Aliyeng'atwa na Nyoka afia Kituo cha Afya kisa hana 150,000 Wilayani Babati

Aliyeng'atwa na Nyoka afia Kituo cha Afya kisa hana 150,000 Wilayani Babati

Mkuu kuweni making na hizi dhana zisizo na ushahidi wa kisayansi.Kuna Watu wanafanya triki tu za kucheza na Nyoka wenye sumu hafifu isiyo hatari kwa biinaadamu au wasio na sumu kabisa mfano Chatu n.k.Tusiwe wepesi wa kuamini jambo Watu wachache tu na kuishia hapo,uwezo wa kuhimili sumu si lingekuwa jambo la Dunia yote ama?Hivi ni Wanasayansi gani wasingependa kumjua Mtu anayehimili sumu kali ya Nyoka au sumu yoyote ile?.Huko kwa Wenzetu kuna Watu wanafanya kazi kwenye maabara zenye aina tofauti karibia elfu moja ya Nyoka na wanachukua tahadhari zote iwapo itatoka akali ya kuchongea nao.
Mzee,
Kua uyaone....tembea ujionee.. mwezi wa 8 mwaka huu tulimpoteza ba mkubwa so tulisafir kwenda msibani kilicho tokea ni kua tukiwa kwenye kikao Cha familia ghafla nyoka mkubwa akaja mbio akakatiza mbele kiasi kikao kila mtu akakimbia na wengine sisi wanaume kubeba fumbo na mawe.

Kaka akatukataza kumpiga na kumponda mawe akamwita jamaa mkamata majoka na kuyafuga yeye na familia yao wakamkamata kwa mikono na kumchukua..

Wanakua na dawa za kuwapumbaza majoka

Hizi sio hekaya ama story za alfa ulela ulela 😅
 

KATIKA hali ya kusikitisha, mkazi wa Magugu, Wilaya ya Babati, Juliana Obedy (44), amepoteza maisha baada ya wataalamu katika Kituo cha Afya Magugu, kudaiwa kumcheleweshea huduma kituoni hapo kutokana na kugongwa na nyoka.

Imedaiwa kuwa, sababu za kucheleweshwa kwa huduma hiyo ni wataalamu kutaka kulipwa Sh. 150,000 ikiwa ni gharama za matibabu.

Akisimulia mkasa huo jana, mume wa Juliana, Obedy Laizer, alisema Desemba 16, mwaka huu, akiwa anavunja jengo la Kanisa la Katoliki Magugu, mke wake alipita akiwa anachuma mboga za majani na kung'atwa na nyoka ambaye hakujua ni wa aina gani.

Laizer alisema baada ya muda mfupi mke wake kuondoka, alikuja mtoto wake na kumwambia anaitwa na mama yake ambaye alidai kung'atwa na nyoka, ndipo alipokimbia kumpeleka Kituo cha Afya Magugu.

Alipomfikisha kituoni hapo kulikuwa na foleni na kushauriana na mke wake waingie ndani na kujisajili, lakini wauguzi waliwaambia kuwa daktari alikuwa chumba cha wazazi na kuomba apigiwe simu ili kuja kumsaidia.

"Daktari alipigiwa simu mara ya kwanza hakupokea, akapigiwa simu mara ya pili ndipo alipopokea akasema anakuja na alitoa huduma na mgonjwa kuandikiwa dawa," alisema Laizer.

Hata hivyo, alisema alipoenda duka la dawa aliambiwa anatakiwa kulipia Sh. 150,000 ambapo Laizer aliomba mgonjwa ahudumiwe na fedha itafuata, lakini wauguzi wawili na daktari mmoja waliokuwapo hawakukubali na kuamua kumpigia Mganga Mfawidhi simu na kujibiwa kuwa anatakiwa alipie Sh. 150,000 na kukata simu.

