Aliyevaa pempers Simba day amesema ana haki kufanya sanaa

Aliyevaa pempers Simba day amesema ana haki kufanya sanaa

Dabil

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2021
Posts
6,823
Reaction score
15,293
Akihojiwa na wasafi amesema anashangaa watu wa haki za binadamu wakilalamika kwa ule ni udhalilishaji.

"Mimi nina haki ya kufanya sanaa, serikali haina bajeti kunilisha mi natafuta na ninalipa kodi, watu wengine wangefanya nilichofanya wala wasingehoji, nina haki zangu kama wengine"
 
Watu wa haki za binadamu na hao wengine wapuuzi, Simba wasiombe radhi halafu waende kushitaki. Aitwe mhusika seme kama ni kweli alidhalilishwa.

Tatizo kubwa ni umasikini hivyo nguvu zao walitakiwa kuzielekeza kwa serikali na sio kukimbilia kwenye vyombo vya habari wakati hawajawahi kumsaidia huyo mtu hata senti tano ya kula
 
Kwan kulitokea nini? Msilete habari kama vile wite tunajua mnachokileta. Toeni ufafanuzi hata kwa picha basi
Siku ya Simba day kuna albino alivaa pampasi katika maigizo ya kuchekesha

Chama cha Albinism kimetoa tamko kuwa Simba inatakiwa kuomba radhi kwa kitendo hicho ambacho wao wamekiona kama ni udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.

Japokuwa muhusika mwenyewe ambaye ni albino amekiri kufanya vile kama sanaa na ni sehemu ya kujipatia mkate wake.

Lakini kuna watu waliokuja na maswali wakiuliza vipi endapo igizo lile lingefanywa na joti ingechukuliwa kwa uzito huu kuwa ni udhalilishaji?

Ukiachana na hilo, kuna Zungu ambaye naye ni Albino ameshangazwa na hiyo taasisi kwa namna walivyopokea hilo igizo.
 
Siku ya Simba day kuna albino alivaa pampasi katika maigizo ya kuchekesha

Chama cha Albinism kimetoa tamko kuwa Simba inatakiwa kuomba radhi kwa kitendo hicho ambacho wao wamekiona kama ni udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.

Japokuwa muhusika mwenyewe ambaye ni albino amekiri kufanya vile kama sanaa na ni sehemu ya kujipatia mkate wake.

Lakini kuna watu waliokuja na maswali wakiuliza vipi endapo igizo lile lingefanywa na joti ingechukuliwa kwa uzito huu kuwa ni udhalilishaji?

Ukiachana na hilo, kuna Zungu ambaye naye ni Albino ameshangazwa na hiyo taasisi kwa namna walivyopokea hilo igizo.
🤣🤣 hapa sasa ndio napata picha kamili.

Kama ni hivi kweli unavyosema nadhani kuna panic button imebonyezwa mahali sasa inajaribu kutafuta aatention ya watu tu lakini there is nothing serious
 
Akihojiwa na wasafi amesema anashangaa watu wa haki za binadamu wakilalamika kwa ule ni udhalilishaji.

"Mimi nina haki ya kufanya sanaa ,serikali haina bajeti kunilisha mi natafuta na ninalipa kodi,watu wengine wangefanya nilichofanya wala wasingehoji ,nina haki zangu kama wengine"
Yule amefanya kwa hiari yake na mapenzi yake.
Wasipende kutaka kuchukua attention kwa vitu ambavyo wala havihitaji attention hiyo.
Kitu gani cha kudhalilisha pale?
 
Hiyo taasisi imetafuta pa kutrend tu, udhalilishaji kivipi? Si ndio sanaa yake, na jamaa mwenyewe anakiri kuwa alifanya kwa hiyari yake.
Simba hakuna kuomba radhi.

Si nchi ya uhuru, hajavunja sheria. Tulieni.
 
Wale Viongozi wa Chama cha Albino Ni Wana Yanga,Sasa wanaliangalia hili swala Kishabiki...!

Badala ya Kumpongeza Mwenzao albino kwa Ujasiri Wake mbele ya Kadamnasi Wenyewe Wanamtoa kwenye reli kumuingizia inferiority Complex..!
 
Simba kama taasisi kubwa
Ilipaswa kupima maudhui ya hilo wanaloliita igizo
Kila kitu kilichofanyika pale kilikuwa ni jambo la simba
Mashabiki kukosa tiketi, mbona wanalaumiwa simba?
Halikuwa jambo zuri uungwana kukosea ni kuomba radhi
 
Siku ya Simba day kuna albino alivaa pampasi katika maigizo ya kuchekesha

Chama cha Albinism kimetoa tamko kuwa Simba inatakiwa kuomba radhi kwa kitendo hicho ambacho wao wamekiona kama ni udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.

Japokuwa muhusika mwenyewe ambaye ni albino amekiri kufanya vile kama sanaa na ni sehemu ya kujipatia mkate wake.

Lakini kuna watu waliokuja na maswali wakiuliza vipi endapo igizo lile lingefanywa na joti ingechukuliwa kwa uzito huu kuwa ni udhalilishaji?

Ukiachana na hilo, kuna Zungu ambaye naye ni Albino ameshangazwa na hiyo taasisi kwa namna walivyopokea hilo igizo.
Tuipuuzeni hiyo taasisi,wanaonekana kuwa ni mashabiki wa jangwani.
 
Akihojiwa na wasafi amesema anashangaa watu wa haki za binadamu wakilalamika kwa ule ni udhalilishaji.

"Mimi nina haki ya kufanya sanaa ,serikali haina bajeti kunilisha mi natafuta na ninalipa kodi,watu wengine wangefanya nilichofanya wala wasingehoji ,nina haki zangu kama wengine"
"Mimi nina haki ya kufanya sanaa ,serikali haina bajeti kunilisha mi natafuta na ninalipa kodi,watu wengine wangefanya nilichofanya wala wasingehoji ,nina haki zangu kama wengine"[emoji419][emoji818]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom