Ally Kessy: Katiba sio msaafu, Rais Magufuli akimaliza muda wake tutatengua Katiba aongezewe muda | Spika Ndugai amuunga mkono

Sioni haja ya kulalama rais kafanya makubwa tumwache na tumpe miaka mingine atuvushe,lawama za nini? Au tunataka rais mla rushwa kitu ambacho JPM kakikataa?

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app

JPM hajazuia rushwa, alichofanya ni kuminya uhuru wa vyombo vya habari ili visitangaze mambo ya rushwa. Lengo hasa ni kuhadaa umma kuwa hamna rushwa ili akae madarakani atakavyo. Hilo la yeye kutaka kukaa madarakani alianza toka alipoingia madarakani kwa kuwatuma kuna Nkamia. Hii kunajisi chaguzi za nchi hii, ni ili kupata watu watakaomuongezea muda wa kukaa madarakani zaidi ya muda wa sasa wa katiba. Ila mjue mnacheza mchezo bwana hatari ile mbaya. Mchelea mwana kulia ...
 
Mbona yeye alishakataa, unalazimishaje dhamira iliyokataa.
Halafu kumpima rais mzuri ni kwenye kipindi chake cha pili siyo hiki cha kwanza
 
Wataliongezea muda kaburi lake.
 
Jpm mwenyewe ni mbugiaji wa rushwa mabonge makubwa makubwa
 
Magufuli anafanya vizuri maamuzi ya kumuongezea muda ni wazo zuri

Kama Mbowe ni mwenyekiti wa kudumu kwanini tusiwe na Rais wa kudumu[emoji16]

Sioni haja ya kulalama rais kafanya makubwa tumwache na tumpe miaka mingine atuvushe,lawama za nini? Au tunataka rais mla rushwa kitu ambacho JPM kakikataa?

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app

wazee ivi mmesoma shule kweli ? kama mmesoma hamkuelimika wakuu, au mpo kazini ? mnanipa ukakasi wakuu..TANZANIA ni nchi na sio chama na hatufanyi mashindano ya nchi vs chama. Yan kina job ndugai kwake hata maji hakuna na wananchi wamemkataa ila bado ana uhakika kuwa atarudi bungeni mnaona hawa watu wako sawa ? . Aisee mtakufa maskini wa mawazo na fikra..
 
Na tumetangaziwa rasmi, mtu asije kusema ni habari iliyonvunjika vunjika.
 
Watanzania hilo bomu mnalotaka kulitengeneza ni zaidi ya bomu la NYUKLIA.
kama watangulizi wake wangefanya haya anayotaka kufanya yeye.
Leo hii TUSINGEMJUA MAGUFULI.
rais angekuwa mwinyi,mkapa,au kikwete.
Hili jaribio mnalotaka kulifanya ni baya na Halifai.
 
Muulize anaongelea rushwa gani, hao wanaonunuliwa ni kwa mshahara wake au kwa rushwa?
 
Uchu wa madaraka anao Mbowe,Lipumba,Mbatia,Mrema hawataki kuachia kiti
 
Kama ni mechi, CCM wametupiga chenga timu yetu wote, sasa kabaki sentahafu wetu ( Sir God ) tumemuachia yeye atuokoe tusifungwe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…