Almanusura brother kunyimwa mke ukweni

Almanusura brother kunyimwa mke ukweni

Ishu siyo kupigwa goti ishu hapo ni hiyo kuvishana pete,hivi haya mambo ya kishenzi shenzi mmeyarithi kutoka wapi?

Unamvalisha pete ili iweje na kwa faida ipi?
Binafsi sikuwaga na Mambo ya mapete,mababu na mababa zetu wamezekeana bila hizo mambo ya kilimbukeni ya kimapete kumpa padri hela ama wauzaji,iweje mie ndie nitoke kwa nature.
Ndoa kiafrika tunaishi swafi Kama ambavyo baba wa babu waliishi miaka iyo zamani before ya mkoloni. Waafrika bana mtt akiongea English anajisifia anaona Kama amesomesha mno
 
Maana yake hasa ni nini hii....yan walikua wana test kama muoaji anakula "tope" maana unyevu wa chakula na mchuz wake si unatengeza tope tope hapo chini.
Sasa angekuka tu ooohh hapo wana piga tick [emoji23][emoji23][emoji23]
Sisi wenyewe hata hatuelewi, tulimuuliza kwetu tunafanya hivi??, Huo ndio mwanzo wa kupewa libwata
 
Hiyo cha mtoto,juzi kati mdogo wangu wa kike,mchumba wake alikuwa anajitambulisha nyumbani kwetu,huyo shemeji yangu ni masai,chakula kilipikwa mapema sana toka saa 7 mchana tayari,kimbembe kilikuja pale tunawasubiri upande wa kiume waje kujitambulisha,tulisubiri wapi hawaji wala nini,nikimuuliza mdogo wangu mbona hao watu hawaji anasema wanakuja subirini,wajomba waliokuwa wametoka moshi wakaona bora waandoke,mama akawaita ndani wajomba wakapewa chakula ndio wakaondoka wakiwa wamechukia sana.

Tuliwasubiri wakaja mda wa saa 10 jioni,na Kigari Chao cha ist,wakiwa wamebeba ndizi mikungu 3,viazi gunia?mafuta dumu kubwa,sukari mfuko mmoja,mchele kilo 50,unga wa ngano kilo 25,kwenye hilo gari kulikuwa hakuna hata mwanaume mmoja,wote walikuwa wanawake.

Kumbembe kilikuja pale waliponiita,nikabebe ile mizigo,niligoma katu katu,yani mimi nikabebe mizigo iliyoletwa na wanawake,tena wamechelewa ,chakula kipo tu kinawasubiri mda wote hakuna aliyekula wanawasubiri mda wote,niliyona yale ni madharau niligoma katu katu mpaka wakatafuta watu wakusomba ile mizigo..
Nina mashaka mnoo na hichi ulichoandika kama ni kweli.

Unasema kwenye hiyo gari ya IST waliyokuja nayo waoaji hakukuwa na mwanaume hata mmoja, wote walikuwa wanawake. Sasa hata muoaji (mwanaume) hakuwepo au naye alikuwa ni mwanamke?

Unasema muoaji alikuwa mmasai, sasa tangu lini wamasai wakapeleka ukweni wanawake tupu kusindikiza mwanaume kuoa? Unazijua mila za kimasai?

Unasema mlipanga shughuli iwe saa saba mchana, lakini waoaji wakachelewa 'mnoo' na kuja saa 10jioni kiasi cha wajomba kula na kusema na kusepa zao kabla ya waoaji kufika. Hivi kwa sisi waafrika na katika uhalisia wake, huo uchelewaji ni kitu kipya au cha ajabu mnoo kiasi cha wenyeji kususa?

