Pre GE2025 Aliyekosoa uteuzi wa Samia kuwa mgombea Urais ahofia maisha yake

Pre GE2025 Aliyekosoa uteuzi wa Samia kuwa mgombea Urais ahofia maisha yake

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Siku chache baada ya kufutwa uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana sababu ya kupinga uteuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea pekee wa CCM, Mchungaji Dkt.Godfrey Malisa amedai kuanza kuingiwa na wasiwasi kuhusu maisha yake na kuwa yupo katika hatari baada ya kusema ukweli.

Akizungumza na Jambo Tv kuhusu kinachoendelea, Malisa amesema “na niwaambie watanzania wajue tu kwamba nipo kwenye wakati mgumu sana kwa sababu tu nimesimama kusema kweli, tumefika mahali hata watu wanatoa ushauri kwamba afadhali uondoke hata nchini”

Soma pia: Aliyepinga Rais Samia kupitishwa Mgombea pekee wa Urais kupitia CCM afukuzwa uanachama

Aidha Dkt. Malisa ameongeza kuwa ameshangazwa sana na hali hiyo ya kufikia kutishiwa hali ya kuwa tu ni kasema ukweli “Tunafika mahali tunasema hivi nchi yetu tupo hapo mahali pa kutishiwa kwa sababu tu unasema kweli. Nakumbuka mwanzoni kuna watu walikuja wakaniambia bana jihadhari” amesema Dkt. Malisa

Aidha amewaomba watanzania kumuombea kwa Mungu kwani anaamini ulinzi wa Mungu utamuwezesha kuivuka hali anayopitia

 
Siku chache baada ya kufutwa uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana sababu ya kupinga uteuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea pekee wa CCM, Mchungaji Dkt.Godfrey Malisa amedai kuanza kuingiwa na wasiwasi kuhusu maisha yake na kuwa yupo katika hatari baada ya kusema ukweli.

Akizungumza na Jambo Tv kuhusu kinachoendelea, Malisa amesema “na niwaambie watanzania wajue tu kwamba nipo kwenye wakati mgumu sana kwa sababu tu nimesimama kusema kweli, tumefika mahali hata watu wanatoa ushauri kwamba afadhali uondoke hata nchini”

Aidha Dkt. Malisa ameongeza kuwa ameshangazwa sana na hali hiyo ya kufikia kutishiwa hali ya kuwa tu ni kasema ukweli “Tunafika mahali tunasema hivi nchi yetu tupo hapo mahali pa kutishiwa kwa sababu tu unasema kweli. Nakumbuka mwanzoni kuna watu walikuja wakaniambia bana jihadhari” amesema Dkt. Malisa

Aidha amewaomba watanzania kumuombea kwa Mungu kwani anaamini ulinzi wa Mungu utamuwezesha kuivuka hali anayopitia

View attachment 3240687
Bado hajasema atajua hajui
 
Hili niwaambie ukweli, kukosoa jambo la mtu ni kukosoa watu wote wenye imani nao, nakukuweka ww kwenye hali mbaya. Katika eneo lolote la maisha.
Watanzania tujifunze hapa haswa vijana. Mzee huyu kakosa tu kaba na Hana Aibu.

Binadamu lazma uwe na kaba na aibu katika matendo yako narudia haswa sisi watanzania.
Kuishi na walimwengu yahitaji uvumilivu sana.
Hata wewe mwanajf leo, mtu akimsema mtu ambae wewe ni rafiki au mkaribu wako, huyo mtu kwako ni kikwazo na hafai.

Kuna watu tunawaona wako radhi wakumalize kwasababu yamapenzi yao au itikadi zao. Tunachoona drc, palestine, malawi, wakulima na wamasai, haya yote yanatengenezwa kwasababu ya utofauti wa itikadi za makundi haya.
Bwana malisa awe ametishwa au hajatishwa, tishio lake kubwa ni watu wenye mapenzi na Raisi na CCM.

Ukiwa against ukawapandisha hasira hawa, tena mbaya huwafahamu kabisa. Watakuumiza watakuua, wapo watu hapa Tanzania wako hvo haswa vijana wakisasa hawa.
 
Huyo anaogopa nini sasa? Awaulize kina TL,Mbowe,Slaa,Lema na wengine wengi,walikuwa wanaishije hapa hapa Tanzania na waitukuna Serikali na hawaogopi kitu.
 
Uzuri watakao kuua na kukutishia wanajitengenezea laana .Ona sasa watoto wa viongozi walivyo kaputi .Viongozi wanaumwa magonjwa ya kutatanisha nk .Na wao hawaishi milele watakufa tu hata uwe raisi au papa.
 
Ajabu ya wanadamu......

MTU unaipigania dunia mpaka uko tayari kuwaangamiza wanadamu wenzako kana kwamba utaishi milele.....

Unapata ujasiri wa kuwaangamiza, kuwadhuru, kuwaringia na hata kujikweza kwenye huu ulimwengu hali ya kuwa siku moja utakufa na mwili wako utahifadhiwa kwenye kipande kidogo cha ardhi......

Hizo fedha, mali na madaraka vinavyokuvua utu kwa wanadamu wenzako vyote utaviacha na hata ukifukiwa navyo havitakuwa na manufaa yoyote kwako.....

Mwanadamu wewe ambaye maiti yako hata wale wapendwa wako watakuwa wanaiogopa unajivuna nini wewe kwenye mgongo wa ardhi....

Ndugu zangu.... maisha ya mwanadamu hapa duniani ni mfano wa msafiri aliyejificha kivulini........

Vyeo, madaraka na mali visitutie upofu na ujivuni mbele ya binadamu wenzako.......

Siku moja utakufa au kupata mtihani na utaiona dunia chungu.....


TUISHI KWA WEMA.....
 
Back
Top Bottom