Elections 2010 Aliyetuhumiwa Kumtukana Kikwete sasa Kugombea jimbo la Musoma Vijijini.......

watu wamesafiri kuja kukuomba ugombee....wengine wamekupigia simu........hakika wametumia pesa na rasilimali nyngi tu......sasa wewe lini unakwenda kule.........halafu kama wewe ni mzaliwa wa kule kwa nini hukugombea kule mwaka jana?.......una mikakati gani katika kipindi hiki mpaka kufikia 2015?........

kingine wengi hawana access na internet huko...wewe unatangaza rasmi hapa! je umeshawataarifu hao wananchi wako huko musoma vijijini?

la mwisho badilisha avata yako............
 
Niiwekeje ndugu yangu....Naomba msaada wako..

kwa uwezo wako wa kufikiri na nafasi unayoomba kwa wananchi wa Musoma vijijini unaona heading hiyo inafaa??
 
kwa uwezo wako wa kufikiri na nafasi unayoomba kwa wananchi wa Musoma vijijini unaona heading hiyo inafaa??

Kaka uwezo wangu wa kufikiri ni mdogo sana na ndo maana nimekuomba kwa nia njema kabisa kuwa unisaidie ili niandike inayofaa...Au nimekosea kukuomba msaada!Maana kwa uwezo wangu mdogo naweza kuandika mbaya zaid so naomba msaada wako ndugu yangu..
 
Ndugu yangu, wewe umeisha tangaza nia wewe nenda kagombee. kama akijitokeza mwingine basi kura ndani ya chama zitaamua. Hata mimi naweza kutangaza kuwa ninakuja hukohuko msoma vijijini kwani kunashida gani mtu akitangaza nia jamani? Acha CDM iende mbele. Temeke atajitokeza mwingine.
 

Hao walionipigia simu walipata namba zangu humu humu coz niliziweka wazi so nimewajulisha
...Ninajiandaa soon ninakwenda coz ndo nimetoka kwa msiba wa kufiwa ba baba mazazi so napumzika kidogo..Niligombea Temeke coz ni mkazi wa Temeke..
 
Assume wewe ni mbunge tayari . jimbo lako linapata mfuko ya jimbo milioni 60, tu kila mwezi.

  • What will you do with this money kwa miezi sita ya mwanzo ili wananchi wajue wamepata mbungu na sio mbunge kapata jimbo ?

Hili swali langu ni kutaja kujua priorities zako na vipi utapendeza zitekelezwe?


  • Je wewe unajiona una tofauti gani na wabunge wengine zadi ya 200 tulionao mjengoni? Mimi singalii elimu nataka kujua watu wana idea gani za kibunifu

  • Tukiondoa matatizo ya ya jimbo lako ni vitu gani pale mjengoni unaona haviko sawa na utapenda vibadilishwe.Je ni halali wabunge kutolipwa kodi.? Je ni haki na halali mbunge kupata mshahara kuzidi afisa kilimo, afya , RPC mhandisi wa mkoa ?

Nitashukuru nikipata majibu ya maswali
 

Nikweli unachosema ndugu yangu Du Bois ideas..Tuko pamoja kaka...
 

Asante ingawa nina wasiwasi na kauli iliyopitwa na wakati ya "nimeombwa nigombee" 2015. Hata hivyo naamini kauli yako hapo juu imeingia kwenye "hansard" na utakuwa mwanifu kwazo ikiwepo kutokuwa msaliti hapo baadaye. Yaliyoandikwa yameandikwa. All the best.
 

Hapo kwenye Red hapo! Panapaswa kupewa weight kubwa sana.
Imekaa vyema mku.
 
Sijuhi ilikuwaje lakn uenda unapandwa na jazba bila msingi kama pale Temeke mtu anakudrive tu kidogo unapanda mori,unakuwa mkali,unatoa lugha mbaya (easy to tease) ,ni lazma ujifunze kuvumilia na kujenga hoja,jibu hoja kwa hoja,hyo ndo siasa ya CDM

lakini pia sie hatuhtaji kujua hayo sahv,ww nenda jimboni piga kazi,simika chama,buni miradi katika jamii,shiriki kutatua matatizo ya wananchi then ndo uje hapa jamvini utwambie umeishafanya nini... kwa njia hyo you can defeat your opponent,otherwise sisi hapa ni washauri tu kazi ni kwako,take t!
 
CCM-CCK-CDM-CCM-CDM-?

sorry, naomba kuuliza,

unataka utuambia kuwa sasa utakuwa na msimamo, au msimamo wako ni popote upepo unapoelekea?
 
MKUU TUPO PAMOJA japo naona kuna viwavi wanakula hii hoja yako lakini hiyo sio kitu unawa handle vizuri sana na kwa upole
mimi ni mwana-jimbo tuwasiliane tuone kama naweza kukupa mchango wa mawazo katika kulikomboa jimbo
hachana na hao WA MJINI MJINI
 
Nakutakia mafanikio. Kumbuka tu, watu wengi wa vijijini wamezoea "lamba lamba". Mheshimiwa mkono, ana vijisenti, katika maeneo kadhaa ya Musoma vijijini amejitahidi kufanya mambo.
 
Nakutakia kila la kheri. Lakini naomba pia ufahamu nguvu ya fedha ya Mheshimiwa Mkono. Tatizo watu wengi wamezoea 'lamba lamba' hasa wakazi wa vijijini.
 

hhhah..deep down hakuwa na mpango wa kugombea huko.......halafu wengi wanapenda kutumia lugha hii kuonyesha alivyokubalika na kuwa yeye ni kama ulimi( tegemeo lao huko) ndio maana anatumia '' nimeombwa''
 
(wewe si ndiyo inasemekana ulilambishwa chapaa na yule jamaa wa Bank M? hahaha! yule jamaa anavaaga kibaragashia chenye mkia kama mzee small!?)

hapa ngoja niwe mwepesi wa kusikia kwanza; nisiwe mwepesi wa kusema,

Hahahaha...hahahahaha....hahahahaha...Mzee Wa Ban unanifurahisha sana...Ni kweli hapa inabidi uwe mwepesi wa kusikia kwanza na mwepesi wa kusema...Hahahahahaha......Hahahahaha...Kaka mimi sijalambishwa chapaa na yule jamaa wa Bank M...Yea namjua anavaaga kibaragashia chenye mkia ka mzee small...Nasema sijalambishwa kwakuwa mwaka 2010 nilikuwa nagombea Temeke angalia avata yangu...Aliyelambishwa ni mwingine na mimi mbona hawezi coz siko hivyo...Temeke kuna mgombea mmoja kutoka lichama moja la mafisadi yeye na lichama lake walitaka kunilambisha nikawagomea na tukapambana mpaka dakika ya mwisho...hivyo usiwe na wasi wasi...Ila umenifurahisha sana kaka....
 

Asante sana ndugu yangu 'VIKWAZO' kumbe na wewe umeviona eeeeh...nway kaka tuko pamoja..Tafadhari unakaribishwa kwa mchango wa mawazo unaweza ni e-mail kwa nghily@hotmail au kwa skype dickson.nghily au waweza nitwangia ukopenda kwa +255716030030,+255765030030 au +255788030030...Ubarikiwe sana kwa kunitia moyo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…