Aliyemuelewa Mo Dewji kuhusu uwekezaji Simba atujuze

Aliyemuelewa Mo Dewji kuhusu uwekezaji Simba atujuze

Wasio na akili timamu utawasikia wakisema ili mradi timu yao inafanya vizuri viwanjani haya mengine hayawahusu.

Kumbe ni ujinga umewajaa kichwani na baadae huko mbele mambo yakienda mlama watashindwa kutafuta mchawi ni nani.
Hawana uwanja,hawana jengo zuri la timu lililopo pale kariakoo ni maduka tu.
 
Muda mnaopeteza kujadili mapungufu ya hasimu wenu simba mngekuwa mnaijenga yanga hakika mngekuwa mbali sana
Wewe ni miongoni mwa watu mliopigwa sindano ya ganzi ya mo na wenzake friends of Simba. Ili kuiondoa hiyo ganzi meza dawa ya kigwangalaquine ili uone Simba inavyomtajirisha mo na kundi lake. Unafahamu gharama halisi ya kuweka tangazo la biashara yako kwenye jezz na magari ya timu kubwa kama Simba yenye mashabiki wengi Africa na duniani? Uliza Rwanda inalipa hela ngapi kuweka katangazo kake ka Visit Rwanda kwenye jezi ya Arsenal? Hata mo ni mchumi, anaijuwa gharama ya kutangaza biashara kwenye jezi ya timu inayofanya vizuri ni ghali, ndiyo maana anasema "sikubali" kutangaza bidhaa ya Sportpesa Africa nzima kwa pesa ile anayotoa Sportpesa msimu uliopita. Lakini yeye ametangaza mo energy lakini bado analalamika amepoteza 24.3b. majuha TU kama wewe ndio wanamuelewa.
 
Hela kuitoa inauma wewe asikuambie mtu. Ushawahi kupewa hela na mkeo uone utakavyosimangwa?
Mo anahitaji kupongezwa sana.
Ameombwa? hata bila yeye wawekezaji wapo na ndiyo maana na yeye amekiri yeye kaikuta Simba na ataiacha.
 
Kama ni hivyo basi asingeitisha press conference kumbe wadhamini wanafahamu kila kitu. Ametusumbua kutuita kwasababu gani kama kila kitu kinafahamika kwenye kamati. Mo peke yake ndiye katoa 20b za 49% ya hisa, kanuni inasema hivyo?
Press ya jana ilikua ni kuueleza umma juu ya walipofikia katika uwekezaji na mchakato wa mabadiliko ya Simba.

Haimaanishi kwamba jana ndio wameeleza kila kitu (further details) pale. Ndio maana nikashauri kama wewe unataka hizo deep info unaweza kuzipata kama ukifuatilia kwenye ngazi husika (FCC, kwenye vikao vya klabu, kupitia vyanzo mbalimbali vya habari vya klabu, n.k). Kama kukwambia ufanye hivi ni kumaanisha kwamba press ya jana haikua na umuhimu, basi unisamehe sana.

Nitoe mfano mdogo tu:
Udhamini wa bidhaa za Mo kwenye jezi za Simba ni wa kimkataba, ilifanyika press wakasaini na kutangaza kwa umma.
Sasa wewe unapotumia suala la udhamini huu kama ishara ya "utapeli" wa Mo, ina maana ama haufuatilii kinachoendelea, au umeamua tu kutuuliza "akina sisi" ili kama hatuna kumbukumbu juu ya hili tuungane nawewe katika kumlalamikia Mo.
Kwanini usingejiridhisha kwamba udhamini ule si wa kimkataba na klabu haipati pesa, ndipo hoja hiyo uijumuishe katika madai yako hapo juu ?
Ina maana unataka Mo aanze kuyazungumzia mambo haya kwenye press mkuu ?

Sikubezi katika hoja zako, ila naona kwamba mengi unayoyahoji unaweza kuyapatia majibu katika ngazi sahihi endapo ukiamua kufuatilia.

Kuhusu suala la MO PEKE YAKE kutoa 20B:
Kama kwenye structure ya Simba inaruhusu mtu mmoja kuweka 20B na akachukua 49% ya hisa, kosa la Mo hapa linakua ni lipi ?

Kama unafahamu kwamba structure ya Simba inataka wawekezaji wanne ndio wagawane hizo 49% sema hapa ili tujue kwamba Mo amekiuka kipengele hicho, na useme ni ibara ipi au sheria ipi iliyokiukwa.

Kama unafanya marejeo kwenye timu nyingine nadhani utakua unakosea na unalazimisha mambo yaende your way.

