Aliyemuelewa Mo Dewji kuhusu uwekezaji Simba atujuze

Aliyemuelewa Mo Dewji kuhusu uwekezaji Simba atujuze

Mbumbumbu katika ubora wao muachwe na litimu lenu maana Mo anawapa mapenzi motomoto hamuoni wala hamtaki kusikia , kila kitakachohojiwa ni utopopolo.
Mngepewa nchi hii nyie mngeshatuuza watanzania wote kwa mabeberu maana so kwa upofu huo wa akili.
Wewe unaumia nn babu kwenu hili au Simba ndio rizk
 
Kuhusu kampuni zinazojitangaza kupitia jezi, tazama hii...



Kila kitu kiko wazi, sema labda haufuatilii au umeamua kwa makusudi "kumsagia kunguni" bwana Mohamed.

Hiyo pesa ya udhamini kupitia mo extra ni sehemu ya 24.3b? Nani alipanga kiwango cha udhamini? Je, makampuni ya Azam, Jambo drinks, sayona, Afiya, nk yalishindanishwa ili kupata hiyo 250ml?
 
Apo suhala la kuhoji ni ayo mapato ya timu ata mm kwa upande wang sijaelewa timu ina mikataba zaid ya minne ukijumlisha na mengne inaweza kufka ata 2bl kwa mwaka,sasa mo anasema anatoa pesa kama yeye karbu 5 bl sio kama haiwezekan ila vzur angeelezea kwamba simba pamoja na mikataba yake na mapato yake yote kwa mwaka ni kias fulan matumiz ya timu kwa ujumla ni kias fulan kwaiyo apo ingekua rahis kujua kat ya mapato ya simba mo anaongezea kias gan ukisema ww unatoa kias fulan bila kusema timu inaingiza kias gan apo kuna ukakasi,ayo mengine sio kama mo analalamika ila ni anaongea kile anachofanya mtu ambae anatoa ela au ktu ikitokea siku anaongea hadharan lazma aseme kile anachofanya maana aliaid kufanya ayo anayosema kama atakaa kimya tu nan atajua sasa ,kama unakumbuka gsm walipishana kidogo kaur na uongoz wakatishia kujitoa ktk barua yao walielezea meng kuanzia mkataba wanachotakiwa kufanya lkn wakaongeza na mengine ambayo walisema wanafanya kwa mapenz nje ya mkataba sio kama waliongea vile kwa kulalamika ila umma ujue nin umuhimu wao na nn wanafanya

Mkuu, kwanza jana Mo hakwenda kwenye press kusoma ripoti ya mapato na matumizi.

Pili, kulikua na maneno mitandaoni kwamba Mo hataki kuweka ile 20B kwa sababu anaona ameshaihudumia timu na "Duniani hakuna cha bure" hivyo watakatana juu kwa juu.

Lengo la kusema kwamba hizo 24B kwa miaka minne alikua anatoa kwa mapenzi yake kuisaidia klabu lakini hiyo 20B iko palepale na anaitoa.
Tena alisema pale kabisa kwamba anaweka 20B ili kuondoa hayo maneno maneno (maana yake maneno yalikuwepo).

Sasa je, kusema hivyo ni kosa ?
Kusema hivyo kunamaanisha Simba ilikua haina chanzo kingine cha mapato ?

Leo hii tuseme kwamba GSM haisaidii Yanga pale hivi tutakua na akili kweli ?
GSM akisema alikua anatoa hizo pesa kwa sababu ya mapenzi yake Yanga litakua ni kosa ?
Akisema hivyo atakua anamaanisha Yanga ilikua haipati pesa toka Sportpesa, viingilio n.k ?
Ili kuyazungumza hayo tunahitaji kusomewa ripoti ya mapato na matumizi kwanza ?

Haya, mapato ya Simba au Yanga kwa mwaka (miaka minne iliyopita) tuseme ni roughly bilioni 3.

Hivi wewe unaweza kuendesha klabu ya Simba au Yanga msimu mzima kwa 3B ? Mtu akisema aliongezea inakua nongwa ?
3B unawezaje kusajili wachezaji wazuri, ukalipa mishahara mizuri, posho nono, wakasafiri kwa ndege msimu mzima, wakalala kwenye hoteli za maana, wakala vizuri, program za mazoezi zikaenda vizuri, ukaboresha benchi la ufundi kwa kuleta wataalam wa kila namna na mengineyo ?

