Kisa hiki kimenikumbusha kitu, siku moja nilipanda dala dala kutoka kituo cha mabibo hostel kuelekea Tabata, kituo kilichofuata (kinaitwa extenal) alishuka mtu nikapata siti nikaketi maana gari lilikuwa level siti tulienda mbele kidogo na kituo kilochofuata (kinaitwa garage) aliingia mama mmoja mtu mzima kidogo nilisita kumpisha siti maana nlikuwa nimechoka na najihisi kuumwa pia gari likiwa bado level siti zaidi yule mama tu ndo alisimama niliona isiwe tabu ngoja nimpishe Nilimuita akaja kuketi akashukuru pia. Vituo vilivyofuata gari ilijaza abailia hakuna mfano hadi mtu inakubidi usimame na mguu moja ndio upate balance, nakumbuka kama kituo cha tano aliinuka mwingne karibu yangu nikakaa na hivyo nikawa sija loose chochote, mfukoni nilikuwa na 35,500 tu. Nikampa konda 500/= ikarudi 100.
Kisa kipo hivi Wakati nashuka ile pesa 35,000 niliiacha kwenye siti nikashuka nikiwa sina hili wala lile' niliitwa na yule mama akaniambia naona umeacha pesa yako hapa. Nikajicheki kweli sina pesa yoyote mfukoni. Nilijiuliza mara mbili mbili imekuwaje huyu pekee ndiye aliyeona hizi pesa nikakumbuka ule wema niliomfanyia haya ndiyo malipo yake.
Nilimshukuru maana nilikuwa sina kitu sio cash wala mpesa nipo mweupe nimebakia mapumbu matupu.
Kila wema hulipwa! Hujui ni lini au nani atalipa.
Sent using
Jamii Forums mobile app