Ripoti za mapato na matumizi ya klabu zipo, unataka Mo aje kwenye press kuzisoma pale ili nawewe ufahamu kwamba deficit zilikua kiasi gani na akaongezea hela yake ?
Hivi ndivyo taasisi zinaendeshwa ?
Kusomeana mapato na matumizi kwenye vyombo vya habari ?

Ndugu yangu mambo mengi uliyoyahoji hapo unaweza kuyapatia majibu kirahisi sana, haujaamua tu. Niamini mimi.
 
Binafsi nilimsikiliza Mohamed Dewji kuhusu utoaji wa 20 billion za hisa 49%. Huyu Bwana anaonekana anatoa hela lakini ananung'unika na kulalama kama vile mtu anaelazimishwa. Anataka aonewe huruma na watu wasihoji chochote kwakuwa anatoa pesa. Yaani asiwepo mtu anayehoji kwakuwa timu inaleta makombe.

Hii ni hatari sana Simba kumpa mtu kama huyu 49% peke yake kabisa kabisa. Ogopa sana mtu anayelalama wakati anakuhudumia, muda wowote atakuacha.

Ambacho sijamuelewa ni:

1. Hiyo tume ya fair competition amemalizana nayo kivipi?
2. Zile 49% hiza ni zake zote mtu mmoja? Kama sio mbona cheque imetoka kwa mo peke yake, hao wawekezaji 2 wengine wanaotakiwa na kanuni wako wapi na ni Nani?

3. Alisema ameihudumia Simba 24.3b kwa miaka 4, hizo ni pamoja get collections, mauzo ya jezz, michango ya wanachama, bonuses za kuingia hatua ya makundi na robo finali, bonus za Sportpesa, zawadi za ushindi wa ligi na FA, Sportpesa, haki za matangazo na kodi za majengo ya Simba?

4. Je, matangazo yake ya mo energy kwenye jezz ya Simba thamani yake ni sh ngap, anailipa Simba kiasi gani kutangaza? Je, Iko humo kwenye 24.3b alizodai ameipa Simba?

5. Kwanini huwa analalamika kuhusu kuihudumia timu kila anapopata nafasi ya kuzungumza?

6. Je, hizo 20b ameshazilipa kwenye account ya Simba tayari au ndio anataka kwenda kuzilipa?
Mashabiki wa Liverpool FC, Manchester United, FC Barcelona, Real Madrid, Bayern Munich, PSG, AC Milan, Al Ahly, Mamelodi Sundowns, TP Englebert Mazembe, Kaizer Chiefs FC na Simba SC hatuna haja sana ya kujua Mapato, ila tuna haja mno ya Ubingwa na Klabu zetu Kuzidi Kung'aa Locally na Internationally kama zing'aavyo sasa.

Hivi kwa Mfano kama Mimi GENTAMYCINE nasikia Simba SC inachukua Ubingwa wa VPL na ASFC tena mfululizo huku katika CAF CL najitahidi kufanya vyema na hata huyo ( hao ) Wababe wa Afrika akina Al Ahly na Kaizer Chiefs nawafunga na Moyo wangu Unaridhika huku nikinenepa kwa Furaha hizo Pesa za Mo au kama anatuibia Simba SC zinanihusu nini?

Halafu kuna Watu wengine ni Wapumbavu na mna Wivu wa Kiuswahili. Hivi kuna Mfanyabiashara ambaye anawekeza kisha nae asitafute mwanya wa Kupiga Hela na Kujifaidisha na Kujitajirisha zaidi? Mnafiki mkubwa Wewe na Chuki zako na Mawazo yako haya ya Kimasikini.

Unashangaa Mo Dewji Kujitajirisha kupitia Simba SC mbona hushangai GSM alivyowadanganyeni Yanga SC kuwa tokea aingie hapo amechapisha tu Jezi 80,000 wakati ukweli ni kwamba mpaka hivi sasa GSM amechapisha Jezi 250,000 za Yanga SC? au unataka sasa tunaoyajua ya ndani ya Yanga SC kupitia Viongozi wao Waandamizi ambao ni Marafiki zetu tuseme yanayoendelea huko Yanga SC Kwenu ili Amani itoweke na Mvurugane zaidi?

Mo tuibie Baba, ila tupe raha Simba SC!!
 
Nae keshajua kuwa Simba ni majuha, kushinda mechi, na ubingwa kunawanyamazisha kimyaa na kuwafanya wakenue tu kama maombie. Hivyo atafanya kila ajuacho na awezalo kuhakikisha timu inashinda, maana hiyo ndiyo ganzi ya wanasimba. Ona anaongelea kawakopesha Simba 24.3b lakini hasemi kuhusu mapato ya zile nyomi za Haji Manara viwanjani, mauzo ya jezz, bonus za ubingwa, kutangaza bidhaa zake kwakutumia Simba wala kuuza wachezaji, wala kodi za majengo wala wadhamini.