Labda tusaidie wewe mkuu, huenda tatizo haliko kwa Mo na halitakuwepo kwa GSM, labda tuna shida kwenye budgeting.

Help us, utakua umesaidia soka la nchi hii.
 
Wewe chura FC ukishajua itakusaidia nn?? Cc wanasimba ata akitoa jero tunaomba apewe timu yote aimiliki na akipenda abadilishe na jina iwe Mo FC muhimu mashabiki tunapata FURAHA timu inafanya maajabu basi tunafurahi ayo mengine ni kukompliketi mambo mwaisa
Ww iko tumishi ya Muhindi,!!
 
Sawa lakini wao hawalalamiki wanazihudumia timu zao. Mo alitishia kujivua uwenyekiti na udhamini wakati timu ilipofungwa. Hatujawahi kusikia mwekezaji wa arsenal, Chelsea, Liverpool, Manchester united anawajambisha wanachama na shabiki wa timu kwa kutishia kujiuzulu pale timu inapofungwa. Mmiliki ambae anataka timu yake ishinde tuuuuuuu mechi zote kwakuwa analipa pesa zake vinginevyo anajiuzulu ni mwekezaji gani? Ni ligi gani hiyo duniani ambayo timu lazima ishinde mechi zote?
Mo atatuharibia mpira wetu kama tusipokuwa makini kwa kufanya "kila kitu" ili Simba ishinde kila mechi.
Kuna mapungufu madogo madogo ambayo kila binadamu anayo, hilo haliwezi kuwa ndio kiini cha mjadala. Kuna wakati hata wewe unaweza kupata hasira juu ya jambo fulani na ukafanya maamuzi ukiwa na hali hiyo na yasiwe mazuri.
Lakini toka Mo awepo Simba, timu hiyo imefungwa mechi nyingi tu, imetolewa kwenye mashindano mbalimbali (ikiwamo raundi ya kwanza kenywe ligi ya mabingwa), na huyo Mo hajatoa kauli kama hizo katika matukio yote.

Je, kiongozi wa timu anapaswa kuwa anakubali defeat kirahisi ?

No, timu yoyote kubwa inapaswa kuwa na winning mentality at first place. Hii inaenda hadi kwa wachezaji kwamba tunatakiwa kupambana, vinginevyo bosi hatatuelewa, mashabiki hawatatuelewa.
Hii inaongeza morali ya mapambano.
Japokua tunaposhindwa ni lazima tukubali, maana mwisho wa siku katika mchezo sio kila siku mshindi utakua ni wewe.

Bottom line:
Mkuu, mimi na weww tunaweza kujadiliana haya mambo hata kwa siku nne mfululizo, lakini naamini sitaweza kubadili mtazamo wako juu ya Mo Dewji.
Huo mtazamo kamwe usiubadili (just be real, its your life anyways), lakini ninachokuomba ni kitu kimoja tu, judge that guy on fair grounds.
 
Kama tapeli wekeni nyie basi, kwani Simba imeanza Leo. Utopolo umaskini wa tumbo na akili unawasumbua
 
Binafsi nilimsikiliza Mohamed Dewji kuhusu utoaji wa 20 billion za hisa 49%. Huyu Bwana anaonekana anatoa hela lakini ananung'unika na kulalama kama vile mtu anaelazimishwa. Anataka aonewe huruma na watu wasihoji chochote kwakuwa anatoa pesa. Yaani asiwepo mtu anayehoji kwakuwa timu inaleta makombe.

Hii ni hatari sana Simba kumpa mtu kama huyu 49% peke yake kabisa kabisa. Ogopa sana mtu anayelalama wakati anakuhudumia, muda wowote atakuacha.

Ambacho sijamuelewa ni:
1. Hiyo tume ya fair competition amemalizana nayo kivipi?

2. Zile 49% hiza ni zake zote mtu mmoja? Kama sio mbona cheque imetoka kwa mo peke yake, hao wawekezaji 2 wengine wanaotakiwa na kanuni wako wapi na ni nani?

3. Alisema ameihudumia Simba 24.3b kwa miaka 4, hizo ni pamoja get collections, mauzo ya jezz, michango ya wanachama, bonuses za kuingia hatua ya makundi na robo finali, bonus za Sportpesa, zawadi za ushindi wa ligi na FA, Sportpesa, haki za matangazo na kodi za majengo ya Simba?