Unasema waoaji walikuja na gari ya IST ikiwa na hivi vitu:
-Wanawake tupu (sijui ni wangapi? Labda tuseme walikuwa watano)
-Gunia la viazi
-Mikungu ya ndizi mitatu
-Kiroba cha sukari
-Mchele kilo 50
-Dumu moja la mafuta ya kula
-Gunia la viazi
-Mfuko wa ngano
Katika hali ya kawaida hiyo gari isingeweza kupakia hizo vitu zote na kuenea. Huo ni mzigo wa kubebwa na pick up au Kirikuu.
 
Binafsi sikuwaga na Mambo ya mapete,mababu na mababa zetu wamezekeana bila hizo mambo ya kilimbukeni ya kimapete kumpa padri hela ama wauzaji,iweje mie ndie nitoke kwa nature.
Ndoa kiafrika tunaishi swafi Kama ambavyo baba wa babu waliishi miaka iyo zamani before ya mkoloni. Waafrika bana mtt akiongea English anajisifia anaona Kama amesomesha mno
Ahaha mkuu now days tumebebwa na upepo wa culture na traditions za kimagharibi kwa kiwango kikubwa sanaa
 
Mm nashangaaga hata hizi engagement, dume linapiga goti ! Naghafilika Sana , yeye (ke) ndo anatakiwa apige goti, ama la tusimame wote ,,,,
Dume linapiga goti alafu linaangua kilio balaa kama dokta kumbuka birthday ya mkewe alilia kama kafiwa na mama mzazi😂😂
 
Mm nashangaaga hata hizi engagement, dume linapiga goti ! Naghafilika Sana , yeye (ke) ndo anatakiwa apige goti, ama la tusimame wote ,,,,

Mwanamke aombe ndoa?
Yeye ndo akawe kichwa wakifika huko ndani, uanze kulia kulia
 
Ishu siyo kupigwa goti ishu hapo ni hiyo kuvishana pete,hivi haya mambo ya kishenzi shenzi mmeyarithi kutoka wapi?

Unamvalisha pete ili iweje na kwa faida ipi?
Acha ujinga ulioridhishwa kutoka kwa Mama Edson( Ellen white) Nabii mwongo .
Uliza kwa uzuri utelekezwa maana ya pete
 
Mwanamke aombe ndoa?
Yeye ndo akawe kichwa wakifika huko ndani, uanze kulia kulia
Kiafrika mwanamke kupiga goti wala sio ishu..ni ishara ya heshima na adabu ndivyo mama zetu wamekua wakifunzwa ndio maana ndoa zao zinabaki kuwa bora sana kuliko hizi na haki sawa
 
Dume linapiga goti alafu linaangua kilio balaa kama dokta kumbuka birthday ya mkewe alilia kama kafiwa na mama mzazi😂😂
Yule sio mwanaume braza.Hata muda wa kufuatilia vimeo kama vile huwa sinaga..wale special group.
 
Nina mashaka mnoo na hichi ulichoandika kama ni kweli.

Unasema kwenye hiyo gari ya IST waliyokuja nayo waoaji hakukuwa na mwanaume hata mmoja, wote walikuwa wanawake. Sasa hata muoaji (mwanaume) hakuwepo au naye alikuwa ni mwanamke?

Unasema muoaji alikuwa mmasai, sasa tangu lini wamasai wakapeleka ukweni wanawake tupu kusindikiza mwanaume kuoa? Unazijua mila za kimasai?

Unasema mlipanga shughuli iwe saa saba mchana, lakini waoaji wakachelewa 'mnoo' na kuja saa 10jioni kiasi cha wajomba kula na kusema na kusepa zao kabla ya waoaji kufika. Hivi kwa sisi waafrika na katika uhalisia wake, huo uchelewaji ni kitu kipya au cha ajabu mnoo kiasi cha wenyeji kususa?

