Aliyemrekodi Mgonjwa anayedaiwa kuvunja Maadili MOI amechukuliwa hatua gani kwa kuingilia Faragha ya mtu?

Aliyemrekodi Mgonjwa anayedaiwa kuvunja Maadili MOI amechukuliwa hatua gani kwa kuingilia Faragha ya mtu?

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Wakuu, naona kama Watu wengi pamoja na Taasisi ya MOI wamejielekeza na kutupia lawama upande mmoja wa Mgonjwa aliyeonekana akimbusu mpenzi wake Wodini. Kimsingi hakuna kosa lolote alilofanya pale, na sidhani kama kuna sheria inazuia jambo hilo. Labda kama aliyefanya naye kitendo kile ni mtoa huduma za afya katika Taasisi hiyo.

Yule Mgonjwa amevunjiwa Haki zake za Faragha kwa Kurekodiwa na Kusambazwa kwa Video ile. Nategemea Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) na Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) watachukua hatua kwa aliyerekodi na kusambaza video hiyo mtandaoni. Kitendo hicho ni ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kwasababu Mgonjwa amerekodiwa bila ridhaa yake na pasipokujua.

Aidha aliyesambaza mtandaoni pia amevunja sheria ya makosa ya mtandao. Hivyo anapaswa kuwajibishwa kwa kusambaza maudhui yasiyopaswa kuwepo mtandaoni. Hapa mamlaka zisikwepe hili jambo, na pia mamlaka zikumbuke pia zenyewe zinapaswa kuwa mfano wa kulinda haki za faragha za wagonjwa na raia yeyote.

Itashangaza sana hili jambo likiishia upande mmoja wa mgonjwa kuonekana amekosea wakati yeye ndiye amekosewa pale kwa kuingiliwa faragha yake.
 

Attachments

  • 1689131269353.png
    1689131269353.png
    116.6 KB · Views: 7
Sikusoma huu upuuzi ulioundika wote, nimesoma heading tu ila umeandika sijui ukiwa unawaza kwa kutumia nini? Hivi unabeba hiko kichwa kwa ajili ya nini? Hivi kuna faragha inayofanywa mbele za watu? Je aliwarekodi chumbani mwao au? Sijui we ni ME au KE ebu futa huu uzi maana unaonyesha uchi wa akili yako jinsi ulivyo. Utadharaulika sanahumu kwa magreater thinkers.
 
Alierekodi pia alikua na upwiru upwiruu ugwaduuu alitamani pia afanyiwe pia.Tumsamehe tu.
 
Hata ingekuwa ni wewe ungejikuta unarekodi kwa mshangao...

Maana hakuna namna unaiita faragha, halafu ifanyike hadharani...

Kitu kimoja ninachohisi ni kwamba waliorekodiwa haikuwa mara yao ya kwanza, huenda wamekuwa wakifanya hivyo kiasi kwamba mgonjwa mwenza akafikia uamuzi wa kurekodi ili kama mbwai iwe mbwai...
 
Sikusoma huu upuuzi ulioundika wote, nimesoma heading tu ila umeandika sijui ukiwa unawaza kwa kutumia nini? Hivi unabeba hiko kichwa kwa ajili ya nini? Hivi kuna faragha inayofanywa mbele za watu? Je aliwarekodi chumbani mwao au? Sijui we ni ME au KE ebu futa huu uzi maana unaonyesha uchi wa akili yako jinsi ulivyo. Utadharaulika sanahumu kwa magreater thinkers.
Watu wengine hubeba vichwa kama dispenser ya kuhifadhia mate tu.
 
View attachment 2685367
Wakuu, naona kama Watu wengi pamoja na Taasisi ya MOI wamejielekeza na kutupia lawama upande mmoja wa Mgonjwa aliyeonekana akimbusu mpenzi wake Wodini. Kimsingi hakuna kosa lolote alilofanya pale, na sidhani kama kuna sheria inazuia jambo hilo. Labda kama aliyefanya naye kitendo kile ni mtoa huduma za afya katika Taasisi hiyo.

Yule Mgonjwa amevunjiwa Haki zake za Faragha kwa Kurekodiwa na Kusambazwa kwa Video ile. Nategemea Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) na Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) watachukua hatua kwa aliyerekodi na kusambaza video hiyo mtandaoni. Kitendo hicho ni ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kwasababu Mgonjwa amerekodiwa bila ridhaa yake na pasipokujua.

Aidha aliyesambaza mtandaoni pia amevunja sheria ya makosa ya mtandao. Hivyo anapaswa kuwajibishwa kwa kusambaza maudhui yasiyopaswa kuwepo mtandaoni. Hapa mamlaka zisikwepe hili jambo, na pia mamlaka zikumbuke pia zenyewe zinapaswa kuwa mfano wa kulinda haki za faragha za wagonjwa na raia yeyote.

Itashangaza sana hili jambo likiishia upande mmoja wa mgonjwa kuonekana amekosea wakati yeye ndiye amekosewa pale kwa kuingiliwa faragha yake.
Kaka unajua kingereza lakini? Hizo faragha ulizoandika hapo hazihusiani na mahaba zinahusiana na matibabu kati ya mgonjwa na mtoa tiba.
 
View attachment 2685367
Wakuu, naona kama Watu wengi pamoja na Taasisi ya MOI wamejielekeza na kutupia lawama upande mmoja wa Mgonjwa aliyeonekana akimbusu mpenzi wake Wodini. Kimsingi hakuna kosa lolote alilofanya pale, na sidhani kama kuna sheria inazuia jambo hilo. Labda kama aliyefanya naye kitendo kile ni mtoa huduma za afya katika Taasisi hiyo.

Yule Mgonjwa amevunjiwa Haki zake za Faragha kwa Kurekodiwa na Kusambazwa kwa Video ile. Nategemea Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) na Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) watachukua hatua kwa aliyerekodi na kusambaza video hiyo mtandaoni. Kitendo hicho ni ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kwasababu Mgonjwa amerekodiwa bila ridhaa yake na pasipokujua.

Aidha aliyesambaza mtandaoni pia amevunja sheria ya makosa ya mtandao. Hivyo anapaswa kuwajibishwa kwa kusambaza maudhui yasiyopaswa kuwepo mtandaoni. Hapa mamlaka zisikwepe hili jambo, na pia mamlaka zikumbuke pia zenyewe zinapaswa kuwa mfano wa kulinda haki za faragha za wagonjwa na raia yeyote.

Itashangaza sana hili jambo likiishia upande mmoja wa mgonjwa kuonekana amekosea wakati yeye ndiye amekosewa pale kwa kuingiliwa faragha yake.
sawa sawa
 
Hiyo video iko wapi! Mbona mnatuchanganya tu sisi wengine ambao tuko dunia ya 3!
 
Back
Top Bottom