Laizer alisema baada ya kuvutana na wataalamu hao alitoka na kwenda kutafuta fedha aliporudi alitoa Sh. 130,000 na badala ya kuanza kutoa huduma, wataalamu hao walianza kupigiana simu ndipo mmoja alisikika akisema mgonjwa ahudumiwe.

Aidha, alisema baada ya kulipia fedha hiyo muuguzi anayehusika na dawa alimpeleka duka la dawa na kumpatia na walirudi kwa mgonjwa ambako alifukuzwa wodini, lakini aligoma akitaka kushuhudia mke wake akihudumiwa.

Alisema mgonjwa aliulizwa anajisikiaje naye akajibu kuwa anajisikia vibaya huku akisema “Bwana Yesu nisaidie” ghafla aliacha kuongea na ndugu na majirani waliokuwapo walianza kumwombea kwa kushirikiana naye bila mafanikio.

Alisema baada ya mke wake kukata kauli wauguzi waliendelea kumchua na kumwekea oksijen, lakini alipoona haisaidii aliwaambia waitoe.

"Baada ya kuona hivyo niliwaambia mke wangu ndio anaondoka hivyo, tulienda duka la dawa wakanipa dawa ya Sh. 6000 ya kumpunguzia maumivu na sikupewa risiti, wala ile ya 150,000 sikupewa," alisema.

Akiongea kwa uchungu alisema licha ya kuwaomba aweke rehani pikipiki yake na kuwapa funguo wauguzi ili wamhudumie mke wake waligoma na kudai akikimbia wao ndio wanawajibika.

Mtoto wa marehemu, Abednego Obedy, alisema mama yake alimwonesha mkono ukiwa umevimba na kumwambia ameng'atwa na nyoka na kumshauri kwenda kituo cha afya.

Aidha, Enoti Philipo ambaye alikuwa akimwita marehemu shangazi, alisema alitoka nyumbani kwake kuchuma mboga za majani na baadaye aliona mume wake anamkimbiza hospitali.

Mkazi wa kijiji hicho, Yona Laizer, alisema kitendo kilichofanywa na wataalamu hao ni uzembe na unyama ambao kama wakiendelea watasababisha vifo vingi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Magugu, Lohay Amos, alilaani tukio hilo na kuwataka wauguzi na madaktari kutii viapo vyao.

Akizungumzia tukio hilo kwa njia ya simu Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Magugu, Dk. Kusta Ndunguru, alikiri kupigiwa simu na Laizer huku akisema alijua anathibitisha malipo aliyoambiwa.

Dk. Ndunguru alisema alimwambia aongee na wataalamu waliopo hospitali ili wamsaidie kwa kuwa yeye yuko nje ya kituo na hakumrudia.

Alisema mtu aking'atwa na nyoka mwenye sumu kali haitakiwi kuzidi nusu saa kwasababu ikizidi anapoteza maisha ndio maana alimwambia awaeleze wataalamu ili wamsaidie asipoteze muda.

Chanzo: Nipashe
...Hivi hao Wasaidizi na Dakitari Mkuu Wao Bado Wako Kazini ?? WanatakiwaMgonjwa alipofariki Kwa Kujizungusha kwao, Hapo Hapo wanatakiwa Kuchapa Lapa'!
Yaani Binadamu mwenzetu afariki Kukosa Dawa Kwa Sababu haba Shs 150, 000/ - ??
Hivi Dawa ya Kuumwa na Nyoka ni Shs Laki Moja na Nusu ??
Na ule utaratibu ahudumiwe kwanza kama Hana Hela Umeishia wapi ?
Huyo Dakitari Mkuu Kwa Nini amuambie Mume wa Marehemu awaambie Wasaidizi wamsaidie Marehemu Badala ya Kuwaambia yeye ??? R.I.P Mama Mpendwa. Yana Mwisho Haya..
 
Hivi unajua ni watu wangapi wanaokuja na excuse za kwamba hawana pesa? Ungekuwa ww ndio mtumishi wa level za chini unadhani ungeonea huruma wangapi ? Na ukumbuke hasara yoyote unayoitengeneza ww ndiyo utalipa.