Unasema waoaji walikuja na gari ya IST ikiwa na hivi vitu:
-Wanawake tupu (sijui ni wangapi? Labda tuseme walikuwa watano)
-Gunia la viazi
-Mikungu ya ndizi mitatu
-Kiroba cha sukari
-Mchele kilo 50
-Dumu moja la mafuta ya kula
-Gunia la viazi
-Mfuko wa ngano
Katika hali ya kawaida hiyo gari isingeweza kupakia hizo vitu zote na kuenea. Huo ni mzigo wa kubebwa na pick up au Kirikuu.
Nakujibu kama ifuatavyo,wamasai wanamila wanatangulia wanawake ukeni kuangalia boma then baada ya miezi kadhaa wanatangulia wanaume wakiwa na muoaji mwenyewe,sehemu sisi tulipo na kwahao wanaume sio mbali wengine walitangulia kwa miguu,na kwenye ist walikaa watu wa 3 mama mkwe alikuwa dereva,dada mtu anayeoa,na shangazi mtu,mbele wamekaa wawili nyuma kakaa mmoja,then siti ikavunjwa wakapakiza vitu kwenye siti na kwenye but,
Wajomba waliondoka mapema kwakuwa wanaishi moshi vijijini kule usafiri unasumbua wa kupanda masama
 
Habari zenu wadau, mambo vipi?
Moja kwa moja kwenye mada.

Juzi kati nikiwa katika harakati zangu za kuzunguka sana mikoani kuuza maneno (marketing) kulingana na nature ya kazi nayofanya ili mradi tu nipate wateja (sales) wa kunipatia mkate wa kila siku nikajikuta niko Iringa mjini.

Hapa mimi ni nyumbani japo kiasili kwetu ni Mbeya Rungwe lakini wazee walijikuta iringa miaka mingi sana hivyo nimezaliwa hapa na elimu yangu yoote nimeipata hapa mpaka kuhitim kidato cha 6.

Kwahiyo kwakifupi nikawa nimerudi Iringa lakini kikazi zaidi na nilikua na plan ya kuwpo kwa siku 6 then ya 7 nigeukie upande mwingine.

Sasa basi, hapa home (nilifikia kwa wazee) nikakuta kuna ratiba ya kwenda maeneo fulani panaitwa KIWELE ambako huko brother alikua amechumbia na anataka kuoa huko.Hii kiwele ni Njia ya kwenda PAWAGA (haya ni maeneo ndani ya Wilaya ya Iringa vijijini chini uwakilishi wa Mh.LUKUVI 😂😂 watu wanaogopa hata kum challenge aondoke).

Basi nikaulizwa kama nitakua na nafasi (ilikua ni siku kama ya 3 mbele toka nifike) ili nijumuike kwenye msafara.
Nikawaambie haina shida , by the way huyu ni brother kukataa kumpa company ni utovu wa nidham wa nje nje.Nikaweka ratiba sawa za nisikosekane.

Siku ya siku ikafika tukaelekea ukweni.Mimi, brother, madogo kadhaa, ma sister, ma aunt na baba na mama.

Baada ya kufika taratibu zote zikaendelea palee ikiwemo suala la kutoa na kupokea mahali (taratib ni ndefu ila kwa kifupi zilifuatwa na kama mjuavyo ni baadhi tu ya watu hujumuika kwenye ile session na sio wote kwa pande zote).

Kama mnavyojua sie wengine tusio na mambo mengine (YASIO NA MSINGI) kama ambavyo imezoeleka siku hizi, tuli plan siku hiyo ya kutoa mahali ndio pia Shemeji atavikwa PETE tufanye mambo simple tu isiwe sherehe separate kama wengi wafanyavyo.

Basi baada ya mahali NDIO KIMBEMBE KILIPOTAKA KUJITOKEZA.

Brother akatakiwa kwenda kuwasalimia mashangazi wa mkewe ambao wao walikua wamekaa location separate kabisa pale nyumbani (ilikua ni shughuli iliyohudhuriwa na ndugu wengi kidogo) na umbali walipokua wamekaa hawa watu ni kama mita 15 toka sitting room ambako mahali ilikua inakabidhiwa na distance hiyo ni mchanga tuuu na vumbi hadi kuwafikia mashangaji waliokua wame relax kwenye viti chini ya ka TENT flani hiv.

