Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Ally Hapi, amehitimisha kampeni za chama hicho mkoani Mbeya kwa kuhimiza wananchi kuwachagua viongozi wa CCM katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024. Katika hotuba yake, Hapi alisisitiza umuhimu wa kampeni za kistaarabu zinazojikita katika kuhamasisha maendeleo badala ya siasa za chuki.
Alieleza kuwa CCM imejipambanua kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ya elimu, afya, na maji chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan
Soma Pia: Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Huku akitoa wito kwa wananchi kuendelea kuwa na imani na viongozi wa CCM, akisema kwamba rekodi yao inaonyesha matokeo ya kweli na kujali maslahi ya wananchi.
Hapi pia alisisitiza kwamba wagombea wa CCM wana uwezo wa kuendelea kusimamia miradi ya maendeleo na kuleta mabadiliko chanya kwa jamii, pamoja na kuhimiza wananchi kuchagua viongozi wenye sera na uwezo wa kuboresha maisha yao.
Alieleza kuwa CCM imejipambanua kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ya elimu, afya, na maji chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan
Soma Pia: Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Huku akitoa wito kwa wananchi kuendelea kuwa na imani na viongozi wa CCM, akisema kwamba rekodi yao inaonyesha matokeo ya kweli na kujali maslahi ya wananchi.
Hapi pia alisisitiza kwamba wagombea wa CCM wana uwezo wa kuendelea kusimamia miradi ya maendeleo na kuleta mabadiliko chanya kwa jamii, pamoja na kuhimiza wananchi kuchagua viongozi wenye sera na uwezo wa kuboresha maisha yao.