Aliyeng'atwa na Nyoka afia Kituo cha Afya kisa hana 150,000 Wilayani Babati

Aliyeng'atwa na Nyoka afia Kituo cha Afya kisa hana 150,000 Wilayani Babati

Pikipiki tu ilikuwa ni hela tosha ya kumtibia huyo mgonjwa
Bado kuna wajinga wanaamini kuwa serikali ya CCM inawapenda wananchi wake😀😀😀😀 Utashangaa viongozi wa CCM wanagharamia msiba kwa mamilion ya hela wakati 150k ilikuwa inatosha kumtibia.
Kwasasa hapa duniani mambo yaliyopewa kipaumbele
1. Pesa
2. Ngono
3. Pombe
4. Sigara / Bangi / shisha, cocaine n.k
5. Kamari
Sasa hivi pesa ina thamani sana kuliko uhai na ni rahisi sana kupata ngono kuliko chakula
ni u jinga wa hali ya juu kuisingizia ccm kwa hili hao wauguzi unajuwaje kama ni ccm au chadema? wachukuliwe hatua kali sana siyo kukaa na kuilaumu ccm mingine michadema iliyoishiwa hoja inauwa watu makusudi ili isingiziwe ccm
 
Eeh Mungu wangu hiki ni nini jamani mbn inasikitisha mno mtu kashasema kangatwa na nyoka badala ya kuangaza kuhangaika kumsaidia mambo mengine yafuate inaangaliwa kwanza hela ndio ahudumiwe mwisho wa siku kafa.Nyinyi madaktari huko chuo mmefundishwa kuzoea kifo au kuokoa watu wanaokufa.Sasa amekufa andaeni cheti cha kifo sababu hicho ndicho mlichokuws mnakitaka.HII NI AIBU KWA MADAKTARI NA WAUGUZI
 
Watumishi wa afya hawana makosa .

Ya kulaumiwa ni serikali, mifumo yao ya uendeshaji ni mibovu na lawama huwa wanawaachia watumishi .
Sio kweli ,uyo mpaka anafika pale sio mkazi wa mbali na eneo husika , yani katika emergency ya mgojwa unatanguliza pesa kwanza ayo ndo maelekezo ya serikali katika vituo vya kutolea huduma? Mfano mtu amepata jeraha anableed na unaona is life threatening so unaanza pambana na pesa au kumuweka sawa mgonjwa then pesa ?

Mengine watumishi wabovu wanaifanya Serikali kubeba lawama bila sababu, mfano kuna vituo vya afya wakati serikali inasema mama mjazito ,watoto chini ya miaka 5 ni bure , wao huwatoza pesa kisa eti wanakusanya mapato ,je hapa serikali inalaumiwa kwa lipi ili hali mwongozo upo wazi?

DMO wapo ,wakurugenzi wapo, madiwani wapo,wabunge wapo, wakuu wa wilaya wapo.
 
Hao wauguzi na madaktari uwakute Jumapili au Ijumaa kwenye makanisa na misikiti yao wakisali wapo mbele kabisa.Njoo huku uone wanachofanya mtu anakata roho wanaangalia hivi na hamna anayeshtuka.Hamkupaswa kupewa hizo nafasi sababu daktari au muuguzi ni mtu wa kuokoa maisha ya watu Ila Tanzania ni kinyume chake!
 
Eeh Mungu wangu hiki ni nini jamani mbn inasikitisha mno mtu kashasema kangatwa na nyoka badala ya kuangaza kuhangaika kumsaidia mambo mengine yafuate inaangaliwa kwanza hela ndio ahudumiwe mwisho wa siku kafa.Nyinyi madaktari huko chuo mmefundishwa kuzoea kifo au kuokoa watu wanaokufa.Sasa amekufa andaeni cheti cha kifo sababu hicho ndicho mlichokuws mnakitaka.HII NI AIBU KWA MADAKTARI NA WAUGUZI
Mkuu madaktari wengi wanajitambua , ni hivi vidactari vya sasa vinavyoingia kwenye ajira mpya ndo vinaaribu ,vinaamini kauli yao katika kusimamia vituo ndo kauli ya mwisho
 

KATIKA hali ya kusikitisha, mkazi wa Magugu, Wilaya ya Babati, Juliana Obedy (44), amepoteza maisha baada ya wataalamu katika Kituo cha Afya Magugu, kudaiwa kumcheleweshea huduma kituoni hapo kutokana na kugongwa na nyoka.