Sasa brother akaanza kupiga hatua kuelekea huko akiongozana na wazee na mshenga ndipo na huko ndiko shemeji alikokua na zoez zima la ENGAGENENT (kumvisha pete shemeji) lilitakiwa kufanyika.

akaambiwa sasa bwana huku unakokwenda UNAPASWA KUTEMBEA KWA MAGOTI MPAKA KUWAFIKIA MASHANGAZI NA KUPITA UWASABAHI UKIWA UMEPIGA MAGOTI...

Aaahhhh hapo sijui ilikuaje ila braza akagoma katakataaaaa..Yan ile strongly amamwambia mshenga wake (huku wazee baba na mama) wakisikia bayana kwamba "MIMI SIWEZI TEMBEA KWA MAGOTI KUMFUATA MKE WANGU NA NDUGU ZAKE ILI KUMVISHA PETE "

Akakataa katakata.Mshenga akamsisitiza sana ile kichini chini kwamba tutaaibika maana hiz ndio mila zao hawa na si unaona wanatungoja sisi kule tufike(maana sisi kiumeni tulikua huku na wao kikeni pamoja na wazaz wao walikua kule af hapa kat hizo mita 15 zimetu set apart ambapo braza anatakiwa kutangulia akitembea kwa miguu sis tukimfuata nyuma).

Braza akagomaa katakataaaa.."SIWEZIIIIII.KWANI MIMI NDIO NAMUOA YEYE AU YEYE NDIO ANANIOA MIMI?".

Baada ya zoez kuonekana gumu na hakuna dalili za braza kukubali ikabidi mzee/ baba yaan aingilie kati maana hata yeye hicho kitu kwa mbali niliona kama hajakielewa hiv ila akawa katulia tuuu shughul ana deal nayo mshenga.

Na ikumbukwe hapo wakwe zetu wakawa kama wameduwaa giv wanajiuliza nini kinaendelea kule mbona kama wana jadiliana badala ya kuja tumalize kazi? Ilichukua kama dakika 7 hiv katika hii sintofahamu.

Ikabidi mzee asogee mbele kidogo kuwaelekea wakwe zetu kwa unyenyekevu akasema Jaman kama mnavyojua VIJANA WA SIKU HIZI WAJUAJI hawapendi kufuata mila zetu.Sasa basi naomba kwakwel mumruhusu aje akiwa anatembea kawaida tu kama itawezekana..Basi upande wa pili nao wakajadili kama dakika 3 hiv kisha wakasema SAWA ..

Hapo sasa ndio tukabjongea kuelekea kunako mahala wakwe walipo ili kumaliza zoezi la Kutoa salamu na kumvisha pete mke wetu ila kwakua shemeji ALIJIPANGA KUPIGIWA GOTI KUVIKWA PETE akajikuta ameshindwa kuiga GOTI yeye pia hivyo wakavishana pete wima wima.

Ma aunt wakagewa Hi ki sela huku wamenunaaa 😂😂

Dah nikastaajab sana haya mambo ya mila yalivyo magumu.
Tukamaliza tukala tukanywa tukaondoka kurud iringa mjini.

Nikiwa njiana nikamuuliza brother kama angekaza mpaka mwisho hata kama ingem gharim kukosa mke ??mana alivunja taratibu za watu!!! AKASEMA KATU ASINGEWEZA KUMPIGIA MAGOTI MKEWE MBELE ZA WATU WALA HAWEZ PIGIA GOTI NDUGU YEYOTE WA MKE WAKAT YEYE NDIO ANAKABIDHIWA MTOTO WAO AKAMTUNZE.
"CHUMBANI PEKE YETU NAWEZA PIGIA MKE WANGU GOTI KAMA NIMEMKOSEA KOSA KUBWA SANA LA KUHATARISHA NDOA YETU ILA SIO HAYA MAMBO YA KIPUUZI YA KUCHORESHANA NISIJE NIKAJIKUTA NIMEKABIDHI NAFASI YANGU KAMA KICHWA KWA MKE WANGU KISHA AANZE KUNISUMBUA KUMBE YOTE NIMESABABISHA MWENYEWE.