Huyo Mganga Mfawidhi hawezi kuondoka kituoni bila ku-delegate mamlaka, kwa nini yeye mwenyewe hakuchukua jukumu la kumpigia yule alomkaimisha ampe maelekezo ya nini cha kufanya, unaposema nenda tu wakusaidie maana yake nini?

Ni kweli kwenye hospitali za umma kuna utaratibu wa msamaha wa muda mfupi na mrefu, lkn anayetoa hiyo misamaha ni Waganga Wafawidhi wenyewe, hivyo bado tunarudi palepaleee...

Na ukumbuke nimekuambia ktk dawa ambayo huwa iko strict kwenye kutolewa ovyo ovyo ni hizo ANTI-VENOM, na nimekuambia utaratibu uliopo ni PRE-PAID.
...Wanakujia Wangapi ambao Wameumwa na Nyoka, na Wako Hatarini Kupoteza Maisha ??
 

KATIKA hali ya kusikitisha, mkazi wa Magugu, Wilaya ya Babati, Juliana Obedy (44), amepoteza maisha baada ya wataalamu katika Kituo cha Afya Magugu, kudaiwa kumcheleweshea huduma kituoni hapo kutokana na kugongwa na nyoka.

Imedaiwa kuwa, sababu za kucheleweshwa kwa huduma hiyo ni wataalamu kutaka kulipwa Sh. 150,000 ikiwa ni gharama za matibabu.

Akisimulia mkasa huo jana, mume wa Juliana, Obedy Laizer, alisema Desemba 16, mwaka huu, akiwa anavunja jengo la Kanisa la Katoliki Magugu, mke wake alipita akiwa anachuma mboga za majani na kung'atwa na nyoka ambaye hakujua ni wa aina gani.

Laizer alisema baada ya muda mfupi mke wake kuondoka, alikuja mtoto wake na kumwambia anaitwa na mama yake ambaye alidai kung'atwa na nyoka, ndipo alipokimbia kumpeleka Kituo cha Afya Magugu.

Alipomfikisha kituoni hapo kulikuwa na foleni na kushauriana na mke wake waingie ndani na kujisajili, lakini wauguzi waliwaambia kuwa daktari alikuwa chumba cha wazazi na kuomba apigiwe simu ili kuja kumsaidia.

"Daktari alipigiwa simu mara ya kwanza hakupokea, akapigiwa simu mara ya pili ndipo alipopokea akasema anakuja na alitoa huduma na mgonjwa kuandikiwa dawa," alisema Laizer.

Hata hivyo, alisema alipoenda duka la dawa aliambiwa anatakiwa kulipia Sh. 150,000 ambapo Laizer aliomba mgonjwa ahudumiwe na fedha itafuata, lakini wauguzi wawili na daktari mmoja waliokuwapo hawakukubali na kuamua kumpigia Mganga Mfawidhi simu na kujibiwa kuwa anatakiwa alipie Sh. 150,000 na kukata simu.

Laizer alisema baada ya kuvutana na wataalamu hao alitoka na kwenda kutafuta fedha aliporudi alitoa Sh. 130,000 na badala ya kuanza kutoa huduma, wataalamu hao walianza kupigiana simu ndipo mmoja alisikika akisema mgonjwa ahudumiwe.

Aidha, alisema baada ya kulipia fedha hiyo muuguzi anayehusika na dawa alimpeleka duka la dawa na kumpatia na walirudi kwa mgonjwa ambako alifukuzwa wodini, lakini aligoma akitaka kushuhudia mke wake akihudumiwa.

Alisema mgonjwa aliulizwa anajisikiaje naye akajibu kuwa anajisikia vibaya huku akisema “Bwana Yesu nisaidie” ghafla aliacha kuongea na ndugu na majirani waliokuwapo walianza kumwombea kwa kushirikiana naye bila mafanikio.

Alisema baada ya mke wake kukata kauli wauguzi waliendelea kumchua na kumwekea oksijen, lakini alipoona haisaidii aliwaambia waitoe.

