Ally Bananga: Mdude Nyagali anatakiwa kupumzika kwanza, kumpatia kipaza sauti mapema sioni tukimpenda na kumsaidia

Mbonà unakuwa juha, Hawa wanatetea demokrasia, kosa liko wapi?
 
Ukiwa ni mtendaji mkuu wa chama taifa,mipango yote hupata baraka kupitia ofisi yako.

BAVICHA waliandaa "KATIBA DAY"ni jambo jema sana kitaifa kupitia BAVICHA.
Kitendo cha MDUDE kupewa nafasi nakuongea upumbavu nje ya mada haikubaliki.

Nakuomba kaa na vijana wako uwaelimishe mipaka ya uwasilishaji.
 
Kwa hiyo unafikir wew hutokufa! Mjifunze kuelewa kwamba watu wana character tofauti. Mdude ndo alivyo! Jitahidi kumtafsiri kwa kutumia hulka yake, na siyo kwa kutumia utashi wako. Yeye ndo yuko hivo, hayo uliyoshauri anaweza kuyapata akiendelea na harakati zake.
 
Waliusoma upepo mapema! Sometimes shari zinaepukika ukitumia akili na hekima kidogo tu
 
Amevurugwa anaongea utumbo mtupu.
 
Ni kweli maneno ya Mdude hayapendezi. Lakini mnapata wapi moral authority ya kumnyooshea vidole wakati maneno mabaya kuliko haya yalitamkwa dhidi ya viongozi wa upinzani hadharani na mlikaa kimya? Watu wametukanwa bungeni, watu wametishiwa maisha yao n.k. lakini mlikaa kimya ama mlishangilia. Mdude amewekwa ndani kwa tuhuma zisizo na mashiko lakini hamkusema kitu. Waliokuwa wakipiga kelele kumtetea ni wale mliowakejeli kwa kuwaita wanaharakati. Ni wangapi kati yenu, pamoja na huyo mheshimiwa wa Arusha, mliwahi kwenda kumtembelea yeye na wenzake gerezani na kujitokeza Mahakamani zinaposikilizwa kesi zao? Na mnajua kuna wangapi bado wako ndani wakingojea hatma zao?

Katika demokrasi kamili uhuru wa kumkosoa kiongozi wako hata kwa lugha ambayo hataipenda ni sacrosant. Kipimo cha demokrasia ni hatua gani zinazochuliwa dhidi ya watu kama Mdude na sio wangapi wanaimba mapambio kuwapongeza viongozi. Kiongozi ukisikiliza vilio vya watu kama Mdude utafaudika sana kuliko kuwasikiliza wale ambao kila kukicha ni kukupamba.

Amandla...
 
Yaani mtu aliyefanya atoke ndiye amfanyie kauli za dharau hivi?

Unajua serikali inaweza kukata rufani na kesi ikapitiwa upya kwa maelekezo?

Mtu akishauriwa muwe mnaacha kumvimbisha kichwa wakati nyie ni waoga kama tumbili
 
Huyu kijana inaonesha kichwani fuse hazipo sawa sawa na Chadema wanamuangalia tuu.
 
Mdude kichwa yake siyo nzuri na Chadema wanaona wamepata mtaji wa kisiasa.
Kama ccm mlivyoona mmepata mtaji enzi za yule kiongozi muovu.
 
Mdude ni kichaa...chadema waangalie jinsi ya kum-handle
 
Huyu kijana inaonesha kichwani fuse hazipo sawa sawa na Chadema wanamuangalia tuu.

Dhalimu wa Chattle mlimchukulia hatua gani kipindi anapora fedha za Bureau de change na korosho? Mnatuletea kilio kwa mambo mepesi wakati mlikalia kimya uovu wa yule kiongozi dhalimu?
 
Mdude asidhani atatujazia magereza tu......nadhani labda dola iangalie namna
 
Mdude anafanywa mtaji wa kisiasa na wana chadema wenzake.

Lazima atumiwe yeye kwa sasa ili itafutwe sympathy kwa wananchi.

Lakini jambo zuri ni kuwa pengine hao wananchi wakaishia kumuonea huruma tu huyo mdude kama mwanachi mwenzao lakini wasivutike na atakayoyasema.

Mdude anapoteza muda wake tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…