Imedaiwa kuwa, sababu za kucheleweshwa kwa huduma hiyo ni wataalamu kutaka kulipwa Sh. 150,000 ikiwa ni gharama za matibabu.

Akisimulia mkasa huo jana, mume wa Juliana, Obedy Laizer, alisema Desemba 16, mwaka huu, akiwa anavunja jengo la Kanisa la Katoliki Magugu, mke wake alipita akiwa anachuma mboga za majani na kung'atwa na nyoka ambaye hakujua ni wa aina gani.

Laizer alisema baada ya muda mfupi mke wake kuondoka, alikuja mtoto wake na kumwambia anaitwa na mama yake ambaye alidai kung'atwa na nyoka, ndipo alipokimbia kumpeleka Kituo cha Afya Magugu.

Alipomfikisha kituoni hapo kulikuwa na foleni na kushauriana na mke wake waingie ndani na kujisajili, lakini wauguzi waliwaambia kuwa daktari alikuwa chumba cha wazazi na kuomba apigiwe simu ili kuja kumsaidia.

"Daktari alipigiwa simu mara ya kwanza hakupokea, akapigiwa simu mara ya pili ndipo alipopokea akasema anakuja na alitoa huduma na mgonjwa kuandikiwa dawa," alisema Laizer.

Hata hivyo, alisema alipoenda duka la dawa aliambiwa anatakiwa kulipia Sh. 150,000 ambapo Laizer aliomba mgonjwa ahudumiwe na fedha itafuata, lakini wauguzi wawili na daktari mmoja waliokuwapo hawakukubali na kuamua kumpigia Mganga Mfawidhi simu na kujibiwa kuwa anatakiwa alipie Sh. 150,000 na kukata simu.

Laizer alisema baada ya kuvutana na wataalamu hao alitoka na kwenda kutafuta fedha aliporudi alitoa Sh. 130,000 na badala ya kuanza kutoa huduma, wataalamu hao walianza kupigiana simu ndipo mmoja alisikika akisema mgonjwa ahudumiwe.

Aidha, alisema baada ya kulipia fedha hiyo muuguzi anayehusika na dawa alimpeleka duka la dawa na kumpatia na walirudi kwa mgonjwa ambako alifukuzwa wodini, lakini aligoma akitaka kushuhudia mke wake akihudumiwa.

Alisema mgonjwa aliulizwa anajisikiaje naye akajibu kuwa anajisikia vibaya huku akisema “Bwana Yesu nisaidie” ghafla aliacha kuongea na ndugu na majirani waliokuwapo walianza kumwombea kwa kushirikiana naye bila mafanikio.

Alisema baada ya mke wake kukata kauli wauguzi waliendelea kumchua na kumwekea oksijen, lakini alipoona haisaidii aliwaambia waitoe.

"Baada ya kuona hivyo niliwaambia mke wangu ndio anaondoka hivyo, tulienda duka la dawa wakanipa dawa ya Sh. 6000 ya kumpunguzia maumivu na sikupewa risiti, wala ile ya 150,000 sikupewa," alisema.

Akiongea kwa uchungu alisema licha ya kuwaomba aweke rehani pikipiki yake na kuwapa funguo wauguzi ili wamhudumie mke wake waligoma na kudai akikimbia wao ndio wanawajibika.

Mtoto wa marehemu, Abednego Obedy, alisema mama yake alimwonesha mkono ukiwa umevimba na kumwambia ameng'atwa na nyoka na kumshauri kwenda kituo cha afya.

Aidha, Enoti Philipo ambaye alikuwa akimwita marehemu shangazi, alisema alitoka nyumbani kwake kuchuma mboga za majani na baadaye aliona mume wake anamkimbiza hospitali.

Mkazi wa kijiji hicho, Yona Laizer, alisema kitendo kilichofanywa na wataalamu hao ni uzembe na unyama ambao kama wakiendelea watasababisha vifo vingi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Magugu, Lohay Amos, alilaani tukio hilo na kuwataka wauguzi na madaktari kutii viapo vyao.

Akizungumzia tukio hilo kwa njia ya simu Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Magugu, Dk. Kusta Ndunguru, alikiri kupigiwa simu na Laizer huku akisema alijua anathibitisha malipo aliyoambiwa.

Dk. Ndunguru alisema alimwambia aongee na wataalamu waliopo hospitali ili wamsaidie kwa kuwa yeye yuko nje ya kituo na hakumrudia.