Nikamkubali sana brother.

Uzi tayari
heko kwa bro, mimi sipigi hata tukiwa peke yetu chumbani, yaani hata iweje
bora aende kwao
 
Habari zenu wadau, mambo vipi?
Moja kwa moja kwenye mada.

Juzi kati nikiwa katika harakati zangu za kuzunguka sana mikoani kuuza maneno (marketing) kulingana na nature ya kazi nayofanya ili mradi tu nipate wateja (sales) wa kunipatia mkate wa kila siku nikajikuta niko Iringa mjini.

Hapa mimi ni nyumbani japo kiasili kwetu ni Mbeya Rungwe lakini wazee walijikuta iringa miaka mingi sana hivyo nimezaliwa hapa na elimu yangu yoote nimeipata hapa mpaka kuhitim kidato cha 6.

Kwahiyo kwakifupi nikawa nimerudi Iringa lakini kikazi zaidi na nilikua na plan ya kuwpo kwa siku 6 then ya 7 nigeukie upande mwingine.

Sasa basi, hapa home (nilifikia kwa wazee) nikakuta kuna ratiba ya kwenda maeneo fulani panaitwa KIWELE ambako huko brother alikua amechumbia na anataka kuoa huko.Hii kiwele ni Njia ya kwenda PAWAGA (haya ni maeneo ndani ya Wilaya ya Iringa vijijini chini uwakilishi wa Mh.LUKUVI [emoji23][emoji23] watu wanaogopa hata kum challenge aondoke).

Basi nikaulizwa kama nitakua na nafasi (ilikua ni siku kama ya 3 mbele toka nifike) ili nijumuike kwenye msafara.
Nikawaambie haina shida , by the way huyu ni brother kukataa kumpa company ni utovu wa nidham wa nje nje.Nikaweka ratiba sawa za nisikosekane.

Siku ya siku ikafika tukaelekea ukweni.Mimi, brother, madogo kadhaa, ma sister, ma aunt na baba na mama.

Baada ya kufika taratibu zote zikaendelea palee ikiwemo suala la kutoa na kupokea mahali (taratib ni ndefu ila kwa kifupi zilifuatwa na kama mjuavyo ni baadhi tu ya watu hujumuika kwenye ile session na sio wote kwa pande zote).

Kama mnavyojua sie wengine tusio na mambo mengine (YASIO NA MSINGI) kama ambavyo imezoeleka siku hizi, tuli plan siku hiyo ya kutoa mahali ndio pia Shemeji atavikwa PETE tufanye mambo simple tu isiwe sherehe separate kama wengi wafanyavyo.

Basi baada ya mahali NDIO KIMBEMBE KILIPOTAKA KUJITOKEZA.

Brother akatakiwa kwenda kuwasalimia mashangazi wa mkewe ambao wao walikua wamekaa location separate kabisa pale nyumbani (ilikua ni shughuli iliyohudhuriwa na ndugu wengi kidogo) na umbali walipokua wamekaa hawa watu ni kama mita 15 toka sitting room ambako mahali ilikua inakabidhiwa na distance hiyo ni mchanga tuuu na vumbi hadi kuwafikia mashangaji waliokua wame relax kwenye viti chini ya ka TENT flani hiv.

Sasa brother akaanza kupiga hatua kuelekea huko akiongozana na wazee na mshenga ndipo na huko ndiko shemeji alikokua na zoez zima la ENGAGENENT (kumvisha pete shemeji) lilitakiwa kufanyika.

akaambiwa sasa bwana huku unakokwenda UNAPASWA KUTEMBEA KWA MAGOTI MPAKA KUWAFIKIA MASHANGAZI NA KUPITA UWASABAHI UKIWA UMEPIGA MAGOTI...