Wajanja kama Dr. Kingwangala ni wachache sana, na hao wanapigwa vita na mazombie wasihiji. Bila akina kingwangala hizo 20b zisingeletwa hakiya mama.
Hivi we jamaa unaongea nini ?
Unajua unashangaza ....

Unazungumzia mauzo ya wachezaji ?
Ndani ya miaka minne Simba imemuuza mchezaji gani hata kwa angalau MILIONI MIAMOJA ?
 
We Manara we, mbona wewe kinganganizi, sana. Umeona utumie JF kumsagia aliyekuwa boss wako? Kwani Mo kakukosea nini? Tuache simba yetu.
Nusu kaputi ya mo imekukolea. Mo hawezi kuweka mchanganuo wa haki ya Lilah kuhusu matumizi hizo 24.3b. Huenda humo zimo pia za kununua mechi, waamuzi, wazee wa Simba, wajumbe wa tume ya Fair competition, nk. Ataziandikaje in public?
 
Hili liko wazi kabisa, ila kwakuwa wanasimba wengi ni mbumbumbu hawawezi kuliona hili, leo wanakenua kwakuwa simba wanafanya vizuri, kesho hali ikiwa tofauti wataanza kungaka, huu ni unafiki kama waliomfanyia Haji

Mo mwenyewe amekiri simba ina fanbase around 60% hii ni potential kwakwe kibiashara lazima anapiga hela kwa kutumia fanbase kifupi matangazo yake yote anatumia mgongo wa simba kutangaza kufikia hao 60% kwenye mahesabu yake ya Kampuni gharama alizotumia anakuja kuziweka kwenye hesabu za kampuni kama matumizi hapo anapata nafuu ya kodi kwenye kampuni.
 
Hiyo nyomi huwa haileti zaidi ya 400M lakini mishahara ya Simba kwa mwezi ni 350M ukumbuke hizo nyomi sio kila mwezi.
Usajili Simba ni wa hela kubwa let say extension contact ya chama ni 500M lakini konde boy alinunuliwa kwa 650M bado chikwende ,Fraga nae alitumia zaidi ya 300M Sasa hapo ona taswira ya bajeti ya Simba kwa msimu moja
Huyu jamaa sijui hata humo kichwani kwake zimo, eti ametaja kuuza wachezaji kama chanzo cha mapato cha Simba (akijumuisha na mapato ya mlangoni, nashukuru hili umemjibu).

Kwa misimu minne iliyopita Simba haijaingiza hata MILIONI 200 kwa kuuza wachezaji, wengi wameondoka free agents, sasa sijui anapata wapi ujasiri wa kusema kwamba simba imepata mapato kwa kuuza wachezaji.

Humu JF tunatakiwa kuvumiliana sana.
 
Wewe chura FC ukishajua itakusaidia nn?? Cc wanasimba ata akitoa jero tunaomba apewe timu yote aimiliki na akipenda abadilishe na jina iwe Mo FC muhimu mashabiki tunapata FURAHA timu inafanya maajabu basi tunafurahi ayo mengine ni kukompliketi mambo mwaisa
Naomba nihifadhi haya maneno yako kwa faida ya kizazi kijacho.

Rage hakuwa mjinga hata kidogo kuwaita mbumbumbu. Na huu ndiyo ushahidi wa wazi kabisa.
 
Hiyo nyomi huwa haileti zaidi ya 400M lakini mishahara ya Simba kwa mwezi ni 350M ukumbuke hizo nyomi sio kila mwezi.
Usajili Simba ni wa hela kubwa let say extension contact ya chama ni 500M lakini konde boy alinunuliwa kwa 650M bado chikwende ,Fraga nae alitumia zaidi ya 300M Sasa hapo ona taswira ya bajeti ya Simba kwa msimu moja
Sawa sasa alitakiwa anyooshe maelezo yake pale kwamba hizo 24.3b ni top up kwenye mapato ya Simba. Lakini pale amesema gharama za kuiendesha Simba kwa mwaka ni 5.1b na zote amezitoa yeye mfukoni mwake, ndiyo maana akatuambia ametumia 24.3b, hakusema ni top up, yaani Simba haina chanzo chochote Cha pesa except mo. Hii ni dharau kwa wanasimba.
 
Kuwekeza siyo kujitolea. Ni lazma uwekeze na upate faida ya uwekezaji. Mo hajawahi kuweka faida anayoipata kwa uwekezaji wake na kimsingi anapata pesa nyingi kuliko alichowekeza. Its just business si kwamba anaipenda sana Simba No ni source of income kwake. Cha msingi hapa simba wangeweka wazi ili hata wawekezaji wengine wawe huru kuwekeza.
Hata iweje lazima awauze miquson konde boy na chama avute mkwanja mrefu. Chezea mo wewe.
 