Alisema mtu aking'atwa na nyoka mwenye sumu kali haitakiwi kuzidi nusu saa kwasababu ikizidi anapoteza maisha ndio maana alimwambia awaeleze wataalamu ili wamsaidie asipoteze muda.

Chanzo: Nipashe
Na wahusika hawatachukuliwa hatua yeyote licha ya kusababisha kifo cha mtu.
 
Ha
Hiyo ni kazi kama kazi zingine .Mnahimizwa sana muwe na bima ya afya ila hamzingatii.

Wewe hapo unapofanya kazi unaweza kumuhudumia mtu bure?
Hakuna mwongozo wowote wa serikali unaosema kwamba mgonjwa wa emergency ukimbizane na pesa katika vituo vya umma, ndo maana hata leo akiokotwa mtu amepata ajali na hana ndugu, atatibiwa Mengine yatajulikana badae
 
Mno especially government hospital watu wanateseka sana,mi niliwahi kugombana na mhudumu mmoja tena sikutaka kuyakuza,pamoja na hayo kuna wahudumu wanaipenda kazi yao.
Hawa form four failure wengi ni tatizo
Hakuna cha form four hapa, huduma ya afya imetoka mbali, unajua mwanzo wahudum wa afya wengi walikua la 7, unajua AMO ndo walikua maincharge kwenye hospital za mikoa na wilaya, unajua Co ndo walikua incharge kwenye vituo vya afya kabla , na je huduma zilikua zinaenda au haziendi .

Kishimba ni Mbunge na ni la saba ila anaakili kuliko maprof unajua hilo.

Msukuma ni mbunge na la saba ila yupo na akili kuliko wenye PhD zao apo Bungeni
 
Kuna watu wanaitwa maboss huko maofisini, Hawa ndio chanzo Cha uharibifu, vikao vyao na watumishi ni vitisho, kuvishana hofu na kutetemeshana, hili linasababisha watumishi wa chini kutokutumia akili na utu sababu mda mwingi Wana hofu
Kutojielewa sheria na kanuni za utumishi wa umma zipo pale ,sasa unatetemeka nini, Daktari we si umeapa kutoa huduma kwa wagonjwa bila upendeleo ,sasa hofu ya nini ili hali ulichofanya ni ethical tokana na taaluma yako ,hofu ya nini kama sio uzwazwa
 
Mkuu, kuna baadhi ya protocols huko utumishi wa umma huwa ni ngumu sana kwa wafanyakazi wa chini.

Hapana lawama zote zinaenda kwa MGANGA MFAWIDHI.

Case kama hii yeye ndiyo anapaswa atoe go ahead ili wale wa chini waweze kutoa hiyo dawa.

Anaposema yuko mbali, wale walioko kazini ndiyo wafanye maamuzi ni anawauzia msala ambao yeye ndiyo anapaswa ausovu.
As for me,still naona hii theory kwenye suala la afya ya mtu haiingii akilini na wa kulaumiwa bado ni hao waliokuwa eneo la tukio hata ukisoma maelezo ya mganga mkuu anasema mtu akiumwa na nyoka mkali anatakiwa atibiwe haraka so yeye hakuwepo hata kama ndiye alitoa amri matibabu yasifanyike mpaka pesa ilipwe inabidi waliokuwepo watoe huduma sababu wao ndiyo walikuwa wanaona mabadiliko ya mgonjwa hatua kwa hatua.

Labda ingekuwa ni private hospital lakini kwenye hospital za serikali huwa kunakuwa na msamaha wa matibabu pale mgonjwa ameshindwa kulipa bill yake kwanini huyu asingetibiwa maisha yake yaokolewe then pikipiki izuiwe ikija kutokea utata baadae aingizwe kwenye program ya msamaha?tunarudi pale pale kwamba hao waliokuwepo hawana wito wa udaktari yaani kabisa mnamuona mtu anakaribia kukata roho mbele yenu nyie bado mnakaza lete hela lete hela?

Watu huruma hawana kabisa yani mke wa mtu mzazi wa mtu anayetegemewa anakata roho mbele yenu nyie mnamtizama tu?wakati dawa zipo na siyo zenu?na mmepewa bond ya pikipiki ya approximately 800K hata angetokea mmoja akawa dhamana akachukua yeye pikipiki huyo mama akatibiwa,umaskini m'baya sana na unakuwa m'baya zaidi ukikutana na watu wenye ufinyu wa kufikiria na roho mbaya.
 
