Almas Kasongo: Bodi ya ligi itatoa adhabu kwa Maofisa Habari wa timu wanaochekesha na kushindwa kuzungumzia Mpira

Almas Kasongo: Bodi ya ligi itatoa adhabu kwa Maofisa Habari wa timu wanaochekesha na kushindwa kuzungumzia Mpira

Aanze na manara aliyesema yeye ni bingwa wa propaganda
 
Hawa wazee wanatakiwa waondoshwe mmoja baada ya mwingine. Yani mwenyekiti wa bodi ya ligi hata hafananii
 
Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi (TPLB), Almas Kasongo amesema msimu watatoa adhabu kwa Maofisa Habari wa timu wanaochekesha na kushindwa kuzungumzia Mpira huku akizikumbusha klabu kufuata kanuni kwa kuajiri maafisa habari wenye elimu ya habari.

“Kuna Muda unamsikiliza Ofisa Habari wa timu na kujiuliza, huyu ni kiongozi wa timu au mchekeshaji? Niseme tu ndugu zangu, msimu ujao tutadili na watu hawa kwa kuwapa adhabu” —— amesema Kasongo.
Huyo Kasongo bwege kweli.
 
NI Tanzania tu mtu kucheka kwenye Mpira unapangiwa. hivi utajuaje huyu ameongea neno la kuchekesha
 
Mbona hata kwenye nyumba zetu za ibada viongozi wetu wa dini huwa wanatuchekesha??
Mpira wa Tanzania ni siasa tu.
 
Naweka mbele weledi katika kazi yeyote.

Ila soka letu bila kelele au vichekesho (sio matusi) vya hawa wasemaji na mashabiki hamna lolote.

Taratibu zifuatwe, ila sisi kwenye pitch bado sana.

Ni kelele tu zinatengeneza fans base kubwa katika soka letu.

Utaratibu huu ikifutwa:
1. Manara nampa wiki tu watamla kichwa.
2. Ahmed Ali miezi mitatu inamtosha, japo anabadilika badilika kulingana na upepo.
3. Ibwe nae anapaswa kujiangalia, haka kajamaa nako kana maneno machafu sana.

4. Ali Kamwe yupo safe kabisa katika hili.
Ally Kamwe naye ana mdomo mchafu tena hana adabu kabisa kumbuka ishu yake na kumlinganisha na andazi. Kwa ujumla wote hao wanne uliowataja wabadilike utani uwepo lakini isifike kukashifiana.
 
Basi angewaambia wanaosikiliza wasicheke, Yani atathibitishaje kama aliezungumza alikuwa na lengo la kuchekesha au no msikilizaji tu kaamua kucheka? atapimaje hivyo vichekesho? Kasongo amsona wasemaji wanapata majina kuliko yeye na raisi wake
 
Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi (TPLB), Almas Kasongo amesema msimu watatoa adhabu kwa Maofisa Habari wa timu wanaochekesha na kushindwa kuzungumzia Mpira huku akizikumbusha klabu kufuata kanuni kwa kuajiri maafisa habari wenye elimu ya habari.

“Kuna Muda unamsikiliza Ofisa Habari wa timu na kujiuliza, huyu ni kiongozi wa timu au mchekeshaji? Niseme tu ndugu zangu, msimu ujao tutadili na watu hawa kwa kuwapa adhabu” —— amesema Kasongo.
Yupo sawa kabisa.
 
Ally Kamwe naye ana mdomo mchafu tena hana adabu kabisa kumbuka ishu yake na kumlinganisha na andazi. Kwa ujumla wote hao wanne uliowataja wabadilike utani uwepo lakini isifike kukashifiana.
Nilikua nimesahau, kumbe naye ni mshenzi mshenzi.
 
Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi (TPLB), Almas Kasongo amesema msimu watatoa adhabu kwa Maofisa Habari wa timu wanaochekesha na kushindwa kuzungumzia Mpira huku akizikumbusha klabu kufuata kanuni kwa kuajiri maafisa habari wenye elimu ya habari.

“Kuna Muda unamsikiliza Ofisa Habari wa timu na kujiuliza, huyu ni kiongozi wa timu au mchekeshaji? Niseme tu ndugu zangu, msimu ujao tutadili na watu hawa kwa kuwapa adhabu” —— amesema Kasongo.
Ni sawa kabisa kwa maana vitengo vilikuwa vimeingiliwa na waimba taarab kutwa nzima ni mipasho tu, badala ya kuongea kiuweledi unakuwa comedy si Bora ukaungane na wakina bambo!
 
Back
Top Bottom