Ally Bananga: Nikifika mbinguni (peponi) nikikuta Mama Samia hayupo natoka peponi

Ally Bananga: Nikifika mbinguni (peponi) nikikuta Mama Samia hayupo natoka peponi

Kunausemi unasemaga ukistaajabu ya Musa.

Leo katika jiji la Arusha aliyekuwa kamanda wa chama cha Demcrasia na Maendeleo Chadema Ally Bananga alirudisha kadi ya chama hicho katika mkutana mkubwa wa adhala wa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Hassan, Kamanda huyo wa zamani ametoa kauli ya ajabu na kushangaza...
Nakwambia hatakuwepo peponi na utakwenda naye jehanamu acha kufuru wewe, unafikiri Mbinguni ticketi ni ushungi?
 
Amemaliza maneno yate, ila njaa mbaya. Siasa ni umalaya..
 
Kunausemi unasemaga ukistaajabu ya Musa.

Leo katika jiji la Arusha aliyekuwa kamanda wa chama cha Demcrasia na Maendeleo Chadema Ally Bananga alirudisha kadi ya chama hicho katika mkutana mkubwa wa adhala wa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Hassan...
Na nyie wafia dini acheni kukuza mambo, huko mbinguni kama kwenda kasema atakwenda yeye, kama hakumkuta atatoka yeye, sasa hiyo ni kesi ya yeye na Mwenyezi Mungu wake, vipi mnaanza kutoa tena hukumu dhidi yake?? sasa mtakuwa na tofauti gani kati yenu na yeye??
 
Ally kaombe toba kwa Mungu. Watu mnaopewa fursa adhimu ya kuongea na Rais wa nchi (sio rais wa Yanga) hadharani msimdhalilishe. Haya ndio masifa yaliyomtoa mwendazake duniani. Uwezo wako wa mwisho ni udiwani na upiga debe. Unataka Rais akusaidie nini? Stupid!
 
Wanasiasa wakikutana kwenye mambo yao waachie na mambo yao.
 
Kunausemi unasemaga ukistaajabu ya Musa.

Leo katika jiji la Arusha aliyekuwa kamanda wa chama cha Demcrasia na Maendeleo Chadema Ally Bananga alirudisha kadi ya chama hicho katika mkutana mkubwa wa adhala wa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Hassan, Kamanda huyo wa zamani ametoa kauli ya ajabu na kushangaza.

Pamoja na kuongea vizuri katika hotuba yake kisiasa lakini ametoa kauli ya ajabu sana hasa kwetu sisi viongozi wa dini imetupa ukakasi mkubwa sana kwa ndugu huyo. Bananga amesema kuwa kama akifika mbinguni na kukuta mama Samia hayupo huko peponi atatoka huko peponi yeye. Sijui atatoka kumtafuta wapi.

Kauli hii nzito na yakushangazana ya kipagani na ya fedhea kwa Mungu wetu imeleta gumzo katika makundi yetu mengi ya wasapu ya viongozi wa dini wakiwemo wachungaji, mashekh, maaskofu, mitume na manabii. Katika haya magrupu viongozi wengi wamebaki midomo wazi na wengine kutatoa macho kanakwamba wanatengeneza saa kwa kukosa pakuanzia kujadili.

Kwa msikilizaji wa kufikiri na akili aliyekuwa anamsikiliza Bananga katika hotuba yake alikuwa kama au likuwa anafanya intavyuu ya kuomba kazi kwa Mhs. Rais na si vinginevyo. Katika maongezi yake alionyesha uzoefu wake wa kazi kuwa anaweza na amekaa katika uongozi kwa vipindi kadhaa na amefanya kadha wa kadha ikiwemo uwazishwaji wa jambo fulani. Alizidi kwenda mbali kwa kusema anauwezo wa kufanya mambo magumu na mchapakazi hivyo anaomba asiachwe benchi atumike katika serikali.

Bananga ambaye mara nyingi amekuwa akitishia kurudisha kadi hiyo ya Chadema lakini leo ametumia mwanya huo kama fulsa kurudisha kadi hiyo na kuomba kazi kwani amekuwa benchi kwa muda sasa kisiasa ukilinganisha na mkewe kuwa mbunge wa viti maarumu kupitia Chadema.

