakuwa na faida gani??
 
Back
Top Bottom