Alivyokamtwa Lema kwenye ndege ni sawa tu alivyochukuliwa mzee Ali Kibao kwenye basi

Alivyokamtwa Lema kwenye ndege ni sawa tu alivyochukuliwa mzee Ali Kibao kwenye basi

Ninakubaliana na wewe.
Swali ambalo ninge shukuru kupata jibu lake ni hiyo "nguvu ya wananchi" inavyo patikana

Kwa nini hawa CHADEMA hawana nguvu ya wananchi; kama ni kweli hawana.
Wamepuuzwa kw sababu ni vibaraka wa Mabeberu
 
Wasingesambaza police wenye silaha kali na vitisho kila mahali , hapo ndio ungekua na nguvu yakusema chadema hawakuungwa mkono na wananchi kwa sababu ulizotaja.
Ili kitokee nini? Nchi zingine mbona Polisi wanasambazwa lakini watu wanaandamana? 😆😆😆😆

Unampambania Mtanzania au siyo? 🤪🤪🤪

Mtanzania hana njaa kwamba anahitaji kupambaniwa
 
Mkuu 'Umkhonto', naamini wewe unaamini hivyo ulivyo elezea. Mimi siamini hivyo hata mara moja.
Kwanza hiyo dhana ya 'Tanzania ni nchi ya amani" maana yake ni nini hasa? Amani ni kutekwa watu, kupotezwa na kuuawa? Hii ni amani ya namna gani?
"WaTanzania hawajazoea vurugu"? Kuna binaadam anaye zoea na kukubali kuvurugwa?

Angalia upotofu mkubwa unao uonyesha: eti "usitegemee kupata nguvu yoyote ya umma kuwaunga (CHADEMA) mkono"? Wewe huu uhakika umeupata wapi. Kwa vile leo gharama kubwa imetumika kuzuia maandamano ndiyo kiwe kigezo cha kujivuna hivi? Hivi huelewi ni kiasi gani viongozi wako huko CCM walivyo na hofu kuu sana ya haya yanayo endelea nchini, au ni kujipa tu moyo unapo ingia humu JF.
Wewe unadhani umma wa waTanzania umetulizana kama ulivyo kuwa umetulizana miaka yote? Huoni kabisa tofauti yoyote inayojiongeza kila siku mnavyo vuruga utulivu huo?

Ni hivi: Hakuna binaadam yeyote anayeweza kuwa mtulivu huku akiona maovu yanayo fanyika kila siku ndani ya nchi yake.

Hao Kenya unao watolea mfano, inaeleweka, hawajawahi kuwa na utulivu ndani ya nchi hiyo, kwa sababu ya ukabila na mauchafu mengine. Sasa mambo hayo hayo ndiyo CCM inayo yapalilia hapa kwetu, na bado watu kama wewe mnaamini waTanzania ni watulivu tu, hawajawahi kupigana popote!

'Umkhonto', wewe hukuchukulia tofauti kidogo na washabiki wenzio wa huko CCM mliomo humu JF, kwa sababu pamoja na ushabiki huo, lakini nadhani bado akili za kuchambua hali halisi ya nchi yetu bado unazo. Lakini kama huoni tunako elekea kama unavyoonyesha hapa, naona mambo yamezidi kuharibika zaidi huko ndani ya hicho chama.

Hii mitutu ya bunduki uliyo iona; halafu bado ukadhani Tanzania ni tulivu? Utakuwa unajidanganya mwenyewe.
Bila hata kuingia uwanjani, Chadema 2, dola 0. Ni wachache sana humu ndani ya hii JF ya sasa wana uwezo na akili ya kuweza kuelewa hilo.

Mambo mawili kwa, mawazo yangu, hivi sasa yamejionesha wazi. Waliomteka Ali Kibao (RIP) ndio hao hao waliomteka Godbless Lema (QED)

Kama ningeweza kutoa ushauri tu wa bure kama Mtanzania mzalendo. Dola mmevuliwa nguo, kama bado mna heshima na hekima chutameni!
 
Sisi raia wema tuliokua kwenye ndege tunaona ni sawa kwa muhalifu anaechochea machafuko kukamatwa , biashara zimeanza kwenda vizuri wao wanataka kuturudisha nyuma
 
Nitakupa sababu moja simpo kabisa. Tanzania ni nchi ya amani, na wananchi wake (hiyo nguvu ya wananchi) hawajazoea vurugu. Kwa hiyo mnapotangaza maandamano yenye viashiria vya uvunjifu wa amani na kuleta vurugu (eti kwa kuwa kenya wanafanya hivyo), usitegemee kupata nguvu yoyote ya umma kuwaunga mkono.
Na sababu ya hili ni ya kihistoria. Sisi tulipata uhuru wetu kwa kujieleza na kujenga hoja, kenya walipata uhuru wao kwa kupigana na kumwaga damu. Hiyo ni tofauti kubwa sana.
Kwa upande wangu niko tofauti kidogo na wewe hawa chadema wamekata tamaa hawana lengo la kushika dola wana lengo la kutafuta mkate wa kila siku tofauti na mwanzo hivyo wananchi wamechoka kusikia ngonjela ambazo hazina matokeo chanya nijuavyo mimi ccm haina uwezo wa kuongoza nchi ni vile tu hakuna mbadala wake na chadema yenyewe inajitafuta kwa kifupi hakuna chama chochote cha siasa kitawafaa wananchi sio ccm wala chadema
 
ccm haitaki upinzani. wapinzani hawaelewi tu? akina mbowe na lisu waachane na mambo ya kutetea watanzania. watanzania hawastahili kusaidiwa wanatakiwa wateseke mpaka ccm watakapochoka wenyewe kuwatesa. kila mtu aishi maisha yake. wa kufa afe wa kupona apone. nchi ilishazindikwa kichawichawi toka awamu ya kwanza. uchawi na maendeleo wapi na wapi.
 
Wasingesambaza police wenye silaha kali na vitisho kila mahali , hapo ndio ungekua na nguvu yakusema chadema hawakuungwa mkono na wananchi kwa sababu ulizotaja.
Acha visingizio wewe Kenya walisambaza polisi na jeshi na silaha nzito hadi magari ya jeshi mbona wananchi waliendelea na maandamano bila woga
 
Back
Top Bottom