4. Je, matangazo yake ya mo energy kwenye jezz ya Simba thamani yake ni sh ngap, anailipa Simba kiasi gani kutangaza? Je, Iko humo kwenye 24.3b alizodai ameipa Simba?

5. Kwanini huwa analalamika kuhusu kuihudumia timu kila anapopata nafasi ya kuzungumza?

6. Je, hizo 20b ameshazilipa kwenye account ya Simba tayari au ndio anataka kwenda kuzilipa?
Mbona pilipili ziko shambani wewe unawashwa ukiwa mezani? Hayakuhusu haya. Kausha.
 
Mo tapeli Tu na sitashangaa Simba ikimshinda
Alishindwa Singida united akakimbia
Akashindwa Africa Lyon akakimbia..

Ana usanii mwingi
Hayo maswali watu wengi wanauliza..
Kubandika bidhaa zake .. kwenye magari na kesi..je Simba walitangaza bid?
Kampuni yake ndo highest bidder?
Au analazimisha kwa bei anayotaka?

Maswali mengi kuliko majibu
Dua ya kuku hiyo wewe mtopolo
 
Mo tapeli Tu na sitashangaa Simba ikimshinda
Alishindwa Singida united akakimbia
Akashindwa Africa Lyon akakimbia..

Ana usanii mwingi
Hayo maswali watu wengi wanauliza..
Kubandika bidhaa zake .. kwenye magari na kesi..je Simba walitangaza bid?
Kampuni yake ndo highest bidder?
Au analazimisha kwa bei anayotaka?

Maswali mengi kuliko majibu
Wanasimba hili watakuja kutueleza siku moja, coz timu haiwezi kuendelea kufanya vizuri siku zote
 
Raha sana kusoma maoni / mawazo ya watawatanzania iwe ktk siasa .uchumi au michezo
 
Mo tapeli Tu na sitashangaa Simba ikimshinda
Alishindwa Singida united akakimbia
Akashindwa Africa Lyon akakimbia..

Ana usanii mwingi
Hayo maswali watu wengi wanauliza..
Kubandika bidhaa zake .. kwenye magari na kesi..je Simba walitangaza bid?
Kampuni yake ndo highest bidder?
Au analazimisha kwa bei anayotaka?

Maswali mengi kuliko majibu
Kama hujui si ni vema kuuliza upate majibu kuliko kujifanya unajua wakati wewe ni mpumbavu tu!!mijitu kama nyinyi kujifanya hujuaji wakati hata kufanya biashara ya kuuza karanga ujawahi kufanya,wakati kila siku CCM inawapa chumvi na kanga mnashangilia kwa kukata mauno.
Unapoandika jambo na ulijui wakati ukweli wake unajulikana ni kuonyesha namna gani una mtindio wa ubongo
 
Nae keshajua kuwa Simba ni majuha, kushinda mechi, na ubingwa kunawanyamazisha kimyaa na kuwafanya wakenue tu kama maombie. Hivyo atafanya kila ajuacho na awezalo kuhakikisha timu inashinda, maana hiyo ndiyo ganzi ya wanasimba. Ona anaongelea kawakopesha Simba 24.3b lakini hasemi kuhusu mapato ya zile nyomi za Haji Manara viwanjani, mauzo ya jezz, bonus za ubingwa, kutangaza bidhaa zake kwakutumia Simba wala kuuza wachezaji, wala kodi za majengo wala wadhamini.

Wajanja kama Dr. Kingwangala ni wachache sana, na hao wanapigwa vita na mazombie wasihiji. Bila akina kingwangala hizo 20b zisingeletwa hakiya mama.
Hawa watu usiwaamshe uwaache hivyo hivyo , kwasababu wakiambiwa ukweli wanaanza kurusha mawe, huo utapeli wa mo wenye akili timamu tulishauona kitambo, uwezi ukawa unalia lia kila siku eti Unapata hasara kwenye timu wakati umeing'ang'ani a iyo timu utaki kuanzisha ya kwako ikupe faida ni kichekesho, kwa miaka 4 yeye amefaidika kiasi gani kwenye biashara zake kupitia mgongo wa simba? Mashabiki wao wanasema wanachotaka ni timu Kufanya vizuri je watapoanza kupoteana ndo wataanza kuhoji? Maana yanga namna wanavyojipanga uko mbele ya safari mambo yatakuwa magumu Sana kwa simba katika nyanja zote
 