Aaahhhh hapo sijui ilikuaje ila braza akagoma katakataaaaa..Yan ile strongly amamwambia mshenga wake (huku wazee baba na mama) wakisikia bayana kwamba "MIMI SIWEZI TEMBEA KWA MAGOTI KUMFUATA MKE WANGU NA NDUGU ZAKE ILI KUMVISHA PETE "

Akakataa katakata.Mshenga akamsisitiza sana ile kichini chini kwamba tutaaibika maana hiz ndio mila zao hawa na si unaona wanatungoja sisi kule tufike(maana sisi kiumeni tulikua huku na wao kikeni pamoja na wazaz wao walikua kule af hapa kat hizo mita 15 zimetu set apart ambapo braza anatakiwa kutangulia akitembea kwa miguu sis tukimfuata nyuma).

Braza akagomaa katakataaaa.."SIWEZIIIIII.KWANI MIMI NDIO NAMUOA YEYE AU YEYE NDIO ANANIOA MIMI?".

Baada ya zoez kuonekana gumu na hakuna dalili za braza kukubali ikabidi mzee/ baba yaan aingilie kati maana hata yeye hicho kitu kwa mbali niliona kama hajakielewa hiv ila akawa katulia tuuu shughul ana deal nayo mshenga.

Na ikumbukwe hapo wakwe zetu wakawa kama wameduwaa giv wanajiuliza nini kinaendelea kule mbona kama wana jadiliana badala ya kuja tumalize kazi? Ilichukua kama dakika 7 hiv katika hii sintofahamu.

Ikabidi mzee asogee mbele kidogo kuwaelekea wakwe zetu kwa unyenyekevu akasema Jaman kama mnavyojua VIJANA WA SIKU HIZI WAJUAJI hawapendi kufuata mila zetu.Sasa basi naomba kwakwel mumruhusu aje akiwa anatembea kawaida tu kama itawezekana..Basi upande wa pili nao wakajadili kama dakika 3 hiv kisha wakasema SAWA ..

Hapo sasa ndio tukabjongea kuelekea kunako mahala wakwe walipo ili kumaliza zoezi la Kutoa salamu na kumvisha pete mke wetu ila kwakua shemeji ALIJIPANGA KUPIGIWA GOTI KUVIKWA PETE akajikuta ameshindwa kuiga GOTI yeye pia hivyo wakavishana pete wima wima.

Ma aunt wakagewa Hi ki sela huku wamenunaaa [emoji23][emoji23]

Dah nikastaajab sana haya mambo ya mila yalivyo magumu.
Tukamaliza tukala tukanywa tukaondoka kurud iringa mjini.

Nikiwa njiana nikamuuliza brother kama angekaza mpaka mwisho hata kama ingem gharim kukosa mke ??mana alivunja taratibu za watu!!! AKASEMA KATU ASINGEWEZA KUMPIGIA MAGOTI MKEWE MBELE ZA WATU WALA HAWEZ PIGIA GOTI NDUGU YEYOTE WA MKE WAKAT YEYE NDIO ANAKABIDHIWA MTOTO WAO AKAMTUNZE.
"CHUMBANI PEKE YETU NAWEZA PIGIA MKE WANGU GOTI KAMA NIMEMKOSEA KOSA KUBWA SANA LA KUHATARISHA NDOA YETU ILA SIO HAYA MAMBO YA KIPUUZI YA KUCHORESHANA NISIJE NIKAJIKUTA NIMEKABIDHI NAFASI YANGU KAMA KICHWA KWA MKE WANGU KISHA AANZE KUNISUMBUA KUMBE YOTE NIMESABABISHA MWENYEWE.

Nikamkubali sana brother.

Uzi tayari
Mambo ya mila na desturi, ya kawaida Sana
 
Back
Top Bottom