Aliyegonga Tembo wa thamani ya Tsh milioni 30 Serengeti anatafutwa

Aliyegonga Tembo wa thamani ya Tsh milioni 30 Serengeti anatafutwa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Tembo mwenye thamani ya shilingi milioni 30 katika hifadhi ya taifa ya Serengeti amekufa baada ya kugongwa na gari namba T 388 DUF Toyota Kluger wakati akikatiza kwenda kunywa maji Ziwa Victoria kwenye barabara ya Mwanza kuelekea Musoma wilayani Bunda mkoani Mara.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mara Daniel Shillah amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa dereva na mmiliki wa gari hajafahamika na wanaendelea na uchunguzi ikiwamo kumsaka aliyehusika na ajali hiyo.

Aidha, Mkuu wa hifadhi ya taifa Serengeti, Bw. Masana Mwishawa, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akiwataka madereva wa vyombo vya moto kujali na kuzingatia usalama wa wanyamapori kwenye maeneo ya hifadhi.

1615625354465.png

1615625406599.png


ITV
 
Bongo nyoso sana. Mafinger print yote mliotuandikisha, mavitambulisho lukuki, Tin Number tra zipo, usajili wa gari hauwezi kukurudia kumpelekea ujue mmiliki wa gari kisha uanzie hapo uchunguzi?

After all mbona hampo concerned kuhusu hali ya huyo dereva/mmiliki kwa hio condition ya gari iliopo? Kama yu mahtuti ama kafariki mtafanyaje?
 
bongo nyoso sana.. mafinger print yote mliotuandikisha, mavitambulisho lukuki, Tin Number tra zipo, usajili wa gari hauwezi kukurudia kumpelekea ujue mmiliki wa gari kisha uanzie hapo uchunguzi?
after mbona hampo concerned kuhusu hali ya huyo dereva/mmiliki kwa hio condition ya gari iliopo? kama yu mahtuti ama kafariki mtafanyaje?
Kama kafa atakuwa kapata bahati, Bima watalipa

Kama kaumia atapata tabu sana lazima alipe.

Katika udereva wako lazima ujue vitu vinne ambavyo havijawahi kugonga mtu/gari nyingine

1. Msafara wa kiongozi
2. Ambulance
3. Wanyama wakiwa mbugani
4. Treni

Hao wote ni wewe unawagonga, sio wao wanakugonga

Kwa pale mbugani lazima alipe na gharama ya kusafisha, kwa hiyo inaweza kutoka hata milioni 40
 
Babu Tembo akiwapa taarifa wajukuu.

Babu: Ebwana mama yenu kagongwa na gari, leo hapa tutakua na msiba kwa dakika mbili kisha kila mmoja atajua anaenda kula wapi.

Wajukuu: Kilio cha pamoja.

Babu: Mimi hua nawaangalia tu mnalelewa kimayai sana. Sasa eti huyo mama yenu kagongwa na gari kafa, kagari kenyewe kadoooogo unajua bibi yenu aliangukiwa na kimondo? Na alipona. Nyinyi tembo wa siku hizi walaini walaini sana.

Mjukuu1: Babu usiseme hivi

Babu: KELELE. Tembo wa siku hizi tembo? Tembo walikua enzi zetu enzi hizo ukiliona jike lenyewe linakuletea mambo siyo siku hizi eti mnapiga magoti kuchumbia shwain.

Na nimekasirika na msiba msifanyie kwangu tokeni hapa.
 
Back
Top Bottom