Kuwekeza siyo kujitolea. Ni lazma uwekeze na upate faida ya uwekezaji. Mo hajawahi kuweka faida anayoipata kwa uwekezaji wake na kimsingi anapata pesa nyingi kuliko alichowekeza. Its just business si kwamba anaipenda sana Simba No ni source of income kwake. Cha msingi hapa simba wangeweka wazi ili hata wawekezaji wengine wawe huru kuwekeza.
Nani amekatazwa kwenda kuwekeza simba? hao unaozani wanaweza kuwekeza simba walikuwa wapi kabla mo hajawekeza? ligi kuu bara haina mdhamini nenda kaizamini wewe basi
 
Hawa watu usiwaamshe uwaache hivyo hivyo , kwasababu wakiambiwa ukweli wanaanza kurusha mawe, huo utapeli wa mo wenye akili timamu tulishauona kitambo, uwezi ukawa unalia lia kila siku eti Unapata hasara kwenye timu wakati umeing'ang'ani a iyo timu utaki kuanzisha ya kwako ikupe faida ni kichekesho, kwa miaka 4 yeye amefaidika kiasi gani kwenye biashara zake kupitia mgongo wa simba? Mashabiki wao wanasema wanachotaka ni timu Kufanya vizuri je watapoanza kupoteana ndo wataanza kuhoji? Maana yanga namna wanavyojipanga uko mbele ya safari mambo yatakuwa magumu Sana kwa simba katika nyanja zote
Acha mambo ya ramli mzee, subiri hao yanga wajipange sio kutabiri upuuzi hapa
 
Huwezi amini wana misimu minne hawajashinda taji lolote sio ligi kuu wala FA .. baada ya kukaa kutathmini namna gani wanaweza kufanya vizuri msimu ujao, wenyewe wako bize na ishu za mabingwa wa nchi huku kila siku wakiambiwa "VIMBA MWANANCHI VIIMBAA!! [emoji23][emoji23]" ..

Siku si nyingi tutaanza kuwaona uwanja wa ndege wakipokea " magarasa" yao mapya huku wakishangilia na wakimbeba Engineer hersi [emoji23][emoji23], alafu boom ligi imeisha bingwa Simba ..

Ifike wakati sasa yanga mchomoe hiyo miiko huko nyuma, Yani huwezi amini hakuna kitu kigumu kama kubishana na shabiki wa yanga hata kama jambo lipo wazi ..

ACHA ITUUE TUMEIPENDA WENYEWE [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ..
 
Sawa wanasimba tumekubali janja janja ya Mo,tuje kwenu nyinyi vyura ambao muwekezaji wenu sio janjajanja mnamafanikio gani tangia gsm achukue umiliki wa jezi za Yanga?
 
Wasio na akili timamu utawasikia wakisema ili mradi timu yao inafanya vizuri viwanjani haya mengine hayawahusu.

Kumbe ni ujinga umewajaa kichwani na baadae huko mbele mambo yakienda mlama watashindwa kutafuta mchawi ni nani.

Wewe mwenye akili zako unaona shida iko wapi, na hao wasiokua na akili hasara ipi watakayoipata kutokana na Mo kununua hizo hisa? Siku GSM wakinunua hisa hapo utopolo i utaandamani sababi maslahi yako yatakuwa hatarini ama ndo utashangilia kwa vile utopolo imepata mwekezaji atakae waepusha na njaa?
 
Wewe chura FC ukishajua itakusaidia nn?? Cc wanasimba ata akitoa jero tunaomba apewe timu yote aimiliki na akipenda abadilishe na jina iwe Mo FC muhimu mashabiki tunapata FURAHA timu inafanya maajabu basi tunafurahi ayo mengine ni kukompliketi mambo mwaisa
Ikibadilishwa jina ikiitwa Mo FC hawa washabiki wa Simba hutawaona hapa
 
Mo tapeli Tu na sitashangaa Simba ikimshinda
Alishindwa Singida united akakimbia
Akashindwa Africa Lyon akakimbia..

Ana usanii mwingi
Hayo maswali watu wengi wanauliza..
Kubandika bidhaa zake .. kwenye magari na kesi..je Simba walitangaza bid?
Kampuni yake ndo highest bidder?
Au analazimisha kwa bei anayotaka?

Maswali mengi kuliko majibu

Tunataka tukupe wewe hiyo Simba usiyrkuwa tapeli, unaweka kiasi gani na mipango yako kuhusu Simba imekaaje? Ama ni wivu tu wa kike unakusumbua?
 
Back
Top Bottom