"Baada ya kuona hivyo niliwaambia mke wangu ndio anaondoka hivyo, tulienda duka la dawa wakanipa dawa ya Sh. 6000 ya kumpunguzia maumivu na sikupewa risiti, wala ile ya 150,000 sikupewa," alisema.

Akiongea kwa uchungu alisema licha ya kuwaomba aweke rehani pikipiki yake na kuwapa funguo wauguzi ili wamhudumie mke wake waligoma na kudai akikimbia wao ndio wanawajibika.

Mtoto wa marehemu, Abednego Obedy, alisema mama yake alimwonesha mkono ukiwa umevimba na kumwambia ameng'atwa na nyoka na kumshauri kwenda kituo cha afya.

Aidha, Enoti Philipo ambaye alikuwa akimwita marehemu shangazi, alisema alitoka nyumbani kwake kuchuma mboga za majani na baadaye aliona mume wake anamkimbiza hospitali.

Mkazi wa kijiji hicho, Yona Laizer, alisema kitendo kilichofanywa na wataalamu hao ni uzembe na unyama ambao kama wakiendelea watasababisha vifo vingi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Magugu, Lohay Amos, alilaani tukio hilo na kuwataka wauguzi na madaktari kutii viapo vyao.

Akizungumzia tukio hilo kwa njia ya simu Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Magugu, Dk. Kusta Ndunguru, alikiri kupigiwa simu na Laizer huku akisema alijua anathibitisha malipo aliyoambiwa.

Dk. Ndunguru alisema alimwambia aongee na wataalamu waliopo hospitali ili wamsaidie kwa kuwa yeye yuko nje ya kituo na hakumrudia.

Alisema mtu aking'atwa na nyoka mwenye sumu kali haitakiwi kuzidi nusu saa kwasababu ikizidi anapoteza maisha ndio maana alimwambia awaeleze wataalamu ili wamsaidie asipoteze muda.

Chanzo: Nipashe
Goli la Mama 5 Million
 
Mbona mnawasema waajiriwa ikiwa wanapewa maagizo na boss wao.

Wapo pale wameambiwa ukitoa ugonjwa huu na huu basi wengine wote watoe hela basi ndy utaratibu upo hvyo.

Sasa tatzo lipo mbali sio kama mnavyo liona
.
 
Naona wahudumu wanashambuliwa sana humu, na nimesikia kuna waliosimamishwa kazi.

Lakini haya yote ni matokeo ya kuendekeza siasa kwenye kila jambo nchi hii. Wanasiasa badala ya kuwekeza kwenye uundaji na utekelezaji wa sera nzuri hasa katika sekta nyeti ikiwemo hiyo ya afya (ikiwemo kupunguza gharama za matibabu na kurahisisha upatikanaji wa vifaatiba), wamewekeza kwenye kukurupuka na maamuzi ya mizuka tu.

Ninaamini kama hao wahudumu wangeamua kutoa huduma kinyume na utaratibu kulinda uhai wa mgonjwa na akapona hata wasingeonekana mashujaa kwani hata wazo la kuwa wameokoa uhai wa mtu lisingekuwepo. Na kama mwenye mgonjwa angeingia mitini ushujaa wao ungegeuka ujuha na wangeishia kuonekana wa ajabu na kuchukuliwa hatua na walewale wazee wa mikurupuko ya kisiasa.

Tatizo kuu hapo ni mifumo, then wahudumu wanafuata baadaye.
 
Nilisoma sehemu kwamba watoa huduma wamesimamishwa ila kiukweli anayetakiwa kuwajibika ni mganga mfawidhi.

Mwananchi inaonyesha alikaa muda mkubwa nyumbani kabla ya kwenda hospitali hii ni kwakua sumu ya nyoka haiui kwa short time kiasi hicho, mpaka mkono kuvimba.

Hiki kifo kilikua kinaweza kuzuilika
 
Back
Top Bottom