Aliyekuwa Mbunge wa Ubungo kupitia CHADEMA, Saed Kubenea amejiondoa ndani ya chama hicho na kujiunga na ACT-Wazalendo

Aliyekuwa Mbunge wa Ubungo kupitia CHADEMA, Saed Kubenea amejiondoa ndani ya chama hicho na kujiunga na ACT-Wazalendo

Basi atakuwa amepatwa na uwendawazimu. Mtu yeyote anayeanza kukisema vibaya chama alichokuwepo kabla, lazima ana shida kichwani.

Siku zote umekaa huko, hukuwahi kulalamika, siku unaondoka au umefukuzwa, unaanza kusema kuwa namwaga mboga - really stupid. Na atakayezingatia unayoyasema, kichwani lazima kuwe na upungufu.

Wenye akili
- Lowasa alipotoka CCM kwenda CDM alisema nini dhidi ya CCM? Alipotoka CDM kwenda CCM alisema nini dhidi ya CDM?

- Dr. Slaa alipotoka CCM kwenda CDM alisema nini dhidi ya CCM? Alipotoka CDM kwenda CCM alisema nini dhidi ya CDM?

- Nyarandu alipotoka CCM kwenda CDM alisema nini dhidi ya CCM?

- Rwakatare alipotoka CUF kwenda CDM alisema nini dhidi ya CUF, alipoenda tena CUF alisema nini dhidi ya CDM

Wapo wengi wa namna hiyo. Hivyo ndivyo wenye akili wanavyofanya.

Lakini wale ambao wanasimama kwenye mstari unaogawanya waliowazima na wenye upungufu wa akili, kama akina Lijuakali, fuatilia walisema nini siku walipoondoka vyama vyao vya awali kwenda vyama vingine. Na ndivyo watakavyofanya watakapoondoka waliko leo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Najaribu kumbuka tu. Hivi Lowassa alipoondoka CHADEMA alisemaje? Mi sikuwepo Ila walokuwepo watasema
 
Tunafahamu kuna mengi unayajua, ndio maana hata msaidizi wa Mbowe ( Kijana wa Rombo ) ilipokuwa ikisemwa amepotea, wewe ulisema yupo na watu wamekutana nae na kuongea.

Utatusaidia sana , yawezekana kama yaliyompata LISSU ni mchezo wa chama cha Mbowe wewe ukafahamu. Na hii inaweza kusaidia taifa kupata ufumbuzi wa mafumbo ambayo tumeshindwa kupata ufumbuzi.. Na hata suala la FARU JOHN wakati akitokea nyumba ndogo Mukya, utata unaweza kumalizwa kabisa. KARIBU KARIBU KARIBU.
 
Hana madhala,alishapima upepo,hata kura za maoni angepigwa chini,limeshakuwa Galasa.
 
Halafu utasikia CHADEMA wanajiendelea kujifariji tu, jikoni fukuto sio la nchi hii.
 
018e5e6ecb3fa5ba4ea510cb58ea3eda

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo

MBUNGE wa Ubungo, Dar es Salaam anayemaliza muda wake kupitia Chadema, Saed Kubenea amejiondoa ndani ya chama hicho na kujiunga na chama cha ACT-Wazalendo.

Kubenea amejiunga na ACT-Wazalendo leo Jumamosi tarehe 18 Julai 2020 na kupokelewa na Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa chama hicho Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Pia, katika hafla hiyo, zaidi ya wanachama 48 wa Chadema wamejiunga na ACT-Wazalendo.

Mara baada ya kukabidhiwa kadi, Kubenea amemshukuru Maalim Seif kwa kumpokea.

Kubenea amesema, “nimelazimika kuondoka huko nilokokuwa. Nawashukuru sana viongozi wakuu bila kuwataka majina waliofanikisha mimi kufika leo.”

“Uamuzi huu haukuwa mwepesi, ulikuwa mgumu sana, kwa sababu katika maisha yangu, hiki ndicho chama cha pili kujiunga,” amesema mwandishi huyo wa habari

Kubenea amesema, “nilifika mahali nikasema, kama Maalim Seif alifika mahali akaondoka CUF aliyoianzisha. Mabere Marando mwasisi wa NCCR-M`ageuzi aliondoka na kujiunga na Chadema na wengine wengine, sembuse mimi.”

“Nilijifunza kwa wazee wangu hawa kwamba lazima safari ya mabadiliko iendelee. Nawashukuru sana wananchi wa Ubungo waliokuja kwenye chama chetu,” amesema

Kubenea amesema, katika Jiji la Dar es Salaam, upinzani una nguvu kubwa na kama vyama vya upinzani vikishirikiana vitafanya vizuri kuliko mwaka 2015 huku akiomba vyama hivyo kutanguliza maslahi ya wananchi mbele kuliko maslahi binafsi.
safari salama
 
Back
Top Bottom