Naamini Kubenea ana kitu kinamsumbua japo hajawa muwazi, maana nikijaribu kutafakari amekuwa akihusishwa na tuhuma za usaliti na hata kuhama chama mara kadhaa na kuna siku aliitisha press conference ikihusishwa na kutangaza kuhama chama japo alibadili gia angani.
Ila imekuwa tofauti na matarajio ya kuhama kwake maana alitarajiwa kuhamia CCM kuunga juhudi ama NCCR-Mageuzi baada ya kugain momentum lakini ameshangaza kuhamia ACT-Wazalendo.
Ameonekana mara kadhaa kupoteza imani ndani ya Chadema na kuonekana hana raha wala amani huko ndani. Nadhani Kubenea ana kitu ambacho hakiko sawa ila amekuwa akijistahi sana kuelezea umma.