Alphonce Simbu: Hatukwenda kuiangalia njia(Olimpiki 2024), tuliiona tu kwenye Mtandao

Alphonce Simbu: Hatukwenda kuiangalia njia(Olimpiki 2024), tuliiona tu kwenye Mtandao

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mwanariadha Alphonce Simbu alipotua Nchini akitokea Ufaransa alihojiwa na hii ni sehemu ya maelezo yake kuhusu sababu za yeye kutofanya vizuri na kushinda Medali kwenye Michezo ya Olimpiki 2024 Jijini Paris:

"Kwanza kabisa tulitakiwa tujijue njia ambazo tutatumia kukimbia hata miezi miwili kabla ili tuweze kuifanyia mazoezi, kuanzia hapo lakini tuliijua siku za karibuni kabla ya kuelekea Paris, hiyo ilikuwa changamoto kwetu.

“Mfano mimi nilikimbia sana katika mteleko, nilipofika kwenye kilima kukawa na ugumu kidogo.

“Tuliona njia hiyo katika mtandao tu, tulivyofika tuliangalia tu ilivyochorwa lakini hatukuwa na nafasi ya kwenda kuifanyia mazoezi.

“Unajua njia sio tu kuiangalia lakini lazima uifanyie mazoezi, usipofanya hivyo kuitumia inakuwa ngumu.”

Alipoulizwa maoni yake kuhusu Olipimiki kwa jumla na Tanzania inafeli wapi mesema “Tuwe na tabia ya kukuza Vijana tusiwe na tabia ya kusubiri watu wajitokeze wenyewe inatengeneza ‘gape’, mfano tukiwa na program ya kutafuta wachezaji hasa vijijini, unajua kuna wachezaji wengi wa riadha wapo vijijini.

"Tukiwa na tabia hiyo ya kutafuta watu na kuwatengeneza kutakuwa hakuna tena ile tabia ya Mtu akistaafu panapoa haitakuwepo.”
 
Alichokiongea Simbu kuna uzi mmoja kuna member nae alikiongelea na nikamwambia kuwa wazo lake ni zuri sana, Tanzania vipaji vipo lakini huko ngazi za juu huwa wanasubiri mpaka wajulikane nje ya nchi nao ndio wanajifanya kuwasapoti ambapo walikuwa na uwezo wa kuwasapoti kabla ya kutoka/kujulikana kwao nje ya nchi.
 
Tanzania tumebarikiwa kuwa na vipaji kadhaa, kuna mabaunsa kama wote, kuna wenye kushinda Gym kila siku kike/kiume then Olympic tumepeleka wakimbiaji wawili na waogeleaji wawili, Hivi hao wanaoshinda Gym na wanyanyua vitu vizito wakifundwa basic ya michezo hiyo ya kutumia nguvu kama vile kurusha mkuki, visahani, tufe na kadhalika watashindwa kufanya vizuri kweli? Ni muda sasa Kamati ya Olympic ya Tanzania wajitafakari, ikiwezekana wazame ndani ndani huko vijijini kutafuta vijana wenye vipaji na kuwafunda basic za michezo wanayoona kuwa itawafaa ili waweze kushiriki na kuliletea taifa walau sifa.
 
Mwanariadha Alphonce Simbu alipotua Nchini akitokea Ufaransa alihojiwa na hii ni sehemu ya maelezo yake kuhusu sababu za yeye kutofanya vizuri na kushinda Medali kwenye Michezo ya Olimpiki 2024 Jijini Paris:

"Kwanza kabisa tulitakiwa tujijue njia ambazo tutatumia kukimbia hata miezi miwili kabla ili tuweze kuifanyia mazoezi, kuanzia hapo lakini tuliijua siku za karibuni kabla ya kuelekea Paris, hiyo ilikuwa changamoto kwetu.

“Mfano mimi nilikimbia sana katika mteleko, nilipofika kwenye kilima kukawa na ugumu kidogo.

“Tuliona njia hiyo katika mtandao tu, tulivyofika tuliangalia tu ilivyochorwa lakini hatukuwa na nafasi ya kwenda kuifanyia mazoezi.

“Unajua njia sio tu kuiangalia lakini lazima uifanyie mazoezi, usipofanya hivyo kuitumia inakuwa ngumu.”

Alipoulizwa maoni yake kuhusu Olipimiki kwa jumla na Tanzania inafeli wapi mesema “Tuwe na tabia ya kukuza Vijana tusiwe na tabia ya kusubiri watu wajitokeze wenyewe inatengeneza ‘gape’, mfano tukiwa na program ya kutafuta wachezaji hasa vijijini, unajua kuna wachezaji wengi wa riadha wapo vijijini.

"Tukiwa na tabia hiyo ya kutafuta watu na kuwatengeneza kutakuwa hakuna tena ile tabia ya Mtu akistaafu panapoa haitakuwepo.”
Aache visingizio aseme tu sisi bado.. angeshida angelaumu njia..?
 
Nini kiliwazua wao kufika hata wiki moja kabla ili kufanya mazoezi kupita hizo njia?

Kuna sababu zingine ukizitoa baada ya kushindwa unaonekana na mpumbavu.
 
Nini kiliwazua wao kufika hata wiki moja kabla ili kufanya mazoezi kupita hizo njia?

Kuna sababu zingine ukizitoa baada ya kushinda unaonekana na mpumbavu.
Kwamba wachezaji wa Olympic kutoka Tanzania walitakiwa wajilipie nauli kwenda kukagua na kufanya mazoezi kwanza?
Ni nchi gani umeona wanamichezo wake wanajigharamikia?

Kwamba wachezaji wa Simba na Yanga huwa wanajilipia nauli kwenda kwanza Morocco na Algeria kukagua viwanja kabla ya club bingwa Afrika, au wanajilipia pre season Uturuki na Zanzibar?

Unaongea as if Sambu ndio Wizara au ndio kamati. Wanariadha wanaofanya vizuri ndio maana wanazikimbia hizi shithole countries, msaada sifuri ila lawama sasa.
 
Stupid excuse.

Hadi kilomita 39 alikua namba 3, ghafla kilomita 3 mbele anakua wa 17, hizo 39 ambazo alikua wa 3 alikua pia ameziona kwenye tv ama online, aliwezaje kuwa wa 3?
Kukimbia mbio ndefu sio kuwa 3 Hadi km 39, ni mikakati ya km 42 , na jinsi ya kutumia hizo nguvu katika nyakati tofauti tofauti
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Back
Top Bottom