Wewe chura FC ukishajua itakusaidia nn?? Cc wanasimba ata akitoa jero tunaomba apewe timu yote aimiliki na akipenda abadilishe na jina iwe Mo FC muhimu mashabiki tunapata FURAHA timu inafanya maajabu basi tunafurahi ayo mengine ni kukompliketi mambo mwaisa
Yule ni mtu,atakufa.

Timu itakuwa kama Mwadui.
 
Hili liko wazi kabisa, ila kwakuwa wanasimba wengi ni mbumbumbu hawawezi kuliona hili, leo wanakenua kwakuwa simba wanafanya vizuri, kesho hali ikiwa tofauti wataanza kungaka, huu ni unafiki kama waliomfanyia Haji

Mo mwenyewe amekiri simba ina fanbase around 60% hii ni potential kwakwe kibiashara lazima anapiga hela kwa kutumia fanbase kifupi matangazo yake yote anatumia mgongo wa simba kutangaza kufikia hao 60% kwenye mahesabu yake ya Kampuni gharama alizotumia anakuja kuziweka kwenye hesabu za kampuni kama matumizi hapo anapata nafuu ya kodi kwenye kampuni.
Mkuu, kwani wewe unatatizwa na watu kupata faida wakiwekeza sehemu ?

1. Mo akiwekeza Simba akapata faida, hupendi ?
2. GSM, Manji, Rostam wakiwekeza Yanga na wakapata faida, hupendi ?
3. Motsepe akiwekeza Mamelodi akapata faida, unaumia ?
4. Glaziers wakiwekeza Man Utd na wakapata faida, unateseka ?
5. Sheikh Mansour akiwekeza City na akapata faida, roho inakuuma ?


Wewe mwenyewe UKIWEKEZA kwenye KILIMO au sekta ya MADINI na UKAPATA FAIDA, huwa unaumia pia ?

Mbona kama inataka kuonekana kwamba habari njema kwako ni pale tu ambapo Mo atakua HAFAIDIKI kwa chochote kwenye uwekezaji wake pale Simba ?

Ujuaji, Wivu na Roho mbaya vitatumaliza watanzania (nikiwemo mimi).
 
Kwahiyo uliupate taarifa hizo sisi wote tushiriki vikao vya simba?
Umekaza sana kichwa, nice moves, kwaiyo wewe huwezi ku access vyanzo vya habari vya FCC hadi ushiriki vikao vya Simba mkuu ?
 
Wewe ni miongoni mwa watu mliopigwa sindano ya ganzi ya mo na wenzake friends of Simba. Ili kuiondoa hiyo ganzi meza dawa ya kigwangalaquine ili uone Simba inavyomtajirisha mo na kundi lake. Unafahamu gharama halisi ya kuweka tangazo la biashara yako kwenye jezz na magari ya timu kubwa kama Simba yenye mashabiki wengi Africa na duniani? Uliza Rwanda inalipa hela ngapi kuweka katangazo kake ka Visit Rwanda kwenye jezi ya Arsenal? Hata mo ni mchumi, anaijuwa gharama ya kutangaza biashara kwenye jezi ya timu inayofanya vizuri ni ghali, ndiyo maana anasema "sikubali" kutangaza bidhaa ya Sportpesa Africa nzima kwa pesa ile anayotoa Sportpesa msimu uliopita. Lakini yeye ametangaza mo energy lakini bado analalamika amepoteza 24.3b. majuha TU kama wewe ndio wanamuelewa.
WIVU, UJUAJI na ROHO MBAYA.

Uwe na siku njema ndugu mtanzania mwenzetu.
 
Yule ni mtu,atakufa.

Timu itakuwa kama Mwadui.
Wale wengine (watatu) wa kule Yanga wataishi milele kwani ?

Abromovic ataishi miaka bilioni ?

Kwa kifupi ni kwamba hoja ya kufa ni dhaifu sana.

Sema tu nimekuelewa "mwanetu", umeona tunastahili kupewa "nondo" za namna hiyo asubuhi hii.
 
Wale wengine (watatu) wa kule Yanga wataishi milele kwani ?

Abromovic ataishi miaka bilioni ?

Kwa kifupi ni kwamba hoja ya kufa ni dhaifu sana.

Sema tu nimekuelewa "mwanetu", umeona tunastahili kupewa "nondo" za namna hiyo asubuhi hii.
Mkuu,kila mtu anakufa.

Hoja yangu ilitokana na comment iliyosema "hata akitoa jero,waanasimba wanataka furaha"

Yaan akiondoka ataacha nini kwa kutoa jero?
 
Back
Top Bottom