Kutojielewa sheria na kanuni za utumishi wa umma zipo pale ,sasa unatetemeka nini, Daktari we si umeapa kutoa huduma kwa wagonjwa bila upendeleo ,sasa hofu ya nini ili hali ulichofanya ni ethical tokana na taaluma yako ,hofu ya nini kama sio uzwazwa
Hujui wa Tz wengi ni mazwazwa!?,,,

Hizo ethics unazizungumzia zipo Kila mahali , lakini utekelezaji wake ukoje!?

Mara ngapi umesikia simu Toka juu zimebatilisha hukumu mahakamani,Sheria barabarani, vibari vya umiliki wa rasilimali nk ,na ethics zipo wazi!?
 
Siku moja miaka mingi iliyopita jioni tukiwa makazi mapya ndio tumehamia nikatoka nje niende dukani kununua vocha.

Nikitembea gizani nikakanyaga nyoka akaning'ata kwenye vidole viwili vya miguu kumulika anatokomea vichakani..

Nilitoka mbio mpaka nyumbani sebureni nikamkuta shangazi, mama yangu mzazi na ndugu zangu wengine wakaanza kunipa first aid

Shangazi akasema yeye pia aliwai kun'gatwa na nyoka hivyo aitwe mmama mmoja jirani aje kunitibu ilikua ni jumapili..akaenda kuitwa akaja akachukua wembe kunichana kidogo kwenye jeraha akaenda nje akaja na mizizi akaniambia nitafune nimeze maji yake then nilipo Tena akachanganya na majani kisha akabandika mguuni..

Akasema Kama ni nyoka wa kawaida umepona Kama ni vice versa Sito ponaa Akaondoka.

Nikalala usiku kwa hofu maana sikujua Yale majani TU yanitibu haaahaa nilipona ☺️😊

From Rock City Mwanza.
Huwa pia inategemea ni aina gani ya Nyoka amekugonga maana sio Nyoka wote wana sumu, na hata wale wenye sumu huweza kugonga bila kuachia sumu(dry bite).Ila kwa huduma ya kwanza iliyotolewa inaonesha huyo ni mjuzi maana kuwahi jeraha na kufanya damu itoke inaweza kupunguza kiwango cha sumu..ila kama nilivyosema inategemea na aina ya Nyoka..ila alitakiwa amalize kwa kuwashauri pia muende Hospitali.
 
Kwa Tabora, koboko atakuuwa kama umechelewa sana kwa mtaalamu...

Tena huwa wanaangalia nywele, koboko akikuuma baada ya mda flani ukivutwa nywele huwa zinang'oka...

Ikifika hali hiyo, inakua ngumu kukutibu...

Japo hao wazee wanakufaga na utaalamu wao.
Mimi nimeelezea ushuhuda wangu kung'atwa na nyoka. Japo wengine wananibishia.

Kutibiwa kwa kutafuna mizizi ya mti nilio pewa na mtaalamu na kukamuliwa juice ya majani Fulani na kubandikwa majani kwenye jeraha la nyoka.

Na mpaka Leo na dunda.
 
Hahaha naufahamu mzima ila sikujua kuhusu hili...

Kuhusu dawa za nyoka ni kweli zipo, maeneo yale mtu akiumwa nyoka haendi hospitali.
Baba yangu mkubwa alipenda kuniambia kua HII MITI INAONGEA.

YAANI AKIWA NA MAANA MITI HUWAGA INAONGEA.

Huko usukumani Kuna mpaka wakamata nyoka na kucheza nao nyoka wanapumbazwa..

Baadae ntatoa kisa Cha bro mmoja alichanjia dawa yaan hata nyoka akimuuma hapati madhara kwa macho yangu NILISHUHUDIA kwenye parking tukifanya usafi akang'atwa na nyoka mkubwa mweusi
 
Mkuu kuweni making na hizi dhana zisizo na ushahidi wa kisayansi.Kuna Watu wanafanya triki tu za kucheza na Nyoka wenye sumu hafifu isiyo hatari kwa biinaadamu au wasio na sumu kabisa mfano Chatu n.k.Tusiwe wepesi wa kuamini jambo Watu wachache tu na kuishia hapo,uwezo wa kuhimili sumu si lingekuwa jambo la Dunia yote ama?Hivi ni Wanasayansi gani wasingependa kumjua Mtu anayehimili sumu kali ya Nyoka au sumu yoyote ile?.Huko kwa Wenzetu kuna Watu wanafanya kazi kwenye maabara zenye aina tofauti karibia elfu moja ya Nyoka na wanachukua tahadhari zote iwapo itatoka akali ya kuchongea nao.
Baba yangu mkubwa alipenda kuniambia kua HII MITI INAONGEA.