Bananga ambaye Mungu amempa neema ya kutembelea upepo kwani zamani alikuwa mwanachama mtiifu wa CCM na baada ya kuona chama hicho ilikuwa ikidorola mika ya 2013 alibadili gia na kuhamia Chadema, lakini leo kilichotokea CCM kinatokea Chadema hivyo anabadili tena gia na kurudi CCM kusaka fulsa kama alivyosikika katika hotuba yake ya kuombakazi.

Mimi kama mtumishi wa Mungu namshauri Bananga kuomba kitubio kwa Mwenyezi Mungu kwa kauli yake ya kibuli cha uzima, kauli yake ni chukizo kwa Mungu kwani haikubaliki kanisa, haikubaliki msikitini na haikubaliki hata kindagateni mpaka chuo kikuu.
Hatari sana
 
Msaka fursa ni mtu wa kumwenea huruma,kalishwa na mke wake muda mrefu anafahamu Hai na Arusha kuna nafasi.
 
Wakristo, hasa wale wanaomkiri Yesu Kristo na kuiamini Biblia Takatifu, tumeaswa tusilumbane na wasiomjua na kumuamini Yesu Kristo na neno lake, yaani Maandiko Matakatifu, Biblia.

Hilo ni katazo kutoka kwa Mungu wetu, Yehova, sasa nyie mnaotaka kulumbana na Ally Bananga juu ya aliyosema ni kwenda kinyume na maagizo ya Mungu, Yehova.
 
unatoa hukum ww kama nan?
Someni basi Maandiko matakatifu .
Mtese watu , mpige risasi watu , mfunge watu bila hatia na muuwe watu..
Kwa nini msiende motoni.
Samia atawaongoza MaCCM wote kuelekea JEHANAMU hamtoki.
Na huo ndio kweli. Tendeni HAKI kama mnaitaka pepo kweli.
 
Hakuna aliyemdhihaki Mwenyezi Mungu akabaki salama, tumpe muda. Kuingia peponi sio sawa na kutoka ccm kuingia chadema na kurudi ccm. Eti mtu anadai kuwa kapewa pepo na Mungu kisha kufika mbinguni akamkose huyo na kuamua kurudi. Njaa hajawahi kumuacha mtu salama.
 
Kwenye kuhama chama na mengine mengi sina tatizo. Kuhusu hilo la viongozi wa dini kubaki vinywa wazi, wao ni akina nani kuzuia watu wasiseme yaliyo moyoni mwao?
 
Mtume S.a.w alitutahadharisha sana kupenda (kujipendekeza) kupitiliza kwa kuwa utajikuta unakufuru tu!

Huyu Mtoto anadhan issue ya Kuingia Peponi ni kama kuingia Bungeni tu

Swahaba Mkubwa sana wa Bw. Mtume s.a.w ambae alikuwa Mweusi (Bilal bin Rabbah) alisema hata akiwa kishaingiza Mguu mmoja ndani ya Pepo bado hatokuwa na uhakika wa kuingia Peponi lakin anatokea mtu kwa kujipendekeza tu anakufuru kwa kumpa Mungu Masharti eti akitaka kumuingiza Peponi lazima na fulani nae aingie…

vyeo vya Kidunia vinaishia huku huku huko hakutakuwa na mambo ya 'kupita bila ya kupingwa'
Mwarabu toleo la mwisho na wala hakuwa na kizazi endelevu wala endelenyuma Bilal bin Rabbah? Hivi waarabu na watu weusi wapi na wapi. Quran inasema mtu mweusi ni mwenye dhambi na anaishi Afrika.
 
Anzisha uzi nitakupa majibu ya maswali yako yote

Hapa si sehemu ya Mjadala husika
Mwarabu toleo la mwisho na wala hakuwa na kizazi endelevu wala endelenyuma Bilal bin Rabbah? Hivi waarabu na watu weusi wapi na wapi. Quran inasema mtu mweusi ni mwenye dhambi na anaishi Afrika.
 
Back
Top Bottom