Aliyetunga wimbo wa "Idd Amin akifa, mimi siwezi kulia..." Ukaimbwa mashule na kambini kama kibwagizo alikuwa nani?

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Habari wadau!

Tuko kwenye mjadala hapa!

Wapo wanaodai ni mwalimu nyerere wengine wanasema ni Mboma, wengine wanasema ni Rais Moi!

Je, ni nani aliyetunga wimbo huo uliosikika kwa maneno "Iddi Amin Akifaa, Mimi siwezi kuliaa, nitamtupa kageraa, ili awe chakula cha mamba!

Je, wimbo huo ulikuwa na ujumbe gani kwa watawala waliofuata?
 
Mkuu ni miaka takribani 40 hivi imepita toka vita ya Kagera, Kwa nini wimbo huu leo ?
 
Jeshini kuna nyimbo za ajabu sana,nimesoma shule moja ya jeshi kwa miaka 4,ni kambi maarufu kwa mafunzo.....kruta wakiwa kwenye mchakamchaka nyimbo zake daaah
 
Iddi Amin Akifaa, Mimi siwezi kuliaa, nitamtupa kageraa, ili awe chakula cha mamba!
Coded...!!!
 
Iddi Amin Akifaa, Mimi siwezi kuliaa, nitamtupa kageraa, ili awe chakula cha mamba!
Coded...!!!
Sasa tuna wahesabu
Walio kufa kwa taabu
Bila hata matibabu

Wengi hawana hesabu
Walio kufa kwa taabu duniani
Mwana lumumba wa kongo
Walimpiga vigongo
Wakamvunja mgongo
Wakamtoa ubongo
Wala sisemi uongo ni ukweli
Tom mboya wa Kenya
Si kiongozi mbaya
Kala risasi ya taya
Maharamia wabaya
Wala hawaoni haya kumuua
Wana kifungo cha maisha gerezani
Na maiti si mwingine ni AMIN
AMIN kapiga ngoma GADDAFI kaimba wimbo maiti nazo husema aaah
Wacha Tanzania utaitambua.
 
Utaka kusema atunge mwingine au
 
Jeshini kuna nyimbo za ajabu sana,nimesoma shule moja ya jeshi kwa miaka 4,ni kambi maarufu kwa mafunzo.....kruta wakiwa kwenye mchakamchaka nyimbo zake daaah
Kwani ile kuruta na kenge nzuri Nani bado unaimbwa?
Maana nilipojibu nzuri kuruta dk 2 nilioga matope mwili mzima.
 
Wewe ilikuwa Coy C? Huu wimbo ulibamba Sana.
 
Nyerere kaenda Uganda
Na sasa Amin hayupo
Insha Allah mungu yupo
Watanzania tutajitawala
Nyerere
 
Wimbo huo ulilenga kuwakumbusha watawala kutawala raia kwa haki na upendo ili wananchi wao wakumbuke yaliyo mema zaidi kwao ........
 
Kama una tone yake nirushie Mkuu, ulikuwa wimbo wangu No.1
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…