YAANI AKIWA NA MAANA MITI HUWAGA INAONGEA.

Huko usukumani Kuna mpaka wakamata nyoka na kucheza nao nyoka wanapumbazwa..

Baadae ntatoa kisa Cha bro mmoja alichanjia dawa yaan hata nyoka akimuuma hapati madhara kwa macho yangu NILISHUHUDIA kwenye parking tukifanya usafi akang'atwa na nyoka mkubwa mweusi
 
Sijui kama hiyo dawa ilikuwepo hapoo kwa level ya kituo cha afya ukute hata friji hawanaa labda walitaji pesa kwanza wakanunue ndipo achomwe so kwa mazingira hayo lawama ni za bureee ubaya kama hiyo dawa ilikuwepo hivyo vituo hata petty cash ya dharura huwa hawanaa.
 
Kutojielewa sheria na kanuni za utumishi wa umma zipo pale ,sasa unatetemeka nini, Daktari we si umeapa kutoa huduma kwa wagonjwa bila upendeleo ,sasa hofu ya nini ili hali ulichofanya ni ethical tokana na taaluma yako ,hofu ya nini kama sio uzwazwa
Unadhani dawa kwenye famasi zinatoka kama nyanya??? kesho ndo mtu akikaguliwa anaambiwa ni mwiziii wa dawa.
 
As for me,still naona hii theory kwenye suala la afya ya mtu haiingii akilini na wa kulaumiwa bado ni hao waliokuwa eneo la tukio hata ukisoma maelezo ya mganga mkuu anasema mtu akiumwa na nyoka mkali anatakiwa atibiwe haraka so yeye hakuwepo hata kama ndiye alitoa amri matibabu yasifanyike mpaka pesa ilipwe inabidi waliokuwepo watoe huduma sababu wao ndiyo walikuwa wanaona mabadiliko ya mgonjwa hatua kwa hatua.

Labda ingekuwa ni private hospital lakini kwenye hospital za serikali huwa kunakuwa na msamaha wa matibabu pale mgonjwa ameshindwa kulipa bill yake kwanini huyu asingetibiwa maisha yake yaokolewe then pikipiki izuiwe ikija kutokea utata baadae aingizwe kwenye program ya msamaha?tunarudi pale pale kwamba hao waliokuwepo hawana wito wa udaktari yaani kabisa mnamuona mtu anakaribia kukata roho mbele yenu nyie bado mnakaza lete hela lete hela?

Watu huruma hawana kabisa yani mke wa mtu mzazi wa mtu anayetegemewa anakata roho mbele yenu nyie mnamtizama tu?wakati dawa zipo na siyo zenu?na mmepewa bond ya pikipiki ya approximately 800K hata angetokea mmoja akawa dhamana akachukua yeye pikipiki huyo mama akatibiwa,umaskini m'baya sana na unakuwa m'baya zaidi ukikutana na watu wenye ufinyu wa kufikiria na roho mbaya.
Hivi unajua ni watu wangapi wanaokuja na excuse za kwamba hawana pesa? Ungekuwa ww ndio mtumishi wa level za chini unadhani ungeonea huruma wangapi ? Na ukumbuke hasara yoyote unayoitengeneza ww ndiyo utalipa.

Huyo Mganga Mfawidhi hawezi kuondoka kituoni bila ku-delegate mamlaka, kwa nini yeye mwenyewe hakuchukua jukumu la kumpigia yule alomkaimisha ampe maelekezo ya nini cha kufanya, unaposema nenda tu wakusaidie maana yake nini?

Ni kweli kwenye hospitali za umma kuna utaratibu wa msamaha wa muda mfupi na mrefu, lkn anayetoa hiyo misamaha ni Waganga Wafawidhi wenyewe, hivyo bado tunarudi palepaleee...

Na ukumbuke nimekuambia ktk dawa ambayo huwa iko strict kwenye kutolewa ovyo ovyo ni hizo ANTI-VENOM, na nimekuambia utaratibu uliopo ni PRE-PAID.
 
Back
Top Bottom