Ambao huwa tunaangalia tamthiliya/movies zilizotafsiriwa tukutane hapa

Khantwe

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
59,415
Reaction score
119,473
Habari,
Najua mtasema huku hawapo ila naamini wenzangu na mimi wapo maana kwenye msafara wa kenge na mamba wamo.
Startimes wameturahisishia sana tusiojua kizungu, kwa sasa sisi tunaangalia
A sister's revenge (Chinese)
Waaris (Indian)
Village boy (Indian)
Wild flower (wafilipino)
Hizi zote zinaoneshwa channel ya St Swahili (kasoro Village boy)
Wewe unaipenda ipi? Nani humpendi? Nani unampenda?

Note:
Ninazungumzia zile ambazo wamechomeka sauti za kiswahili, yaani unaona mchina anazungumza kiswahili sio zile za kina Rufufu

Uzi tayari
 
Ahahahahaaa... Mi simo..
CC: shemelaake Khantwe
 
Kama nilishindwa kuangalia sultan sidhani Kama nitaweza kufuatilia tamthilia iliyotafsiriwa
 

Kuna ambayo DJ Afroo ametafsiri?
 
Ndiyo zinawafanya mpaka mnaunguza mboga jikoni, unarudi toka job unakuta majirani (wanawake) wamejazana sebuleni kufuatilia sultani, yaani hata Kama ulikuwa na Nia ya kuangalia kipindi mhimu inabidi uufyate tu, halafu unakula na kuwaacha tu.

But so funny! Wanawake bhana[emoji16][emoji16][emoji16][emoji28]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…